Friday 29 August 2014

MANJI ACHARUKA....SUALA LA OKWI KWENDA SIMBA

SUALA LA OKWI KUSAINI SIMBA, MANJI ACHARUKA..

August 29, 2014
Manji akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
Wanahabari wakisikiliza kwa makini.
Kikao kikiendelea.
Mwenyekiti wa Yanga (Manji) akisisitiza jambo, kushoto ni Makamu wake, Clement Sanga.
Msistizo ukiendelea.
... Akionesha kidole kutoa mfano.
Kocha Marcio Maximo (kushoto) akizungumzia kuimarika kwa timu yake Visiwani, Zanzibar.
BAADA ya jana uongozi wa timu ya Simba chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope, kutangaza kumsainisha mshambuliaji, Emmanuel Okwi, raia wa Uganda, uongozi wa Yanga kupitia mwenyekiti wake, Yusuph Manji, mchana huu nao umetoa tamko rasmi la kumshitaki mchezaji huyo kwa shirikisho la soka nchini (TFF) pamoja na viongozi wa Simba na Klabu hiyo.
Katika mashitaka hayo Yanga imemshitaki Okwi, Simba na viongozi wake kwa kuvunja mkataba wakati mgogoro wa mchezaji huyo na Yanga ukiwa haujapatiwa ufumbuzi. Manji amesema katika madai hayo wanadai fidia ya dola milioni mia tano za Kimarekani.
Wakati huohuo, kocha wa kikosi hicho Mbrazil Marcio Maximo ameelezea kuimarika kwa kikosi chake kwenye kambi ya wiki mbili waliyofanya Visiwani Unguja na Pemba.

No comments:

Post a Comment