Sunday 24 August 2014

HABARI NA PICHA:VIPI MBUNGE WAKO YUPO KAMA HUYU???

Wananchi wa Kijiji cha Luvuyo Kata ya Madope wakimpokea Mbunge wao, Deo Filikunjombe kwa maandamano.
Wanachama wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi wa Kijiji cha Luvuyo kata ya Madope wakishirikiana jana na Deo Filikunjombe (kushoto) kuchimba mifereji ya maji katika barabara ya Luvuyo - Njombe yenye urefu wa Kilomita 6 ambayo inajengwa kwa ufadhili wa mbunge huyo kwa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 50.
Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe akiwahutubia wananchi wa Luvuyo mara baada ya  kuzindua ujenzi wa barabara ya Luvuyo - Njombe.
Deo Filikunjombe akisafirishwa katika mkokoteni wa kukokotwa na ng'ombe baada ya wananchi wa  Luvuyo ambao awali walitishia  kuhama  wilaya ya Ludewa kuhamia Njombe kusikilizwa kilio chao  cha ubovu wa  miundombinu kwa  kuanza kujengewa barabara na mbunge huyo

No comments:

Post a Comment