Wednesday 22 October 2014

NDANI::MADANSA WA DIAMOND WAKAMATWA,SARE ZA JESHI....


Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond' (wa pili kutoka kushoto), akiwa na madansa wake pamoja na Nay wa Mitego wakitoa burudani katika tamasha la Serengeti Fiesta 2014, Leaders Club jijini Dar.
Madansa wa Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinum wamekamatwa leo na wapo Kituo cha polisi cha Oyster Bay, Dar kwa kuvaa sare za JWTZ.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond'.
Wakati huohuo polisi  wanaendelea kumtafuta bosi wao, Nasibu Abudul ' Diamond Platinumz' kwa mahojiano naye kwa kuvaa sare za Jeshi hilo katika Tamasha la Serengeti Fiesta, lililofanyika Leaders Club, Dar usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.
Meneja wa  Diamond, Babu Tale, hakupatikana kuzungumzia suala hili, juhudi za kumtafuta zinaendelea.
(HABARI NA MUSA MATEJA/GPL)

No comments:

Post a Comment