Friday 29 August 2014

TANZIA!TANZIA!!!!TAARIFA ZA MSIBA WA MAREHEMU MARIAM JARUFU.

TAARIFA ZA MSIBA WA MAREHEMU MARIAM JARUFU.
Friday, August 29, 2014




Marehemu Mariam Jarufu amefikwa na umauti baada ya kupata ajali ya gari maeneo ya Gairo juzi usiku 26 August 2014. DC wa Mvomero alikuwa anapita akaona gari imedondoka upande na kama kuna mama ahangaika...ndio kusimama kukuta gari imegonga mti upande damu zimetapakaa mbele kote...akapigia simu kituo cha karibu police waje na ambulance. Wakafika mapema Mariam alikuwa hai akiongea na dereva. Nyuma watoto wazima na mama mdogo...wakatolewa kupandishwa ktk ambulance. Mariam aliumia sana kichwani na mdogo wake miguu na mwili kidogo. Ila kufika katika ambulance just 10mins drive akafariki Mariam na dereva kupoteza fahamu mpaka jana asubuhi.

Kwa watu wa UK
KUTOKANA NA MSIBA WA NDUGU YETU Mariam Jarufu ULIOTOKEA TANZANIA KWA AJALI YA GARI TUNAPENDA KUWAFAHAMISHA KUWA MSIBA UPO NO.32 COLNE TINKERS BRIDGE MILTON KEYNES MK 6 3 DJ. WOTE MNAKARIBISHWA KUTOA SHUKRAN NA RAMBIRAMBI ZENU ASANTENI

Kwa watu wa Tanzania:
 Msiba uko Mbezi Beach unapita shule ya Mwalimu Nyerere sehemu inaitwa Naguruwe ukiulizia utaonyeshwa wanazika Ijumaa makaburi ya Kinondoni

Hii ndo gari iliyo chukua uhai wa mwenzetu
Naomba tujumuike kwa pamoja kuifariji familia hii kwa msiba huu mzito. Wale watu wa UK ambao tuko Bongo na mgependa kwenda msibani basi tuwasiliane twende kwa pamoja leo jioni tukatoe pole zetu.
R.I.P MARIAM.

No comments:

Post a Comment