Saturday 11 October 2014

SIASA IRINGA::KATIBU MKUU WA CCM AIMALIZA CHADEMA NYOLOLO, LEO KUUNGURUMA IRINGA MJINI

Katika mkutano uliofanyika kijiji cha Nyololo  aliyekuwa Katibu wa CHADEMA  Kijiji cha Igowole Bw. Josephat Sibadi Soda amerejea CCM  baada ya uongozi wa chama hicho kutomlipa madeni ya vifaa mbalimbali alivyochukua madukani wakati wa ujenzi wa mnara wa marehemu Daud Mwangosi aliyeuwawa wakati wa mapambano ya jeshi la polisi na wafuasi wa CHADEMA mwaka jana uliojengwa katika kijiji cha Nyololo yeye akiwa mkandarasi na mbunfu wa mnara huo.2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma mara baada ya kuwasili katika mashamba ya chai ya Ngwazi wilayani Mufindi kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana kulia  na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa ,Ittikadi na Uenezi wakishiriki kuchuma chai katika shamba la chai la Ngwazi wilayani Mufindi.1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kumwagilia maji katika bustani ya miche ya miti ya mbao katika vitalu vya kuotesha miti vya Umoja wa Vikundi vya Kijamii vya Kigamboni mjini Mafinga.13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Nyololo Njiapanda kata ya Nyololo wilayani Mufindi.15Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ili aongee na wananchi wa kata ya Nyololo.14Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa ,Ittikadi na Uenezi  akiwahutubia wananchi wa kata ya Nyololo wilayani Mufindi katika mkutano uliofanyika uwanja wa Nyololo Njiapanda.
16Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Nyololo Njiapanda kata ya Nyololo wilayani Mufindi.18Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa ,Ittikadi na Uenezi  akimkaribisha aliyekuwa Katibu wa CHADEMA  Kijiji cha Igowole Bw. Josephat Sibadi Soda aliyerejea CCM leo baada ya uongozi wa chama hicho kutomlipa madeni ya vifaa mbalimbali alivyochukua madukani wakati wa ujenzi wa mnara wa marehemu  Daud Mwangosi aliyeuwawa wakati wa mapambano ya jeshi la polisi na wafuasi wa CHADEMA mwaka jana uliojengwa katika kijiji cha Nyololo19Aliyekuwa Katibu wa CHADEMA  Kijiji cha Igowole Bw. Josephat Sibadi Soda akikabidhi kadi yake pamoja na wanachama wa chama hicho 27 kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanabaada ya kurejea CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Nyololo Njiapanda. 20Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi alizokabidhiwa na wanachama wa CHADEMA  baada ya kurejea CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Nyololo Njiapanda. 21Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi  pamoja na benderaalizokabidhiwa na wanachama wa CHADEMAbaada ya kurejea CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Nyololo Njiapanda. 22Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongoza wana CCM waliojiunga na chama hicho kula kiapo mara baada ya kukabidhiwa kadi zao katika kiutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Nyololo Njiapanda wilayani Mufindi.23Waimbaji wa kwaya ya CCM Band wakiimba katikia mkutano huo.24Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiserebuka pamoja na wana CCM mbalimbali mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo.25Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa ,Ittikadi na Uenezi  wa tatu kutoka kulia na Katibu wa CCM wilayani Mufindi Ndugu Miraji Mtaturu wakipiga picha na waimbaji wa CCM Bandi waliotumbuiza katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment