Sunday 24 August 2014

MSIBA:MASHABIKI WAMUUA MCHEZAJI ALGERIA..

MASHABIKI WAMUUA MCHEZAJI ALGERIA

MCHEZAJI kutoka Cameroon amekufa baada ya kupigwa kichwani wakati mashabiki waliokereka waliporusha mawe mwisho wa mechi ya Ligi ya Algeria.
Albert Ebosse enzi za uhai wake.
Albert Ebosse, aliyekuwa na umri wa miaka 24, ndiye aliyefunga mabao mengi katika Ligi ya Algeria msimu uliopita.
Alirushiwa kitu wakati mashabiki walipokerwa kuwa timu yake, JS Kabylie, iliposhindwa kwa mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa nyumbani, Tizi Ouzou.


Marehemu ndiye aliyefunga bao hilo pekee kwa timu yake.
Wizara ya mambo ya nchi ya Algeria imeamrisha uchunguzi ufanywe kuhusiana na kifo hicho.

No comments:

Post a Comment