WIKI
iliyopita nilifungua somo muhimu sana kwa wanaume ambalo ni tatizo la
wanaume kuwahi kufika kileleni au kuwahi kumaliza katika tendo la ndoa
ikiambatana na uchovu wa ghafla wa kushindwa kurejea katika tendo na
mbaya zaidi usingizi pia huwakumba ghafla wakiwaacha wenza wao bado na
hisia kali za mapenzi.
Nilisema
ninaliita hili kuwa ni janga la kitaifa kwa kuwa kliniki kwangu
nimekuwa nikipokea wanaume wengi wenye tatizo hili lakini sababu ya pili
ya kuliita janga la kitaifa ni kuwepo wanaume wengi wenye tatizo hili
lakini hawajui kama ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine, lina
vyanzo vyake na tiba kamili kwa hiyo wengi wao hubaki na tatizo hili
likiwatafuna mpaka uzeeni.
Niliishia kwenye vyanzo na nilianza kwa kusema kwamba:
1.
Kujichua (masturbation ) ni chanzo kikubwa cha tatizo hili kwa kuwa mara
nyingi mtu mvulana anapoanza mchezo huu huwa anafanya kwa siri na
huhitaji amalize mapema kabla hajakutwa na watu na tabia hii hujijenga
kisaikolojia na kujikuta mvulana/mwanaume huyu huendelea na tatizo hili
la kuwahi kumaliza hata katika tendo halisi.
Madhara haya ya kujichua huambatana na uume kusinyaa, kuwa mfupi na
mwembamba tofauti na awali. Tafiti za kitabibu zinatabanaisha kwamba
kila mwanaume aliyewahi kujichua mfululizo katika maisha yake ni lazima
atakumbwa na tatizo hili kipindi fulani cha maisha yake.
2. Msongo wa mawazo. Wanaume wengi hasa wa mijini hujikuta katika
msongo wa mawazo usiokwisha na hivyo hurudi nyumbani kutoka katika
shughuli zao za kila siku.
3. Kukamia kupita kiasi.
4. Uoga/kutojiamini. Hali hii huwakumba wanaume wasio na taarifa
kwamba wao ni wakamilifu, wanaume ambao hujidharau na kujiona hawafai
kuwa na mwanamke wa hadhi fulani
5. Dr. Abrahams James wa Saint
Magreth Clinic iliyopo Washington Dc katika andiko lake liitwalo `Sex
and Fertility` la mwaka 2011,
amesisitiza kwamba wanaume kutofuatilia majarida /elimu au taarifa za
mbinu mbalimbali za kumwezesha mwanaume kuchelewa kufika kileleni,
huchangia kuendelea kwa tatizo hili kwa kizazi na kizazi na hasa kwa
wanaume wa mijini ambao wengi wao miili yao haifanyishwi mazoezi kwa
kazi zao au hata kwa kupanga muda.
Anasisitiza kwamba mwanaume anapopata ufahamu huu hupata hali ya kujiamini na hivyo kushiriki kikamilifu katika tendo la ndoa.
6. Ulaji mbovu ukiambatana na uzito kupita kiasi.Ulaji wa siku hizi
hasa mijini ni mbovu kwa maana ya kwamba watu hujali rangi na ladha na
si viini lishe vilivyomo na pia hawajali matokeo mabovu ya ulaji huo.
Inashangaza kuona wasomi wengi na watu wenye uwezo kifedha wakiongoza
kwa ulaji mbovu unaosababisha pamoja na mambo mengine, kukumbwa na
tatizo la wanaume kuwahi kufikia mshindo na kutoweza kuendelea mpaka
masaa mengi au hata siku zaidi ya moja zipite.
7. Kutofanya mazoezi na mwili kuwa legevu bila stamina ya kutosha.
Inashangaza kuwaona watu wenye uzito mkubwa kupita kiasi au wazee au
wagonjwa ndio wapo mazoezini asubuhi na jioni.
Hiki ni kiashiria kwamba watu hufanya mazoezi pindi wanaposhauriwa na
daktari kwamba hiyo ndiyo suluhu ya wao kuendelea kuishi ilhali mazoezi
yanapaswa kuwa sehemu ya maisha ili pamoja na faida zingine, yawasaidie
wanaume kuchelewa kufika kileleni hasa wale ambao bado hawajakumbwa na
tatizo hili.
No comments:
Post a Comment