| Sehemu ya watu waliojitokeza katika mkutano huo | 
| Wakionesha ishara ya chama chao | 
CHAMA
 cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimelitaka jeshi la Polisi 
kudhibiti misafara mirefu ya magari na pikipiki, na aina yoyote ya 
maandamano wakati wa mapokezi ya katibu mkuu wa  Chama cha Mapinduzi 
(CCM) Abdulahman Kinana wakati wa ziara yake mkoani Iringa .
Kauli
 ya Chadema  imekuja  ikiwa ni siku takriba tatu kabla ya kuwasili 
Kinana Oktoba 6-11  mwaka huu kuanzia ziara yake mkoani Iringa 
 Kwa
 mujibu wa taarifa  kwa  vyombo  vya habari zilizotolewa na CCM mkoa 
Kinana ataambatana na Katibu Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nnape 
Nauye wanatarajia kufanya ziara ya kukijenga chama hicho na kukagua 
utekelezaji wa Ilani ya CCM katika wilaya zote za mkoa wa Iringa wakati 
wa  ziara  hiyo.
Akiwahutubia
  juzi wananchi wa kata ya  Kihesa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la 
Chadema (BAVICHA) Patrick Ole Sosopi alisema  wamesikitishwa na  jeshi 
la polisi  kuzuia mapokezi yake mkoani Iringa huku  wakitambua wazi kuwa
 ni haki ya  wanachama  kumpokea  kiongozi  wao ila polisi  waligoma 
kutoa kibali  zaidi ya kuruhusu mkutano wa hadhara pekee.
| Akiwa na Makamu Mwenyekiti Bavicha, Patrick Ole Sosopi | 
Alisema
 wakati wakijiandaa kuchukua Dola wanataka kuona wanashindana katika 
uwanja sawa wa kisiasa kwahiyo hawatakubali kuona jashi la Polisi 
linaruhusu maandamano katika misafara ya Kinana wakati kwao linakataa.
Sosopi
 aliyekuwa na Mchungaji Peter Msigwa wakitokea jijini Dar es Salaam 
kulikofanyika chaguzi mbalimbali za kitaifa za chama hicho, walipokelewa
 katika eneo la Igumbilo na viongozi wachache wa chama hicho baada ya 
Polisi kudaiwa kuwazuia wafuasi wao kuwapokea kwa misafara ya magari, 
bodaboda na maandamano.
“Tumetii
 maelekezo ya Polisi, vijana wetu wa bodaboda wamezuiwa kutupokea; ili 
haki itendekea tunataka Kinana na timu yake watakapoingia mjini Iringa, 
misafara yao isiwe na maandamano ya watu, pikipiki wala magari,” alisema
 Mchungaji Msigwa katika mkutano wao mkubwa uliofanyika katika kata ya 
Kihesa mjini Iringa.
Mchungaji
 Msigwa alisema watashangaa na kuchukua hatua endapo Polisi itairuhusu 
CCM kuwa na maandamano na misafara ya magari na pikipiki.
 
No comments:
Post a Comment