Monday 27 October 2014

SHARIA:::wanawake wa Saudia waamua

Najla Hariri akiendesha gari kinyume na sheria inayomzuia kufanya hivyo
Harakati za kutetea haki za wanawake nchini Saudi Arabia kutaka na wao wapewe haki ya kuendesha magari kama wanaume zashika kasi kubwa, sasa wanaadhimisha mwaka mmoja wa kupinga amri ya kwatazo kwa wanawake wasiendeshe magari na wanawake wanapinga na kuendesha magari kinyume na amri waliowekewa.
Kwenye mitandao ya kijamii kumetolewa miito kadhaa ya kuwataka wanawake wapinge amri hiyo kwa wingi na waendeshe magari,wanaharakati wanaopinga amri hiyo wameiambia BBC kuwa harakati zao zinaendelea vizuri na mwito umepokelewa vyema ingawa mwaka huu utatumika kuongeza uelewa zaidi juu ya suala hilo.
Nayo mamlaka ya Saudi Arabia imetoa onyo kali na kuwataka wasaudia wote wasijihusishe na mgomo huo,na mmoja kati ya wanaharakati ambaye ana ushawishi mkubwa ameelezea mgomo huo uloanza mwaka wa jana kuwa umeitia hofu kubwa serikali ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment