Saturday 6 September 2014

AJALI AJALIIII....MSAFARA WA MAALIM SEIF WAPATA AJALI.

September 6, 2014
Moja ya gari ambalo lilikuwa kwenye msafara wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Katibu Mkuu wa Cuf, Maalim Seif Sharif Hamadi baada ya kupata ajali, Misungiwi, Mwanza leo.
Hili ni gari lingine ambalo lenye usajili namba T397ANU nalo lilihusika katika ajali hiyo leo.
Keria ya moja ya magari yaliyopata ajali ikiwa chini baada ya kufyatuka baada ya ajali.
Baadhi ya wananchi wakishuhudia msafara wa Maalim Seif, mara baada ya ajali.
Msafara wa Maalim Seif ukijiandaa kuondoka mara baada ya magari mawili kati ya saba yaliyokuwa kwenye msafara kupata ajali.
Katibu wa CUF Wilaya ya Nyamagana, Rehema Mwenda amejeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Rufaa Bugando (kulia) na muonekano wa gari (kushoto) baada ya ajali katika wilaya ya Misungwi, jijini Mwanza.
Mkuu wa kitengo cha habari Wilaya, Mh Shido ambae pia ni Mwenyekiti wa Mtaa Utemini Kata ya Mirongo amejeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Rufaa Bugando.
Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamadi.
Habari zinasema msafara wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamadi umepata ajali ukihusisha magari mawili ya msafara wa kiongozi huyo ambayo jumla yake yalikuwa saba yalipogongana na lori lenye tela.

Akizungumza na mtandao huu, Mkurughenzi wa Habari wa CUf, Adam Kambaya alisema  Viongozi wawili wa CUF, katibu wa wilaya ya Nyamagana na mwenyekiti wa mtaa wa Nyamagana  ambao hakuwataja majina wamelazwa katika Hospitali ya Bugando kwa matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment