Sunday 24 August 2014

CHRIS BROWN ANUSURIKA KIFO

CHRIS BROWN ANUSURIKA KIFO, SUGE KNIGHT AKIJERUHIWA KWA RISASI

 
Cris Brown akiwa Klabu 1OAK kabla ya vurugu kutokea.
 
Prodyuza mkongwe, Suge Knight amejeruhiwa tumboni na mkononi katika shambulio hilo.
MWIMBAJI Cris Brown amenusurika kuuawa katika shambulio la risasi ndani ya klabu ya usiku jijini Los Angeles ambapo prodyuza Suge Knight amejeruhiwa.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo katika klabu ya usiku iitwayo 1OAK iliyopo magharibi mwa Hollywood wakati wa shoo iliyokuwa ikiongozwa na Cris Brown kabla ya zoezi la utoaji Tuzo za VMA ambapo watu watatu wamejeruhiwa mmoja akiwa mahututi.
Suge Knight alipigwa risasi mara mbili tumboni na mkononi na kukimbizwa hospitali ambapo anaendelea na matibabu.
Mastaa wengine waliokuwepo kwenye klabu hiyo wakati tukio hilo likitokea ni pamoja na Justin Bieber, rappa The Game, Pia Mia, Tyson Beckford, Robert Ri'chard  na wengineo.
Indaiwa mlengwa mkuu katika shambulio hilo alikuwa Cris Brown.

No comments:

Post a Comment