| 
 ........................................................................................................ 
 
MBUNGE   wa  jimbo  wa  jimbo la 
 Kalenga  Godfrey  Mgimwa  ajipongeza kutumia kiasi cha  zaidi ya Tsh 
milioni 68 kwa ajili ya  kufanikisha  utekelezaji wa ahadi  zilizotolewa
 na mbunge  aliyefariki Dr  Wiliam Mgimwa  kwa  asilimia 90 kwa  muda 
 wa  miezi mitatu pekee . 
 
Akizungumza na  wananchi  wa  kijiji 
 cha Mangalali   baada ya  kukamilisha ahadi ya bati 100 kwa ajili ya 
ujenzi wa  vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Lukwambe , mbunge 
Mgimwa  alisema  kuwa alianza  kutekeleza  ahadi hizo hata kabla ya 
 kuapishwa   bungeni na  hadi sasa  bado asilimia 10 pekee ya 
utekelezaji wa ahadi zilizoachwa na mbunge  aliyefariki  dunia mwanzoni 
mwa mwaka  huu marehemu Dr Mgimwa ambae alikuwa ni babake mzazi. 
 
" Ni jambo la kumshukuru  mwenyezi Mungu
  kwani ahadi  zilizokuwa  zimetolewa na  mbunge  aliyefariki  dunia 
marehemu Dr  wiliam Mgimwa  zilikuwa ni asilimia 100 na hadi 
mnanichangua  kuwa  mbunge ahadi  hizo  zilikuwa  bado kutekelezwa na 
ndio  sababu ya mimi   katika kampeni kutoahidi  ahadi mpya  zaidi ya 
 kuzipokea  zile  zilizoachwa na baba ambazo  kimsingi nilizipokea 
.......ila kwa sasa ahadi  hizo nimetekeleza kwa asilimia 90  bado 
asilimia 10 pekee ambazo hadi mwakani  nitakuwa nimezimaliza kikubwa 
naomba mzidi kuniombea  uzima" alisema  mbunge Mgimwa. 
 
Alisema  kuwa hakuweza  kuahidi ahadi 
mpya  wakati wa kampeni  hizo za uchaguzi mdogo  jimboni humo kutokana 
na kuwepo kwa ahadi nyingi ambazo  zilikuwa zimetolewa na mbunge 
 aliyepita na zilikuwa bado  kutekelezwa na muda  wa   utekelezaji 
 ulikuwa bado  hivyo aliamua  kuzichukua  zote kama  zilivyo na kuanza 
 kuzifanyia kazi moja baada  ya nyingine . 
 
Mbunge Mgimwa alisema  kuwa ahadi  hizo 
 zinazotekelezwa  ni  zile ahadi  binafsi ambazo mbunge  aliyepita 
alikuwa amezitoa ila  zipo ahadi mbali mbali ambazo zimo katika ilani ya
  CCM ambazo pia  zimeendelea  kutekelezwa  kwa  nguvu  kubwa . 
 
Hata
  hivyo  alisema kuwa ahadi ambazo  zimetekelezwa kwa asilimia 90 ambazo
 zilikuwa ni ahadi binafsi ni pamoja  na elimu ,afya na  uchangiaji wa 
 vikundi  vya Vicoba pamoja na uanzishwaji wa  vikundi  hivyo pia katika
  sekta ya  michezo na huduma  nyingine  za kijamii kama  upelekaji wa 
umeme katika maeneo ya kata ya Mgama  na Magulilwa zoezi hilo 
 linaendelea ambayo   ahadi  hiyo ya umeme  ipo katika ilani ya CCM 
pamoja na zile za  huduma za maji vijijini ambazo baadhi ya maeneo mradi
 kata ya Maboga  na kata ya Lumuli wa maji  unatekelezwa . 
 
Pia  alisema  kuwa bado  anautamani 
 ubunge wa  jimbo  hilo la Kalenga kwa mwaka 2015 -2020   hivyo kamwe 
hatawaangusha  wana Kalenga kwa  kipindi  hiki  cha miaka miwili 
alichopewa  hadi 2010. 
 
" Ndugu  zangu hii nafasi ya  ubunge 
 mimi  nimeipata mwishoni ila sikutaka  kuwaangusha  nilitaka 
kuwaonyesha  utendaji  wangu na kamwe  sitakuwa mbali na ninyi  wananchi
  wangu  nitakuwa  bega kwa  bega  kuhakikisha jimbo la Kalenga linapata
 maendeleo na linakuwa ni  jimbo la mfano katika maendeleo  kule 
 bungeni kutokana na umri  wangu  wabunge  wananiita bwana mdogo ila 
 kiutendaji kweli  ni bwana mkubwa kwani kati ya wabunge zaidi ya 300 
bungeni  mimi ni mmoja kati ya  wabunge  tuliochanguliwa  kuingia katika
 kamati ya bunge ya bajeti ya  serikali " alisema mbunge Mgimwa . 
 
Awali katibu  wa mbunge huyo  Martine 
Simangwa  aliwaonya  wana CCM ambao  wameendelea  kujipitisha katika 
 jimbo  hilo na kuwa kwa kufanya hivyo ni kutowatendea haki  wananchi wa
  jimbo la Kalenga ambao kwa  sasa wameshikamana na  wapo tayari kuona 
 maendeleo na sio kampeni za  uchaguzi wa mwaka 2010. 
 
"  wapo  baadhi ya  wana CCM bila haya 
 wameendelea  kujipitisha kwa wananchi na  kuponda utendaji huu mzuri wa
 mbunge Godfrey Mgimwa ....sasa  wananchi  nawaombeni  sana 
msidanganyike na  watu hao kwa sasa mbunge ni Godfrey Mgimwa wakija na 
kuwapa  pesa chukueni ila msikubali kugawanywa kwa misingi ya pesa 
kubalini  kuungana katika misingi ya kimaendeleo" 
 
Kwa upande  wao  wananchi hao  walieleza
  kufurahishwa na utendaji mzuri wa mbunge  wao Mgimwa na  kuwa kamwe 
hawatakubali kudanganyika na kuwa  wamejipanga  kumchukulia  fomu 
mwakani  ili kuwaongoza vipindi  vingine viwili zaidi baada ya  kuona 
utendaji  wake mzuri. 
 
MWISHO | 
No comments:
Post a Comment