Monday 25 August 2014

SIASA SI HASA:::USICHEZE VIBAYA NA SIASA....MAKONDA ROHO JUU JUU

Hali Ndani ya CCM ni Mbaya, Roho ya Makonda Inatafutwa Usiku na Mchana

Udaku Specially on Monday, August 25, 2014
Kwa mujibu wa nzi wetu anayecheza viunga vya Lumumba akitutiririshia habari zote mpaka mapigo ya mioyo ya akina Kinana, Nape na wana CCM wote walio juu ya maharamia wote, anatujuza kuwa huko CCM moto wake sio wa kitoto,

Makonda anatuhumiwa kumtusi Lowassa hadharani tena akivaa mwavuli wa UVCCM ilihali hana cheo chochote ndani ya Chama,

Baada ya matusi yale ya nguoni ambayo aliyaporomosha huyu dogo nikuwa mashitaka rasmi yalifikishwa kwenye kamati ya maadili na Lowassa,

Sheria ya CCM inasema kama mtu hayupo kwenye kikao husika cha mashitaka ni mwiko kujadiliwa,

Sasa siku ambayo tayari kamati kuu ilijipanga kumwajibisha (kumvua uanachama) kwenye kikao chake cha mwezi jana, Makonda alikimbilia Ufaransa akitoroshwa na Ridhiwan Kikwete na Bernard Membe kwa madai kuwa anakwenda kwenye semina ya masuala ya katiba,

Baada ya kutokuwepo kwenye kikao husika huvyo iliamuliwa suala hilo lisogezwe kwenye kikao kitakachofuata hasa hiki cha dharula juzi,

Kikao cha juzi tena wakati akiwa tayari kajulishwa kwa barua toka kwa katibu mkuu, Makonda tena alisafiri kwenda Ujerumani kwa madai ya kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya yake, safari hii Membe akihusika kuratibu na taarifa za kuaminika nikuwa hakwenda Ujerumani bali aliongozana na Membe kwenye ziara yake huko Mashariki ya Mbali ambako aliendelea kubaki huko hata baada ya Membe kurudi mpaka cc ilipomaliza kikao chake juzi,


Upande wa Lowasa wanaoonekana ndio wenye nguvu wameapa kuwa ni lazima waikate "roho" ya kisiasa ya Makonda kwa kuhakikisha anafukuzwa uanachama.

No comments:

Post a Comment