Sunday 19 October 2014

IRINGA>>MSIGWA: KINANA AMETUSAIDIA KUPONDA MAWE MAGUMU

 Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Dkt.Yahaya Msigwa akiongea na waandishi wa habari jana mjini Iringa kuhusu ziara ya siku sita ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana aliyeifanya mkoani hivi karibuni. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)
NA FRIDAY SIMBAYA
Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Dkt. Yahaya Msigwa amesema kuwa ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana aliyeifanya mkoani hapa imesaidia kuponda mawe magumu na kutuachia mawe madogo madogo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu mawe magumu hayo ndani ya chama katibu mwenezi huyo wa mkoa alisema kuwa ziara ya siku sita ya kinana kutatua kero mbalimbali zilizokuwa zinakikabili chama hicho.
Alisema kuwa kiongozi huyo wa kitaifa aliwapa fursa wananchi kuuliza maswali ambayo yamesadia kuibua changamoto mbalimbali na wao kama chama mkoa kero hizo wanaendelea kuzifanyia kazi.
“Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana  na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye walikuwa katika ziara ya siku sita mkoani Iringa kuimarisha uhai wa chama, kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi,” aliongeza katibu mwenezi wa mkoa huyo.
Aidha, katibu mwenezi huyo wa mkoa alisisitiza viongozi kuwa karibu na wananchi ili kuweza kusikiliza matatizo yao kuliko kukaa ofisini kuhusu kuletewa kero hizo ofisini.
Alisema kuwa katibu mkuu kinana alisisitiza umuhimu wa kuweka viongozi wanaokubalika na wananchi pamoja kuheshimu moani ya wananchi ili kusimamisha viongozi  wanaokubalika  kwa kufuata katiba, kanuni na taratibu za chama.
Wakati huohuo, Katibu Mwenezi CCM Mkoa, Dkt. Msigwa aliwaasa wananchi kujiandikisha katika daftari ya mpigakura ili wawezekushiriki kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa na ule Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Alisema kuwa ni lazima wananchi wa hakikishe wanachagua viongozi wazuri wanaotokana na chama cha CCM ili kuweza kudumisha amani na utulivu wa nchi yetu  kama tunu aliyetuachia Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Nyerere.

No comments:

Post a Comment