Saturday 16 August 2014

MAN UNITED YALAMBWA 2-1 KWA SWANSEA ' OT'

Matokeo ya Manchester Utd vs Swansea City haya hapa

IMG_6442.JPG
Ligi kuu ya Uingereza maarufu kama Barclays Premier League imeanza rasmi leo hii kwa mchezo wa ufunguzi kati ya Manchester United dhidi ya Swansea City.
Mchezo huo uliomalizika hivi punde katika dimba la Old Trafford, United imeendelea pale pale ilipoachia msimu uliopita kwa kupoteza mechi ya kwanza kwenye dimba la nyumbani kwa kipigo cha magoli 2-1.
Swansea ndio walikuwa wa kwanza kuona nyavu za United kwenye dakika ya 28 kipindi cha kwanza kupitia Ki Sung, kabla ya Wayne Rooney kusawazisha dakika 58.
Huku United wakiwa wanatafuta goli la pili, kinda Tylor Blackett akapoteza mpira kwa Wilfred Bony na kusababisha goli la pili lilofungwa na
Sigurdsson.
Mpaka dakika 90 zinamalizika Swansea 2-1 Man uTD.
Hiki ndio kipigo cha kwanza kwa United katika mechi ya ufunguzi wa EPL tangu mwaka 1972.
Man Utd (3-4-1-2): De Gea; Jones, Smalling, Blackett; Lingard (Januzaj (24min), Fletcher, Herrera (Fellaini 67), Young; Mata; Hernandez (Nani 46), Rooney.
Subs: Kagawa, Michael Keane, Amos, James.
Goal: Rooney 53.
Booked: Blackett, Young.
Swansea (4-2-3-1): Fabianski; Rangel, Amat, Williams, Taylor (Tiendalli); Ki, Shelvey; Routledge, Sigurdsson; Dyer (Montero 67), Bony (Gomis 77).
Subs: Tiendalli, Montero, Tremmel, Bartley, Richards, Sheehan.
Booked: Dyer, Taylor, Shelvey.
Goals: Ki 28, Sigurdsson 72.
Referee: Mike Dean (Wirral).