Thursday 16 October 2014

DODOMA::NEC:HATUNA TIME KUJADILI UKAWA



Na Joyce Kasiki,Dodoma

CHAMA cha Mapinduzi kimesema hakina muda wa kujadili watu waliokataa ama kukubali mchakato wa Katiba mpya katika Bunge Maalum la Katiba.

Kauli hiyo imetolewa  leo  na Katibu w itikadi na Uenezi wa Chama hicho Naoe Nnauye wakati akizungumza na waandishi kuhusiana na vikao vya Halmashauri Kuu ya CCM vinavyoendelea mjini hapa.

Alisema chama hakina sababu ya kufanya hivyo keani lengo lilikuwa ji kuoatikaana kwa katiba na tayari imepatikana.

Alisema eanaofai  kwamba vikao hivyo vitajadili  watu waliokuwa wakitaka mchakato usitishwe wana uwezo mdogo wa kufikiri.

"Sisi hatuwezi kujadili watu,keani hakuna msingi wala tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla,sisi tunajadili hoja.

"Hakuna muda wa kujadili watu ,sisi tunajadili   hoja,chama hakina muda wa kujadili watu,bali kinatakiwa kujafili ni tulipotoka,tulipo na tunapikwenda,kujadili watu hakusaidii   nchi ,chama wala mchakato wenyewe wa katiba." alisema Nape

Alisema ,wanaogukiri vika hivyo vya juu vy achama hicho vitajadili watu, wanatumia akili ndogo kufikiri,ili mradi mchakato ulifanyika vizuri na katiba imepatikana  kwa nini tujadili  watu,hoja za msingi ni kujadili mambo ya kulijenga  taifa letu

"Kujadili watu hata sisi akili yetu itakuwa siyo nzuri sana, sula la nani alikataa na nani alikubali hiyo haina msingi kwa sasa." alisema Nape

Pia alisema kikao cha Kamati kuu kilichofanyika juzi kimefanya uteuzi Wa  makatibu wa wilaya 27  wa CCM.


Kuhusiana na ucahguzi wa serikali za mitaa,alisema pia chama hicho kumejipanga kuhakikisha kinashinda kea kishindo.

No comments:

Post a Comment