| Kigola akifurahi kabla kibao hakijageuka | 
| Nasifiwe Ponziano Miwoo mbele ya Waziri Nyalandu alipokuwa akihoji uadilifu wa mbunge wa Mufindi Kusini, Mendrad Kigola | 
SAKATA
 la  vibali vya uvunaji miti katika msitu wa Taifa wa Sao Hill Mufindi 
mkoani Iringa limemuweka pabaya mbunge wa  jimbo la Mufindi kusini 
Mendrad Kigola baada ya wapiga kura  wake kumgeuka mbele ya  waziri 
maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu  kuwa mbunge huyo ni mchochezi 
katika  sakata  hilo.
Katika
 mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Igowole juzi Kigola 
alimkaribisha waziri huyo huku akikosoa mgao wa vibali vya kuvuna miti 
katika msitu wa Taifa wa saohill ambao sehemu yake upo katika jimbo 
hilo, ulivyofanywa kwa vikundi vya wajasiriamali wa wilaya ya Mufindi.
Huku
 akipigiwa makofi ya mara kwa mara yaliyomfanya ashindwe kusimama sehemu
 moja wakati akiongea, Kigola alisema: “sina pingamizi dhidi ya watu na 
vijiji vilivyopata mgao wa mwaka huu.”
“Shida
 yangu ni mgao uliotolewa kwa vikundi vya wilaya ya Mufindi yenye 
majimbo mawili. Wakati jimbo langu la Mufindi Kusini vimepata vikundi 12
 kati ya 48, vingine vyote vilivyobaki vimetoka upande mwingine. 
Mheshimiwa waziri, nakuomba ulione hilo,” alisema.
Kauli
 ya Kigola ilitafsiriwa na baadhi ya watu waliokuwepo katika mkutano huo
 kwamba ilikuwa ikimpiga vijembe mbunge wa jimbo jirani la Mufindi 
Kaskazini, Mahamudu Mgimwa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na 
Utalii.
Taarifa
 zisizo rasmi kutoka ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya 
Mufindi zinadai kwamba Mgimwa na Kigola hawapikiki chungu kimoja ikiwa 
ni matokeo ya kinachoelezwa na walio jirani na wabunge hao kwamba mmoja 
wao ana wivu wa kisiasa dhidi ya mwenzake.
Taarifa
 hizo zisizo rasmi ambazo hata hivyo hazijawahi kutolewa ufafanuzi na 
Kigola mwenyewe zinadai kwamba amekuwa akimuonea wivu Mgimwa baada ya 
kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Naibu Waziri.
Wivu
 huo ndio umepelekea kuchochea chokochoko ya kuhoji uwiano wa mgao wa 
vibali vikiwemo vibali 48 vilivyotolewa kwa vikundi 48 vya wilaya ya 
Mufindi.
Hoja
 ya Kigola dhidi ya mgao wa vibali hivyo ilionekana ina mashiko kwa muda
 wote wa mkutano huo mpaka pale Waziri Nyalandu alipotoa ruksa kwa 
wananchi wa kijiji hicho cha Igowole kuuliza maswali.
Alikuwa
 Nasifiwe Ponziano Miwoo aliyechafua hali ya hewamara baada ya kupata 
nafasi ya kuuliza swali alilotoa kwa mtindo aliodai wa kujenga hoja ili 
wananchi wamuelewe.
Akinukuu vifungu kadhaa vya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano huku akioanisha na uadilifu wa mbunge huyo Miwoo alisema:
“Kuna
 haja ya kuoanisha hoja za mbunge huyu Kigola na uadilifu wake; na kuna 
haja ya kujua mali zinazomilikiwa na mbunge huyu ili tuone kama 
kunasababu kwa familia yake kupata kibali cha kuvuna miti wakati baadhi 
ya vijiji na vya wilaya ya Mufindi na wajasiriamali wake wakikosa,” 
alisema.
Alisema
 katika orodha ya wanufaika na vibali vya mwaka huu, jina namba 388 ni 
la mtoto wa Kigola anayesoma katika moja ya shule bora zilizoko wilayani
 Mufindi.
Alisema
 zipo dalili kwamba Kigola alitumia jina la mwanae huyo kupata kibali 
hicho jambo linalojenga mashaka dhidi ya uadilifu wake.
“Mheshimiwa
 Waziri tuna mashaka na huyu mtu na kama kila mwaka anajaza fomu 
inayoonesha mali anazomilikia. Kwanini jina la mwanae litumike,” Miwoo 
alisema huku waliokuwa wakimshangilia Kigola wakigeuza kibao na 
kumshangilia yeye.
 
No comments:
Post a Comment