Friday 3 April 2015

Na hizi ndio nchi zilizoongoza kwa kunyonga watu mwaka 2014, Afrika nani anaongoza?

Unaambiwa idadi ya watu walionyongwa imekua na tofauti katika mwaka 2013 na 2014 kwenye nchi mbalimbali duniani ambapo mwaka 2013 watu waliohukumiwa kunyongwa ni 778 kote duniani tofauti na mwaka 2014 ambapo walionyongwa ni 607 imeshuka kwa ongezeko la sawa na asilimia 22.
Sawa idadi ya walionyongwa imeshuka lakini taarifa ikufikie tu kwamba idadi ya waliohukumiwa kunyongwa kwa mwaka 2014 ni 2,466 ni idadi ambayo imepanda kwa asilimia 28 ukilinganisha na mwaka 2013.
Kwenye hii picha hapa chini ndio unapata picha kamili nchi zilizoongoza kwa kunyonga watu mwaka 2014.
AmnestyNchi iliyoshika namba 1 ni Iran kwa kunyonga watu 289, ya pili ni Saudi Arabia kwa kunyonga watu 90, ya tatu ni Iraq ambayo ilinyonga watu 61, ya nne ni Marekani iliyonyonga watu 35 na Yemen ndio wamechukua namba 5 kwa kunyonga watu 22.
Nchi ambazo zina idadi ndogo ya watu walionyongwa ni Singapore iliyonyonga watu wawili, Gaza/West Bank watu wawili, Japan watu watatu.
Kwenye nchi za Afrika zilizoongoza kwa kunyonga watu mwaka 2014 ni Sudan 23, Egypt ndio imeshika namba 2 kwa kunyonga watu 15, Somalia 14 wamechukua namba tatu na wa mwisho kwenye hii list Equatorial Guinea walionyonga watu 9.

Ripoti ya kinachoendelea Chuo kilichovamiwa Kenya.. Idadi ya vifo yaongezeka #RIP

Ke Attack
Hali bado sio shwari kwa wenzetu Kenya, jana taarifa kubwa iliyoripotiwa kwa siku nzima kutoka kwenye nchi hiyo ni ishu ya kuvamiwa kwa Chuo Kikuu cha Garissa, ambacho kiko karibu na mpaka wa nchi ya Somalia.
Wavamizi hao walivamia jana katika Chuo hicho na kuua walinzi wawili na baadae kuendelea kuwashambulia wanafunzi.
Idadi ya vifo iliyoripotiwa mpaka sasa ni watu 147, askari na Vikosi vya Jeshi la nchi hiyo wameendelea kuzunguka maeneo ya Chuo hicho.
Shambulio hili ni kubwa, linafananishwa na tukio la uvamizi wa Shopping Malls za Westgate, Nairobi September 2013 ambalo lilisababisha vifo vya watu 67 na wengine zaidi ya 170 kujeruhiwa.
Mpaka sasa wavamizi waliouawa ni wanne na mmoja wao amekamatwa.
.
Ramani ya Majengo ya Garissa University College.
Zaidi ya wanafunzi 500 walifanikiwa kutoka salama katika eneo hilo la Chuo.

Monday 10 November 2014

HESHIMA PESA SHIKAMOO KELELE::WAKE ZA WATU OVYOO!

Stori: Dustan Shekidele, Morogoro
Mtu mzima ovyoo! Akina mama watatu ambao ni wake za watu, wanaounda Kundi la Heshima Pesa Shikamoo Makelele lenye maskani yake maeneo ya Mawenzi mjini hapa wanadaiwa kuwachefua baadhi ya watu baada ya kujitoa fahamu na kumwaga ‘lazi’ hadharani na mbaya zaidi mbele ya watoto wadogo.
Wake za watu wanaofahamika kama mama Sabra mwenye kigauni kifupi cha draftidrafti, mama Jenifa mwenye kimini cha njano na mama Athuman wakijitoa ufahamu mbele ya mahrusi.
Kwa mujibu wa ‘shujaa’ wetu, tukio hilo la aibu ya aina yake lilijiri juzikati  kwenye Ukumbi wa Savoy mjini hapa ambapo wanawake hao walialikwa kuburudisha kwenye sherehe ya harusi ya jirani yao.
Wanawake hao waliofahamika kwa majina ya watoto wao ni pamoja na mama Sabra aliyekuwa akibinuka, aliyevalia kigauni kifupi cha draftidrafti.Mwingine alikuwa ni mama Jenifa aliyekuwa ametupia kimini cha njano na mama Athuman ambao kwa pamoja walikuwa na vikuku miguuni.
Mama Sabra mwenye kigauni kifupi cha draftidrafti, mama Jenifa wakimwaga radhi ukumbini.
Mtu wetu huyo aliyekuwa ndani ya ukumbi huo aliwashuhudia wanawake hao wakimwaga lazi mara baada ya MC kuita kundi lao kwa ajili ya kutoa zawadi.
Mama Sabra akijiachia kwa raha zake bila kujali matokeo.
Kabla ya kutoa zawadi, wamama hao walimfuata DJ na kumtaka kuwawekea wimbo wowote wa Taarab, wakawekewa ambapo wakiwa na zawadi yao ya doti moja ya khanga, walipita mbele ya maharusi kwa mbwembwe zote na baada ya kukabidhi zawadi hiyo ndipo balaa lilipoanza.
Mama Sabra akizidi kumwaga radhi bila uoga.
Huku wakipeana nafasi na mara nyingine kulaliana, walikuwa wakijibinua na kuonesha staili za chumbani huku ‘makufuli’ yakiwa nje, jambo lililotibua harusi hiyo.
Ilifika hatua hadi baadhi ya wazazi wakawa wanawaziba watoto wasione, jambo lililosababisha wazazi wa pande zote mbili (wakwe) kununa pamoja na MC wa shughuli hiyo, MC Chuma ambaye baada ya kuona wanawake hao wanazidi kuvua nguo aliwashtua:
Wakwe wakichoshwa na tabia chafu za wanawake hao.
“Ninyi mnaofanya hivyo mjue OFM (Oparesheni Fichua Maovu ya Global Publishers) ipo humu ndani, sasa  kesho au keshokutwa msitafute lawama.”
Pamoja na angalizo hilo la MC, ndiyo kwanza wanawake hao walipozidi kumwaga lazi ikawa ni laana tupu.
Baada ya pati kukamilika, mwanahabari wetu aliwafuata wanawake hao na kuwahoji kulikoni kumwaga radhi kiasi hicho? Msikie huyu:
Huyu ni Mama Sabra aliyekuwa alimwaga radhi waziwazi.
“Kazi yetu ni kuchangamsha sherehe. Shughuli ilipooza lakini baada ya sisi kuserebuka, ilibadilika, habari ndiyo hiyo,” alisema mama Sabra.

HABARI::WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA

IMG_5158
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri mara baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga Mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu na wa pili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).

* Ataka iundwe timu kufuatilia utekelezaji wa Azimio la Arusha 2014

Na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema inahitajika dhamira ya kweli kutoka kwa wadau wote katika kutekeleza Azimio la Arusha la kukabiliana na ujangili na kuendeleza hifadhi za wanyama katika nchi za Afrika Mashariki na zilizo Kusini mwa Ikweta.


Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya kufunga mkutano wa kikanda wa siku mbili uliojadili mbinu za kupambana na biashara haramu ya wanyamapori ulioandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Arusha, Waziri Mkuu alisema: “Suala hili linataka uwajibikaji wa pamoja. Mashirika na taasisi, wananchi na viongozi sote kama wadau wakuu, kila mmoja anapaswa kushiriki vita hii kama kweli tunataka tuitokomeze.”

“Kwenye hili Azimio la Arusha na nyie waaandishi wa habari pia mna sehemu yenu mmetajwa... wamesema wanatafuta jinsi ya kushirikiana na vyombo vya habari ili visaidie kutoa elimu kwa jamii kama njia ya kuelimisha umma,” alisema.

Waziri Mkuu aliwaeleza waandishi hao kwamba Azimio hilo lina vipengele 20 ambavyo vinataka utekelezaji katika ngazi ya nchi mojamoja, ngazi na kanda na ngazi ya kimataifa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

IMG_5160
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akielekea kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu, wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

“Nimepata faraja kwamba mkutano huu haukuisha kijumlajumla tu, bali umekuja na maazimio 20 ambayo yametengwa kwa ajili yetu sisi wa ndani, mengine yanahusisha ushirikiano wa kikanda na yako mengine yanawahusisha wadau wa maendeleo,” alifafanua.

Ili kutekeleza azimio hili, nimeshauri iundwe timu itakayoshirikisha vyombo vingi zaidi badala ya kuiachia Wizara ya Maliasili na Utalii peke yake. Timu hii ikutane kila baada ya miezi sita ili kufuatilia utekelezaji wa maazimio haya na ikibidi Waziri atoe taarifa bungeni kuhusu utekelezaji huo,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema, akizungumza na washiriki wa mkutano huo wakati wa kuufunga, Waziri Mkuu alisema kuwepo kwa watu wa ngazi tofauti kwenye mkutano huo ni kielelezo tosha cha umakini wao na nia thabiti ya kutokomeza ujangili katika ukanda huu.

IMG_5167
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli kwenye chumba maalum cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.


“Tumeanzisha vita, tusisahau kwamba bado kuna kazi kubwa mbele yetu na vita haijaisha. Tuzidishe mapambano katika sehemu tatu: kwenye nchi unakofanyika ujangili, nchi ambazo nyara zinapitishwa na nchi zinazopokea ama kununua hizo nyara,” alisema Waziri Mkuu.

“Nakubaliana nanyi kwamba hakuna nchi inayoweza kukabili suala la ujangili ikiwa peke yake. Tunahitaji tuwe na sera mahsusi, sera ya pamoja ya kutuunganisha na kutuongoza wakati tukitekeleza Azimio hili kwa kusaidiana na wadau wa maendeleo,” alisema.

Alisema Azimio hilo litaipa kazi ya ziada ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo kazi kubwa itakuwa ni kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wa wa Azimio hilo unakuwa wa ufanisi.
Jumla ya nchi tisa zimetia saini azimio hilo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5170
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mbunge wa Kahama, James Lembeli, huku Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akifurahi jambo ndani ya chumba cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye chumba cha mikutano.

IMG_5169
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli (wa pili kulia) kwenye chumba cha mapumziko baada ya kuwasili ukumbi hapo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

IMG_5182
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, kwenye chumba maalum cha mapumziko.

IMG_5253
Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akimkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kushoto) kufunga rasmi mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Magese Mulongo, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu, Mbunge wa Kahama, James Lembeli na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli wakiwa meza kuu.

IMG_5264
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akizungumza na wadau waliohudhuria mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014 wakati akifunga rasmi mkutano huo wa siku mbili.

IMG_5198
Mwakilishi wa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania akichukua taswira za baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea mkutanoni hapo.

IMG_5197
Baadhi ya wadau mbalimbali walioshiriki mkutano huo.

IMG_5236
Baadhi ya wawakilishi kutoka nchi tisa wakitia saini Azimio la Arusha la kukabili ujangili mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5205
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa kwenye ufungaji wa mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.

IMG_5224
Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke, akizungumza kwa niaba ya serikali ya Ujerumani.

IMG_5212
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu wakati wa ufungaji rasmi wa mkutano huo uliodumu siku mbili jijini Arusha.
IMG_5268
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiondoka ukumbini hapo mara baada ya kuufunga rasmi mkutano huo.

HABARI::WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA

IMG_5158
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri mara baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga Mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu na wa pili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).

* Ataka iundwe timu kufuatilia utekelezaji wa Azimio la Arusha 2014

Na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema inahitajika dhamira ya kweli kutoka kwa wadau wote katika kutekeleza Azimio la Arusha la kukabiliana na ujangili na kuendeleza hifadhi za wanyama katika nchi za Afrika Mashariki na zilizo Kusini mwa Ikweta.


Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya kufunga mkutano wa kikanda wa siku mbili uliojadili mbinu za kupambana na biashara haramu ya wanyamapori ulioandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Arusha, Waziri Mkuu alisema: “Suala hili linataka uwajibikaji wa pamoja. Mashirika na taasisi, wananchi na viongozi sote kama wadau wakuu, kila mmoja anapaswa kushiriki vita hii kama kweli tunataka tuitokomeze.”

“Kwenye hili Azimio la Arusha na nyie waaandishi wa habari pia mna sehemu yenu mmetajwa... wamesema wanatafuta jinsi ya kushirikiana na vyombo vya habari ili visaidie kutoa elimu kwa jamii kama njia ya kuelimisha umma,” alisema.

Waziri Mkuu aliwaeleza waandishi hao kwamba Azimio hilo lina vipengele 20 ambavyo vinataka utekelezaji katika ngazi ya nchi mojamoja, ngazi na kanda na ngazi ya kimataifa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

IMG_5160
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akielekea kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu, wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

“Nimepata faraja kwamba mkutano huu haukuisha kijumlajumla tu, bali umekuja na maazimio 20 ambayo yametengwa kwa ajili yetu sisi wa ndani, mengine yanahusisha ushirikiano wa kikanda na yako mengine yanawahusisha wadau wa maendeleo,” alifafanua.

Ili kutekeleza azimio hili, nimeshauri iundwe timu itakayoshirikisha vyombo vingi zaidi badala ya kuiachia Wizara ya Maliasili na Utalii peke yake. Timu hii ikutane kila baada ya miezi sita ili kufuatilia utekelezaji wa maazimio haya na ikibidi Waziri atoe taarifa bungeni kuhusu utekelezaji huo,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema, akizungumza na washiriki wa mkutano huo wakati wa kuufunga, Waziri Mkuu alisema kuwepo kwa watu wa ngazi tofauti kwenye mkutano huo ni kielelezo tosha cha umakini wao na nia thabiti ya kutokomeza ujangili katika ukanda huu.

IMG_5167
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli kwenye chumba maalum cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.


“Tumeanzisha vita, tusisahau kwamba bado kuna kazi kubwa mbele yetu na vita haijaisha. Tuzidishe mapambano katika sehemu tatu: kwenye nchi unakofanyika ujangili, nchi ambazo nyara zinapitishwa na nchi zinazopokea ama kununua hizo nyara,” alisema Waziri Mkuu.

“Nakubaliana nanyi kwamba hakuna nchi inayoweza kukabili suala la ujangili ikiwa peke yake. Tunahitaji tuwe na sera mahsusi, sera ya pamoja ya kutuunganisha na kutuongoza wakati tukitekeleza Azimio hili kwa kusaidiana na wadau wa maendeleo,” alisema.

Alisema Azimio hilo litaipa kazi ya ziada ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo kazi kubwa itakuwa ni kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wa wa Azimio hilo unakuwa wa ufanisi.
Jumla ya nchi tisa zimetia saini azimio hilo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5170
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mbunge wa Kahama, James Lembeli, huku Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akifurahi jambo ndani ya chumba cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye chumba cha mikutano.

IMG_5169
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli (wa pili kulia) kwenye chumba cha mapumziko baada ya kuwasili ukumbi hapo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

IMG_5182
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, kwenye chumba maalum cha mapumziko.

IMG_5253
Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akimkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kushoto) kufunga rasmi mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Magese Mulongo, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu, Mbunge wa Kahama, James Lembeli na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli wakiwa meza kuu.

IMG_5264
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akizungumza na wadau waliohudhuria mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014 wakati akifunga rasmi mkutano huo wa siku mbili.

IMG_5198
Mwakilishi wa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania akichukua taswira za baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea mkutanoni hapo.

IMG_5197
Baadhi ya wadau mbalimbali walioshiriki mkutano huo.

IMG_5236
Baadhi ya wawakilishi kutoka nchi tisa wakitia saini Azimio la Arusha la kukabili ujangili mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5205
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa kwenye ufungaji wa mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.

IMG_5224
Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke, akizungumza kwa niaba ya serikali ya Ujerumani.

IMG_5212
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu wakati wa ufungaji rasmi wa mkutano huo uliodumu siku mbili jijini Arusha.
IMG_5268
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiondoka ukumbini hapo mara baada ya kuufunga rasmi mkutano huo.

HABARI::WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA

IMG_5158
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri mara baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga Mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu na wa pili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).

* Ataka iundwe timu kufuatilia utekelezaji wa Azimio la Arusha 2014

Na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema inahitajika dhamira ya kweli kutoka kwa wadau wote katika kutekeleza Azimio la Arusha la kukabiliana na ujangili na kuendeleza hifadhi za wanyama katika nchi za Afrika Mashariki na zilizo Kusini mwa Ikweta.


Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya kufunga mkutano wa kikanda wa siku mbili uliojadili mbinu za kupambana na biashara haramu ya wanyamapori ulioandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Arusha, Waziri Mkuu alisema: “Suala hili linataka uwajibikaji wa pamoja. Mashirika na taasisi, wananchi na viongozi sote kama wadau wakuu, kila mmoja anapaswa kushiriki vita hii kama kweli tunataka tuitokomeze.”

“Kwenye hili Azimio la Arusha na nyie waaandishi wa habari pia mna sehemu yenu mmetajwa... wamesema wanatafuta jinsi ya kushirikiana na vyombo vya habari ili visaidie kutoa elimu kwa jamii kama njia ya kuelimisha umma,” alisema.

Waziri Mkuu aliwaeleza waandishi hao kwamba Azimio hilo lina vipengele 20 ambavyo vinataka utekelezaji katika ngazi ya nchi mojamoja, ngazi na kanda na ngazi ya kimataifa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

IMG_5160
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akielekea kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu, wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

“Nimepata faraja kwamba mkutano huu haukuisha kijumlajumla tu, bali umekuja na maazimio 20 ambayo yametengwa kwa ajili yetu sisi wa ndani, mengine yanahusisha ushirikiano wa kikanda na yako mengine yanawahusisha wadau wa maendeleo,” alifafanua.

Ili kutekeleza azimio hili, nimeshauri iundwe timu itakayoshirikisha vyombo vingi zaidi badala ya kuiachia Wizara ya Maliasili na Utalii peke yake. Timu hii ikutane kila baada ya miezi sita ili kufuatilia utekelezaji wa maazimio haya na ikibidi Waziri atoe taarifa bungeni kuhusu utekelezaji huo,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema, akizungumza na washiriki wa mkutano huo wakati wa kuufunga, Waziri Mkuu alisema kuwepo kwa watu wa ngazi tofauti kwenye mkutano huo ni kielelezo tosha cha umakini wao na nia thabiti ya kutokomeza ujangili katika ukanda huu.

IMG_5167
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli kwenye chumba maalum cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.


“Tumeanzisha vita, tusisahau kwamba bado kuna kazi kubwa mbele yetu na vita haijaisha. Tuzidishe mapambano katika sehemu tatu: kwenye nchi unakofanyika ujangili, nchi ambazo nyara zinapitishwa na nchi zinazopokea ama kununua hizo nyara,” alisema Waziri Mkuu.

“Nakubaliana nanyi kwamba hakuna nchi inayoweza kukabili suala la ujangili ikiwa peke yake. Tunahitaji tuwe na sera mahsusi, sera ya pamoja ya kutuunganisha na kutuongoza wakati tukitekeleza Azimio hili kwa kusaidiana na wadau wa maendeleo,” alisema.

Alisema Azimio hilo litaipa kazi ya ziada ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo kazi kubwa itakuwa ni kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wa wa Azimio hilo unakuwa wa ufanisi.
Jumla ya nchi tisa zimetia saini azimio hilo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5170
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mbunge wa Kahama, James Lembeli, huku Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akifurahi jambo ndani ya chumba cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye chumba cha mikutano.

IMG_5169
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli (wa pili kulia) kwenye chumba cha mapumziko baada ya kuwasili ukumbi hapo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

IMG_5182
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, kwenye chumba maalum cha mapumziko.

IMG_5253
Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akimkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kushoto) kufunga rasmi mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Magese Mulongo, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu, Mbunge wa Kahama, James Lembeli na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli wakiwa meza kuu.

IMG_5264
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akizungumza na wadau waliohudhuria mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014 wakati akifunga rasmi mkutano huo wa siku mbili.

IMG_5198
Mwakilishi wa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania akichukua taswira za baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea mkutanoni hapo.

IMG_5197
Baadhi ya wadau mbalimbali walioshiriki mkutano huo.

IMG_5236
Baadhi ya wawakilishi kutoka nchi tisa wakitia saini Azimio la Arusha la kukabili ujangili mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5205
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa kwenye ufungaji wa mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.

IMG_5224
Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke, akizungumza kwa niaba ya serikali ya Ujerumani.

IMG_5212
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu wakati wa ufungaji rasmi wa mkutano huo uliodumu siku mbili jijini Arusha.
IMG_5268
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiondoka ukumbini hapo mara baada ya kuufunga rasmi mkutano huo.