Thursday 14 August 2014

KWANIN DR.SLAA NA MNYIKA WALITAKA KUDUNGULIWA....

Habibu Mchange Akana Tuhuma za Kuhusika Kulipua Helkopta iliyombeba Mnyika na Slaa

Written By Udaku Specially on Thursday, August 14, 2014 
Leo mchana katika mkutano wake na waandishi wa habari,Mchange amewashambulia waziwazi viongozi wakuu wa chama cha demokrasia na maendeleo na kuwatuhumu kuhiska na mauaji ya aliyekua mbunge wa CHADEMA Tarime,marehemu Chacha Wangwe,kisha kumkana mtu aliyehusika na mauaji hayo Deus Mallya,wakati alikuwa mjumbe katika kamati iliyokuwa chini ya John Mnyika,na rafiki wa Mnyika lakini Mnyika kumkana hajawai hata kumuona.

Kisha kawataja Lissu,Mbowe na Slaa kuajiri vijana na kuwalipa kuwatesa vijana wanaoonyesha kuiunga mkono CCM katika kampeni mbalimbali za chama,hasa kwa kumwagia watu tindikali.

Pia amesema Lissu ni mbinafsi na fisadi aliyedhurumu fedha za miradi ya mazingira,na kujenga nyumba ya ghorofa Tegeta,Mbowe anahujumu mamilioni ya CHADEMA,na Slaa akihujumu fedha za chama kulipia mkopo wa NSSF.