Wednesday 1 October 2014

MWANAMKE AKIOLEWA KUNA ULAZIMA AITWE JINA LA UKOO WA MUMEWE?

KARIBUNI tena na tena, wasomaji wa safu hii motomoto inayozungumzia maisha kwa ujumla. Lengo sa safu hii ni kuwekana sawa katika mazingira ya maisha ya uhusiano tunayoishi.
Mada yetu ya leo imetokana na kuzidi kushamiri kwa hoja kwamba je, mwanamke akishaoelewa kuna umuhimu wa kuitwa kwa jina la ukoo wa mumewe?Mfano, awali mwanamke aliitwa Julieth Thomas Rupia, akaolewa na Samuel Aloyce Masumbuko. Je, Julieth akishaolewa aitwe Julieth Thomas MASUMBUKO?
Tangu miaka na miaka, wanawake wamekuwa wakibadili majina yao ya mbele na kuachana na ya wazazi wao kwa kutumbukiza ya waume zao, hasa ya ukoo ndiyo zaidi.
Lakini miaka ya hivi karibuni, baadhi ya wanawake wameachana na dhana au utaratibu huo, wanatoa hoja kwamba hawaoni sababu ya kutumia majina ya ukoo wa waume zao baada ya kuolewa.
MADAI YAO
Nilibahatika kuzungumza na baadhi ya wanawake waliotoa hoja ya kupinga matumizi ya majina ya waume zao.
Wengi walisema kuwa, kwa ndoa za siku hizi ni kujisumbua tofauti na zamani.
“Unajua ndoa za sasa tofauti na zile za mababu na mabibi zetu, wao walikuwa wanadumu katika ndoa, lakini sisi siyo. Ndiyo maana tunahofia kwamba, leo ukiitwa kwa jina la mumeo, watu wakikuzoea, kesho ukaachika na kurudi kwenye jina lako unakuwa mgeni katika jamii.
“Hali hii inasababisha wanawake wengi siku hizi tukiolewa tunapenda kuendelea kuitwa kwa majina ya ukoo wa wazazi wetu,” anasema mama Patrick, mkazi wa Bunju jijini Dar.
KUNA UKWELI?
Labda hili ndiyo swali la msingi kuliko yote, kwamba kuna ukweli wowote kuwa ndoa za siku hizi hazitoi fursa kwa mke kutumia jina la mumewe?
Ni kweli, ndoa za sasa si za kutilia maanani wala kujiapizia hata kidogo. Zipo ndoa zinazovunjika miezi michache baada ya kufungwa, nyingine mwaka mmoja tu. Ukikutana na ndoa zina miaka mitano ni majaliwa au neema ya Mungu.NI KIGEZO?
Si kigezo hata kidogo, ni jukumu la wanandoa wenyewe kutengeneza mazingira safi na salama ili hali ya kuachana isiwepo. Lakini tangu miaka na miaka, mwanamke akiolewa hupaswa kutumia jina la ukoo wa mumewe.
MR & MRS INATOA MWANGA
Haya ni maneno yanayojulikana na wengi, wakiamini kuwa ni bibi na bwana! Ni sawa kabisa, lakini ukifuatilia tafsiri ya Kiingereza, Mr au Mister ni bwana! Ili liendelee lazima liwe Mr fulani. Mfano, Mr Ndauka (bwana Ndauka).
Mrs ni bibi lakini kwa maana ya mke (Kenya wanatumia sana mke kumwita bibi). Lakini pia mrs katika tafsiri ya Kiingereza lina maana mke wa… Mfano, Mrs Kapipi (mke wa Kapipi). Lakini neno Mr haliwezi kutafsirika kuwa ni mume wa…yaani haiwezekani kuwa mr Margaret ikawa ni mume wa Margaret.
Ufafanuzi huo unaonesha kuwa asili ya wanawake kuitwa kwa majina ya waume zao ilitokana na kutambulishwa kuwa mke wa fulani (mrs).
MIFANO YA VIONGOZI
Wako wake wa marais, mawaziri nakadhalika wanaitwa kwa kutumia majina ya ukoo wa waume zao. Mfano, mama Salma Kikwete, mama Tunu Pinda, Anna Kilango Malecela, Anna Kajulumo Tibaijuka, Asharose Mtengeti Migiro, mama Hillary Rodham Clinton.
MAJINA KUFA
Ndoa kama inavyotakiwa kuwa na uvumilivu ili idumu ndiyo silaha ya matumizi ya majina ya waume lakini wapo wanawake walioachwa kwa talaka au kufiwa, waliendelea kujulikana kwa majina ya waume zao bila kuathiri maisha. Mfano, Winnie Madikizela Mandela na Graca Simbine Machel.
MADHARA YAKE SASA!

No comments:

Post a Comment