Wananchi wa Kijiji cha Luvuyo Kata ya Madope wakimpokea Mbunge wao, Deo Filikunjombe kwa maandamano.
Wanachama
 wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi wa Kijiji cha Luvuyo 
kata ya Madope wakishirikiana jana na Deo Filikunjombe (kushoto) 
kuchimba mifereji ya maji katika barabara ya Luvuyo - Njombe yenye urefu
 wa Kilomita 6 ambayo inajengwa kwa ufadhili wa mbunge huyo kwa kiasi 
cha zaidi ya shilingi milioni 50.
Mbunge
 wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe akiwahutubia wananchi wa Luvuyo 
mara baada ya  kuzindua ujenzi wa barabara ya Luvuyo - Njombe.
Deo
 Filikunjombe akisafirishwa katika mkokoteni wa kukokotwa na ng'ombe 
baada ya wananchi wa  Luvuyo ambao awali walitishia  kuhama  wilaya ya 
Ludewa kuhamia Njombe kusikilizwa kilio chao  cha ubovu wa  miundombinu 
kwa  kuanza kujengewa barabara na mbunge huyo
 
No comments:
Post a Comment