Monday 27 October 2014

MAHAFALI::2228 WAHITIMU KATIKA MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO KIKUU CHA IRINGA


Afisa mahusiano wa chuo cha Kikuu cha Iringa, Agness Kitundu akimpaa maelekezo mlinzi wakati wa mahafali ya chuo hicho.
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIUMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU
WAHITIMU


HOTUBA YA MAKAMU MKUU WA CHUO PROF. NICHOLAS T. A. BANGU KWENYE MAHAFALI YA KWANZA YA
CHUO KIKUU CHA IRINGA
TAREHE 25 OKTOBA 2014
1.    UFUNGUZI
Mheshimiwa Mkuu wa Chuo, Mh. Judge Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani,
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Iringa, Bishop Dr. O. Mdegela,
Wakuu wa Serikali na Taasisi mbalimbali,
Wafanyakazi wa Chuo,
Wanafunzi mliohitimu,
Wanafunzi mnaoendelea,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana.
2.    KUKARIBISHA WAGENI:
Awali ya yote kwa heshima na taadhima naungana na Mwenyekiti wa Baraza kuwakaribisha katika mahafali haya ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Iringa kuwashukuru kwa kuhudhuria.
3.    PONGEZI:
Natoa pongezi kwa wanakamati ya maandalizi walioongozwa na Bwana Aloyce Suleiman na wengine waliohusika kwa namna mbalimbali kukamilisha maandalizi.
Nawapongeza wafanyakazi wote (wanataaluma na waendeshaji) kwa ujumla na kwa mmoja mmoja kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kipindi cha mwaka 2013/14 na kutufikisha kuwa na mahafali ya kwanza.
Nawapongeza wahitimu wote kwa kufikia hatua hiyo.  Ni dhahiri kuwepo kwenu hapa chuoni kumechangia kuwajenga kielimu, na ninaamini kumechangia kuwajenga kiroho na kimaadili na kuwa mtatumia nyenzo hizo zote kuchangia katika juhudi za kitaifa za kuboresha hali ya maisha ya Watanzania na walimwengu wote kwa ujumla.
4.    SHUKURANI
Katika kipindi cha mafunzo 2013/2014 wafuatao ni baadhi ya waliotufadhili kwa hali na/au mali:
·        Wazazi/walezi wa wanafunzi,
·        Serikali ya Tanzania kupitia taasisi yake ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB),
·        Serikali ya Umoja wa Ulaya,
·        Serikali ya Finland,
·        Serikali ya Uholanzi kupitia Shirika lake la NUFFIC,
·        Chuo Kikuu cha Nelson Mandela,
·        Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kupitia LMC,
·        Shirikisho la Kilutheri la Amerika (ELCA):  kupitia Synod ya Eneo la Mt. Paul (St. Paul ares Synod),
·        Uongozi wa ngazi mbali mbali za Mkoa wa Iringa 
5.     MATUKIO- KIPEKEE MWAKA WA MASOMO 2013/2014
5.1.        Mradi wa Hifadhi ya Utamaduni, Utalii na Maendeleo endelevu Kanda ya Kusini mwa Tanzania (Cultural Heritage conservation, Tourism and Sustainable Development in Southern Highlands of Tanzania.
5.1.1               Mradi huu unafadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya (EU)
5.1.2               Katika Utekelezaji tuna washirika 8 na baadhi yao ni Chuo Kikuu cha Cottingen Ujerumani, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ofisi ya Manispaa ya Iringa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa.
5.1.3               Shughuli zilizofanyika mwaka huu zimo katika makundi matano:
5.1.3.1       Utafiti na uchoraji ramani.
5.1.3.2       Maandalizi ya upatikanaji Boma la Kijerumani toka Serikalini na mipango ya ukarabati.
5.1.3.3       Maandalizi ya kibiashara utamaduni na promotion
5.1.3.4       Kuhusisha wananchi katika biashara ya utalii wa utamaduni
5.1.3.5       Kwa kushirikiana na vyuo vya Ujerumani, Finland kujenga uwezo wa kitaaluma: vijana 9 wamepata ufadhili kwa ngazi ya Masters (M.A) na 1 kwa digrii ya falsafa (Ph.D) lengo ni kufanya utafiti wa utalii wa utamaduni kuwa moja ya agenda ya Chuo cha Iringa.
5.2.        Kuelekea kuwa Chuo Kikuu cha Kizazi cha Tatu (SGU) kizazi hiki kinatofautina na vizazi viwili vya awali kwa kufanya ujasiliamali kuwa sehemu ya taaluma. Tendo la kuingiza ujasiliamali linaenda kwa hatua:
5.2.1.            Kuelimisha waalimu na wanafunzi nafasi ya ujasiliamali katika taaluma.
5.2.2.            Kubadili mfumo wa ufundishaji kuwa mwanafunzi ndio kitovu cha kujenga elimu na pili kuhamasisha tambuzi zote sita za ubongo; kukumbuka (remembering), kuelewa (understanding), kuchambua (analyzing), kuchanganya (synthesizing), kutumia (Application) na kubuni (Creating)
5.3.        Kuwahamasisha wanafunzi kuanzisha makapuni ya kuzalisha mali wakingali choni kwa maana hiyo kuelekeza mafunzo wanayoyapata kwenye kampuni wanaoijenga. Hadi sasa shughuli kadhaa zimeanzishwa na zinaendelezwa na wanafunzi waliohitimu. Kwa mfano SAMIS inafanya shughuli za supermarkets na PESSI inayoshughulika na kuzungusha plastics na kadhalika.
Hatua ya nne ambayo imeanza mwaka huu ni kuimarisha uundaji wa kampuni kutumia nadhania inayoitwa Team Academy. Mwaka huu wa masomo tuna wanafunzi 40 ambao watafanya masomo yao kwa utaratibu huo sambamba na mafunzo ya kawaida na kuanzia mwakani mfumo wa masomo yao utakuwa unaelekea kwenye kampuni ambazo wameamua kuziunda na kuziendeleza.
Mafunzo ya namna hii yalizinduliwa huko Finland. Mwaka 1993 na hivi sasa umesambaa katika nchi kadhaa duniani Netherlands Hungary Argentina hususani Finland, France, UK, Spain, China, Brazil, Austelia). Kwa Africa chuo chetu kitakuwa cha kwanza. Juzi nilipata fursa ya kuelezea mfumo huu kwenye Mkutano wa NEPAD. Wajumbe wengi walifurahia na chuo cha Africa Zimbabwe na Jomo Kenyata wametukarisha tukawaeleze zaidi.
5.4.        Kitengo cha Kilimo (Institution of Agriculture) na kitengo cha mitaji midogo (Inst. Of Microfinance) vimepata ufadhili wa Kitengo cha America kinachoitwa Iringa Hope USA ufadhili wa Jengo litakalokuwa na vyumba vya ofisi na vyumba vya mijadala ya wakulima kuhusu stadi za kilimo na fedha.
5.5.        Kitengo cha Marekani cha ubadilishaji wa elimu kimefungua tawi katika Chuo cha Iringa. Kwa mwaka huu tawi lilipokea wanafunzi 5 mwezi wa Januari na mwezi huu hivi sasa wameongezeka hadi 20. Kila kundi limekuwa hapa kwa miezi mitatu na wanajifunza mambo mbali mbali. Matumaini yetu ni kwamba wanafunzi wetu wataweza kwenda katika vyuo huko Marekani.
6.     WAHITIMU:
Mheshimiwa Kaimu Mkuu wa Chuo,
Katika mwaka 2013/2014 jumla ya wanafunzi 2228 wanahitimu kwa mchanganuo ufuatao:
1.
Astashahada ya Theolojia (Certificate in Theology)
20
2.
Stashahada ya Theolojia (Diploma in Theology)
12
3.
Shahada ya Kwanza ya Tauhidi (Degree of Bachelor of Divinity –  (BD)
5
4.
Astashahada ya Ushauri Nasihi (Certificate in Counseling Psychology)
7
5.
Stashahada ya Ushauri Nasihi (Diploma in Counseling Psychology)
40
6.
Shahada ya Kwanza ya Ushauri Nasihi (Degree of Bachelor of Counselling (BCOUNS)
37
7.
Astashahada ya Utawala na Biashara (Certificate in Business Administration – CBA)
125
8.
Astashada ya Ununuzi na Usimaminzi wa Mali (Certificate in Procurement and Material Management)
24
9.
Stashahada ya Utawala na Biashara (Diploma in Business Administration)
353
10. 
Stashahada ya Sayansi katika Uhasibu na Fedha (Diploma in Accounting and Finance)
23
11.
Stashahada ya Ununuzi na Usimaminzi wa Mali (Diploma in Procurement and Material Management)
40
12.
Shahada ya Kwanza ya Sayansi katika Uhasibu na Fedha (Bachelor of Science in Accounting and Finance - BAF )
39
13.
Shahada ya Kwanza ya Uchumi na Fedha (Degree of Bachelor of Science in Economics and Finance)
34
14.
Shahada ya Kwanza ya Utawala wa Biashara (Degree of Bachelor of Business Administration)
88
15.
Astashahada ya Sheria (Certificate in Law)
52
16.
Stashahada  ya Sheria (Diploma in Law)
33
17.
Shahada ya Kwanza ya Sheria (Bachelor  in Law
166
18.
Astashahada ya Sanaa ya Maendeleo ya Jamii (Certificate in Community Development
65
19.
Stashahada ya Sanaa ya Maendeleo ya Jamii (Diploma in Community Development)
48
20.
Shahada ya Kwanza ya Sanaa ya Maendeleo ya Jamii (Bachelor of Arts in Community Development)
198
21.
Shahada ya Kwanza ya Anthropolojia ya Utamaduni na Utalii (Bachelor of Arts in Cultural Anthropology and Tourism)
94
22.
Astashahada ya Sanaa ya Uwanahabari (Certificate in Arts in Journalism)
7
23.
Stashahada ya Sanaa ya Uwanahabari (Diploma in Arts in Journalism)
6
24.
Shahada ya Kwanza ya Sanaa ya Uwanahabari (Bachelor of Arts in Journalism)
68
25.
Astashahada ya Sayansi na Teknolojia ya Habari (Certificate in Information Technology)
62
26.
Stashahada ya Sayansi na Teknolojia ya Habari (Diploma in Information Technology)
36
27.
Shahada ya Kwanza ya Sayansi katika Teknolojia ya Habari (Degree of Bachelor of Science in Information Technology)
43
28.
Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Hisabati (Bachelor of Education Mathematics)
58
29.
Shahada ya Kwanza ya Elimu katika ….. (Bachelor of Education – Arts)
274
30.
Stashahada ya Uzamili ya Elimu Ualimu (Postgraduate Diploma in Education – Teaching)
26
31.
Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Maendeleo ya Jamii na Usimamizi wa Miradi (Master of Arts in Community Development and Project Management)
38
32.
Shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Saikolojia (Master of Science in Counseling Psychology)
2
33.
Shahada ya Uzamili ya Elimu – Sanaa (Master of Education –  Arts)
3
34.
Shahada ya Uzamili ya Sheria katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Master of Law in Information and Communication Technology Law
15
35.
Shahada ya Uzamili katika Mfumo wa Sheria za Jinai za Kimataifa na Haki za Binadamu (Master of Laws in International Criminal Justice and Human Rights (LLM-ICJ-HR)
9
36.
Shahada ya Uzamili ya Anthropolojia ya Utamaduni na Utalii (Master of Arts in Tourism, Culture and Society)
6
37.
Shahada ya Uzamili ya Utawala na Biashara (Master in Business Administration)
72
JUMLA
2228
Prof. NICHOLAUS . T. A. Bangu
VICE CHANCELLOR

No comments:

Post a Comment