Tuesday, 16 September 2014

IKIZIDI::Sumaye: Rushwa ikizidi CCM nitajiondoa

Waandishi wa habari waandamizi wa gazeti la Mwananchi wakifanya mahojiano na Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye, nyumbani kwake Kiluvya, mkoani Pwani. Picha na Venance Nestory 
Na Joyce Mmasi, Mwananchi
Sumaye, ambaye alipewa adhabu ya kudhibitiwa kwa miezi 12 kwa kosa la kuanza kampeni za urais mapema, alisema msimamo wake wa kupinga rushwa na tabia yake ya kujishirikisha kwenye mambo ya kijamii vinaweza kuwa sababu ya kutuhumiwa kufanya kampeni na baadaye kupata adhabu hiyo.
Dar es Salaam. Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema iwapo misingi ya uchaguzi ndani ya CCM italalia kwenye rushwa, hataendelea kuwa mwanachama na kuonya kuwa tatizo hilo limefikia pabaya na litakiangusha chama hicho.
Sumaye, ambaye alipewa adhabu ya kudhibitiwa kwa miezi 12 kwa kosa la kuanza kampeni za urais mapema, alisema msimamo wake wa kupinga rushwa na tabia yake ya kujishirikisha kwenye mambo ya kijamii vinaweza kuwa sababu ya kutuhumiwa kufanya kampeni na baadaye kupata adhabu hiyo.
Alionya kuwa vurugu zinazotokea sasa, hasa kwenye mikoa ya Kusini si ajali, bali hasira za wananchi dhidi ya viongozi wao ambao alisema wamejitenga baada ya kupata madaraka na hivyo wananchi wanatumia kila nafasi wanayoipata kuwaadhibu.
Katika mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili, Sumaye ambaye alijitokeza kwenye kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005 lakini hakupitishwa na CCM, alisema hawezi kuendelea kuwamo kwenye chama endapo kitachagua viongozi kwa rushwa.
“Suala si kama mimi nagombea au sigombei… Hata kama sigombei. Kama nitajiridhisha mwenyewe kuwa huyu amefika pale (amechaguliwa) kwa sababu ya rushwa, sitakuwapo sehemu hiyo (kwenye chama hicho), hata kama sigombei,” alisema Sumaye katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Kiluvya, takribani kilomita 30 kutoka jijini Dar es Salaam.
Sumaye, ambaye ndiye waziri mkuu pekee aliyemaliza awamu mbili za jumla ya miaka 10 bila ya kuondolewa, alikuwa akijibu maswali kuhusu mustakabali wake ndani ya CCM ambayo anadai imetawaliwa na rushwa. Maswali hayo na majibu yake yalikuwa:
Waandishi: Mwanzo ulisema rushwa inapokithiri kuna watu wanaweza wakatoka kwenye chama. Inavyoonekana katika mazungumzo yetu haya, wewe ni mtu ambaye unaichukia sana rushwa. Unafikiri, hivi (rushwa) inavyoendelea na labda kwenye uchaguzi wa mwakani itakuwa hivyo, unaweza siku moja ukatoka CCM?
Sumaye: Hilo nafikiri nilishawahi kulisema… nilisema kama misingi ya uchaguzi kwenye Chama Cha Mapinduzi italalia kwenye rushwa, mimi sitakuwa sehemu ya hiyo. Hilo nilishalisema na wala sibahatishi. Sasa suala si kama mimi nagombea au sigombei, hata kama sigombei. Lakini… kama nitajiridhisha mwenyewe kuwa huyu amefika pale (amechaguliwa) kwa sababu ya rushwa, sitakuwapo sehemu hiyo. Hata kama sigombei.
Waandishi: Utakuwa radhi kusema sipo mahali hapa?
Sumaye: Sasa kama naweza kusema sasa, unataka nisemeje? niandike kwa damu? (anacheka).
Sumaye, ambaye alishindwa kwenye uchaguzi wa wajumbe wa Nec mwaka 2012 kwenye Wilaya yake ya Hanan’g, alisema nchi imefika mahali pabaya kiasi kwamba watu wanaona wakati wa uchaguzi ndiyo halali kwao kupokea rushwa.
“Unajua, imefika mahali watu hawawezi kujitokeza kwa sababu inaonekana mazingira yanayotakiwa ni ya rushwa. Kwa hiyo anasema ah, ya nini? Hata usiende kwenye ngazi ya urais, hivi unadhani hakuna watu wazuri ambao wangekuwa wabunge? Wako,” alisema mbunge huyo wa zamani wa Hanang na kuongeza:
“Lakini wanasema to hell (potelea mbali). Kwa nini niende nikajiaibishe wakati wananchi watakachotaka ni hela? Kwa sababu sisi tumewafikisha hapo... nenda dada gombea uenyekiti wa mtaa, uone kama una plot kama hujaiuza! Kwa sababu wananchi wanasema ‘huyu anakuja kugombea. Tuone atatuletea nini. Hapo hujagawa khanga, fulana, pochi, bahasha hazijatembea. Unaona? It’s that filthy… na tumewafikisha wananchi wetu sasa wanafikiri wakati wa kampeni ni halali kwao kula rushwa. Actually wanadhani ni wakati wa mavuno, which is nonsense (ni upuuzi).”
Sumaye alisema vitendo vya wananchi wa Masasi au Liwale kuchoma nyumba za wabunge, polisi au madiwani, havitokani na kukasirishwa na kugongwa kwa bodaboda, bali hasira dhidi ya viongozi wao na hivyo hutumia nafasi hiyo kuwaadhibu.
“Wale wa Masasi; bodaboda anagongwa na gari la polisi, wanachoma nyumba ya mbunge, wanachoma halmashauri, wanachoma polisi. Hivi unadhani ni kwa sababu ya bodaboda kugongwa? Bodaboda? Watu kila siku wanauawa.
“Kila mtu anawajua (waendesha bodaboda). Hata kama wasingekuwa rough… sasa hiyo ni traffic case. Watu wamekutana barabarani, kwa nini wakachome magari ya wabunge na nyumba za wabunge? Lazima msome maandishi kwenye ukuta,” alisema Sumaye akimaanisha hadithi ya kwenye Biblia ya Mfalme Belishaza ambaye alitumia vyombo vya ibada kunywea pombe na baadaye kiganja cha mkono kikajitokeza ukutani kuandika “ufalme wako umekwisha”.
“Tumefika mahali pagumu. Kule Liwale wananchi wamechoma nyumba zote za madiwani na wote ni wa CCM, wamechoma nyumba ya mbunge na ya mama yake mbunge wakachoma. Eti (kwa sababu) bei ya korosho inashuka na kupanda! Diwani anapanga bei ya korosho?
“Watu hamuoni tu vitu ambavyo watu wanafanya. Mnadhani ni ajali tu zinatokea. Wapo watu wanachukizwa kabisa na rushwa na wanaumizwa kabisa na rushwa. Ninyi waandishi wengine mnaweza kufaidika na rushwa, lakini itakupeleka wapi.”
Hata hivyo, Sumaye alisema kwa sasa mambo yamebadilika kiasi kwamba hata vyombo vya habari vimekuwa tofauti.
“Ukisoma magazeti ya sasa ni tofauti. Zamani ulikuwa unasoma mpaka unatamani uhame nchi, mambo ya ajabu kabisa,” alisema.
Kuhusu mustakabali wa chama hicho kilichoshika madaraka kwa takribani miaka 50 sasa, Sumaye alisema anavyokiona, kama hakitadhibiti rushwa, kitakufa.
Alisema ndani ya CCM na serikalini wapo viongozi wasiofaa kutokana na kuwa wamechaguliwa kwa kutumia rushwa.
“Kwa mfano tuseme wewe unataka kugombea Ulanga na wananchi wanakujua, wanakutaka ugombee, lakini akaja mtu mwingine mwenye mapesa akawahonga viongozi wa pale Ulanga kisha anapita yeye… yule mtu anayependwa na wananchi walio wengi atahamia chama kingine na unafikiri nini kitatokea? CCM itapoteza kiti kile. Sasa kama zaidi ya nusu ya nchi ikifanya hivyo, unafikiri nini kitatokea?” alihoji.
Alisema hiyo inatokana na mabadiliko makubwa yaliyopo nchini kwa sasa, akifafanua kuwa wananchi wengi wamebadilika, wamekuwa na upeo mkubwa wa kutazama na kuelewa mambo na kuwa wanajua wanachotaka na kamwe hawahadaiki kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
“Lazima tukubali mazingira haya, si yale ya zamani… Zamani ukishapita CCM, hata ukiwa wewe ni dude la ajabuajabu tu, unajua utapita tu. Lakini siyo leo. Mambo yamebadilika kabisa,” alisema Sumaye.
Alisema wananchi wameanza kufunguka na wanajua haki zao, wanajua nini maana ya kumchagua mwakilishi, kiongozi na kuwa watafika mahali watachoka.
“Wala siyo kwa CCM tu, chama chochote kinachojihusisha na rushwa, maisha yake si marefu katika uongozi. Iwe CCM iwe chama gani, iwe shughuli nyingine yoyote, ukiwa unajihusisha na rushwa huwezi kufika mbali,” alisema Sumaye ambaye aliingia Nec katika miaka minane ya mwanzo kwa nafasi yake ya Waziri Mkuu.
Sumaye pia alizungumzia jinsi rushwa ilivyotawala wakati wa uchaguzi wa wajumbe wa Nec, akiungana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye pia aliliambia gazeti hili kuwa mabilioni ya fedha yalichangwa kwa ajili ya kuhonga wajumbe.
“Katika uchaguzi ule pesa ilitumika… kulikuwa na matumizi ya ajabu ya pesa. Nilikiandikia chama barua kutaka kichukue hatua, lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Hata nyinyi wenyewe nendeni kule Hanang muulizeni mwana-CCM yeyote, atawaambia jinsi anavyoshangaa sababu za kutochukuliwa hatua zozote,” alisema.
Alisema katika chaguzi zote za ndani ya CCM na hata zile za Serikali, rushwa imekuwa tatizo kubwa, ingawa anasema kwamba anaamini ipo siku hali hiyo itakwisha.
Alisema pamoja na ukweli kuwa rushwa ilikuwapo hata katika kipindi cha utawala wa awamu ya kwanza, ya pili na tatu, haikuwa kubwa na ya wazi kama ilivyo sasa.
“Wakati ule rushwa ilikuwa ni pombe na nyama. Hata mwalimu alikuwa akisema anajua kuna vichaichai vimetembea, lakini alionya watu hao wasichaguliwe na kweli watu walikuwa wanawakataa, hawawachagui. Sasa hivi kuna utamaduni mpya umeanza katika nchi yetu, watu wanauliza wazi huyu ametoa ngapi, wakati wa kupiga kura wanasema jamani huyu ametoa nyingi ndiye apewe bila kujali uwezo na uadilifu na sifa zake… hili ndilo linalotuangamiza.”
Sumaye ni mmoja wa makada sita wa CCM waliopewa adhabu ya kufungiwa kwa miezi 12 na Kamati Kuu ya chama hicho kwa madai ya kuanza kampeni za urais mapema kinyume na kanuni za uchaguzi, lakini anasema hadi leo hajui alifanya kosa gani na bado anasubiri uamuzi wa rufaa zake mbili.
“Kanuni inasema mtu yeyote ambaye amepewa adhabu na hakuridhika atakata rufaa kwenye Kamati Kuu. Ndiyo kanuni inavyosema. Lakini nikaeleza wazi kuwa hili naona lina tatizo kwa sababu nitapewaje haki kwenye Kamati Kuu wakati ndiyo iliyoniadhibu?” alihoji na kuongeza:
“Lakini nikasema kwa sababu kanuni ndiyo inataka hivyo, ninatimiza sharti la kanuni. Mimi sijaridhika, sioni kosa langu ni nini. Nikakata rufaa. Nikakaa miezi mitatu sikujibiwa. Nikakata rufaa nyingine, nikasema sasa nakata rufaa ambayo nadhani ndiyo hasa nilikuwa naiwania; kwenye Halmashauri Kuu kwa sababu ndicho chombo cha juu ya kile kilichoniadhibu. Nikakata rufaa tangu mwezi wa sita hadi leo sijajibiwa,” alisema.
“Kwa hiyo ndiyo maana nikasema hata mimi sijui hatima ya rufaa yangu… lakini mimi nimeandika kwamba siridhiki, siyo siridhiki na adhabu niliyopewa, sielewi, sijaridhika kwa nini nipewe adhabu. Sasa nilitegemea angalau wangelikaa wakasema bwana tumekupa adhabu tunadhani ni sahihi kwa sababu hivi, hivi na mimi sababu zangu za appeal (rufaa) nimeziweka pale.
“Sasa ninaendelea kusubiri majibu. Huwezi kwenda kuvunja mlango ukasema ninataka majibu yangu,” alisema Sumaye na kufafanua kuwa, alivyojieleza kwenye Kamati ya Maadili alidhani ameeleweka, lakini akajikuta akijumuishwa kwenye adhabu hiyo.
“Unajua unaweza ukajieleza ukafikiri watu wamekuelewa. Umehojiwa ukajibu, ukaona watu wameridhika lakini ndiyo hivyo unashangaa unapoona hakuna majibu,” alisema akijibu swali kama hakuelezwa kosa wakati alipoitwa kuhojiwa.
Hata hivyo, alisema hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kina kwa sababu liko kwenye rufaa na hivyo anaweza kuonekana anakata rufaa kwenye chombo kingine.
Kuhusu urais
Hata hivyo, Sumaye, ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 64, aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa bado hajaamua kuingia kwenye mbio za urais, akisema kuwa wakati ukifika atatangaza.
“Actually kinachoniponza sana ni hili suala la rushwa. Kwanza kanuni hiyo ya CCM inasema kutangaza nia siyo kosa. Kwa maana hiyo, hata ningetangaza si kosa ingawa sijawahi kufanya hivyo. Nimesema tu kuwa muda ukifika wa kufanya hivyo nitasema.
“Yaani ungeweza kutangaza nia mwaka 2010 baada ya Rais (Jakaya) Kikwete kuapishwa. Hiyo haina tatizo ilimradi usifanye kampeni. Ndiyo maana hata January Makamba alipotangaza nia, Rais alisema hakuna kosa isipokuwa aliwahi sana. Kinana aliulizwa akasema hivyohivyo, Nape aliulizwa akajibu hivyo.”
Hata hivyo, akasisitiza kuwa hawezi kutangaza sasa hata kama wengine wanaendelea kufanya hivyo.
“Watangaze tu kwa sababu uzuri wake ni kwamba jambo hili si riadha kwamba wenzako wameanza kuzunguka uwanja nawe ukianza watakuwa wamekuzunguka mara nyingi,” alisema.
Hata hivyo, alipoulizwa kama anaona iwapo kuna mtu ambaye anamwona hana doa la rushwa ndani ya CCM au upinzani ambaye anafaa kugombea urais, alisema: “Mimi naweza nikanyoosha. Siwezi kujua watu wengine, lakini mimi najijua. Siwezi kupokea rushwa yako hata siku moja (pakawa kimya)… mna wasiwasi?”
Msimamo wake kuhusu mchakato wa Katiba
Sumaye alisema msimamo wake kuhusu muundo wa Serikali ni kuwa na serikali mbili na siyo tatu.
“Mimi, argument (hoja) yangu ni... so simple (rahisi)... ipo wazi. Ninachokisema ni kwamba, kwanza tunautaka Muungano au hatuutaki? Tunautaka, maana mimi nautaka. Sasa mimi nasema kama tunautaka, ni nini kinatufikisha hapa leo? Kila upande unamlalamikia mwenzake,” alisema.
“Sasa badala ya kusema tunataka serikali tatu, tukae ndani ya serikali mbili ili turekebishe yale ambayo yanatufikisha huko. Nyinyi Wabara mnasema Wazanzibari wamevuka mipaka yao sasa wana nchi yao na nini kwa maana ya kuwa almost a sovereign state (karibu kuwa taifa kamili linalojitegemea). Sasa turudi nyuma, kwamba tusifike huko.
“Nyinyi Wazanzibari mnasema hawa wamefunikwa kwenye blanketi la Muungano, wanajificha humo, wanakula humo. Sasa tulifunue hilo blanketi.”
Mtendaji huyo mkuu wa zamani wa Serikali alisema kama ukianzisha serikali ya tatu, huyo rais wa Tanganyika na Watanganyika wake hawatakubali chochote pungufu ya kile walichonacho Wazanzibari.
Alisema kama Zanzibar ina wimbo wa taifa, bendera au rais wake anapigiwa mizinga 21, basi na Watanganyika watayataka hayo pia.
Alisema kuanzisha serikali ya tatu ni kutengeneza rais ambaye ataitwa mkubwa lakini kwa uhalisia atakuwa mdogo.
“Sasa nasema Zanzibar ni kadogo, tena kisiwa wanafanya hayo. Hili linchi likubwa hivi, lenye watu hao wote, wakiamua kufanya hao, bado kuna Muungano? Huyo rais wa Muungano ataheshimika kwa sababu ipi?”
Alisema kufanya hivyo, ni kutengeneza rais wa Muungano ambaye ataitwa mkubwa, lakini hana mamlaka na kwamba hali hiyo itaendelea hadi kwenye rasilimali, ambazo kimsingi nyingi ziko Bara na hivyo kukiwa na matatizo Bara, rais wa Tanganyika hatakubali kuilisha Zanzibar na kuacha wananchi wake.

SIASA::DK SLAA ATEULIWA TENA KUWA KATIBU MKUU WA CHADEMA


Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Chadema,  Dk. Willbrod Slaa, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika kuwa na Salum Mwalim ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar. 
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe amewateua Dk. Willbrod Slaa kuwa Katibu Mkuu, John Mnyika kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara na Salum Mwalim ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar. Viongozi hao wameteuliwa jana usiku na kupitishwa na Baraza Kuu la Chadema hivyo kufikia tamati ya uchaguzi wa ndani ya chama hicho.
Mhe. John Mnyika anateuliwa kushika nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Mhe. Zitto Kabwe ambaye aliondolewa katika nafasi hiyo na kamati kuu ya chama hicho kwa kudaiwa kuvunja katiba ya chama.

MTUME PETER RASHID AOA MKE WA PILI



Mtume Peter Rashid Abubakari, kiongozi wa kanisa la RGC lililoko Mbezi Kimara Dar Es Salaam, ameamua kumuacha mke wake Bi Zuwena (Catherine) aliyeoana naye tangu mwaka 1985.
 
Alipohojiwa inakuwaje kwa nini amuache na kumuoa Pamela Didas Asenga, binti mdogo wa miaka 20, alidai ndoa yake hiyo ya mwanzo haikuwa halali kwa kuwa alioa akiwa bado mwislamu na alifungishwa na shehe! Kwa hiyo mungu amemfunulia na amempa mke mwingine mwema!

Ndoa hiyo ilifungwa tarehe 29/08/2014, ilifungishwa na Askofu Innocent Lugagi, wa kanisa la White House la Durban Afrika Kusini!





Mtume Peter Rashid na mkewe mpya, hapa ni siku ya kufunga ndoa huko South Africa.

Mtume Peter Rashid Abubakar baada tu ya kutoka kufunga ndoa yake South Afrika amerudi nchini Tanzania na Jumapili akiwa kanisani kwake awatangazia waumini wake kuwa kama una mke ambaye mlichukuana wakati wa ujinga wenu na umekaa naye miaka mitatu au zaidi na hana tabia ya kimungu mkorofi na mchokozi na hujafunga naye ndoa ACHANA NAYE ILI MUNGU AKUPE MKE MWEMA. Na mwanamke naye vilevile.

Alipohojiwa na mmojawapo wa marafiki zake aliyeshangazwa na tukio hilo, kwenye ukurasa wake wa Facebook mtume huyo alijibu hivi:
“…… tafsiri ya mke ni yule uliyefunga naye ndoa kanisani au kwa DC 1Kor 7:15. Huyo nilikuwa nazini naye tu!! Mungu aliponifunulia siri hiyo nikatubu na kumuomba Mungu anipe mke mwema na amenipa.”

Mtume Peter Rashid akiwa na mke wake mpya

Utambulisho kanisani mara baada ya kurudi nchi wakitokea Afrika Kusini.

Baada ya kuwasili wakitokea Afrika kusini.
 
credit;rumafrica

Monday, 15 September 2014

FUNZO LA LEO:::UKIWA HODARI WA KUHONGA, KAA MKAO WA KUACHWA WAKATI WOWOTE!

Leo nataka kuzungumzia suala la uhongaji katika uhusiano. Kuhonga ni tabia ambayo imeshamiri sana katika jamii yetu. Kipindi cha nyuma tumezoea kusikia ama kuona wanaume wakiwahonga wanawake lakini sasa hivi mambo yamebadilika.Wanawake nao wameingia katika mkumbo wa kuwahonga wanaume ili wakubali kuwa nao kimapenzi tu ama waoane kabisa.Tabia hii imekuwa ikiwatia majaribuni walio wengi hali ambayo imesababisha baadhi ya watu wenye tamaa za kijinga kushawishika kufanya ngono na watu ambao katika mazingira ya kawaida wasingeweza kufanya nao.
Ni kitu cha kawaida kabisa kumkuta kijana wa kiume mwenye umri mdogo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mama mtu mzima ambaye angeweza kuwa mama yake. Lakini hafanyi hivyo kwa matakwa yake bali kwa kushawishiwa na pesa ama vitu vingine vya thamani.
Kuna utata kidogo katika neno hili kuhonga, wapo wanaojiuliza kwamba hivi ninapompatia mpenzi wangu fedha kwa ajili ya matumizi madogomadogo nitakuwa nimemhonga? Katika uhalisia neno kuhonga ni kitendo cha mwanaume kutoa fedha ama zawadi kumpa mwanamke hasa pale anapomtongoza ili awe mpenzi wake ama mke wake.
Pia katika kamusi ya kiswahili sanifu neno hilo limetafsiriwa kama malipo ama zawadi itolewayo ili kupata kile unachohitaji au kutaka jambo f’lani liharakishwe, kwa maana nyingine ni rushwa.Maana halisi ya kuhonga itapatikana kutokana na nia ya mwanaume hasa pale anapotoa pesa ama kitu kingine kwenda kwa mwanamke. Kwa mfano kama unatoa pesa kwa ajili ya kumsadia mpenzi wako ama kumkidhia haja mke wako kutokana na tatizo fulani alilonalo, hapo haiwezi ikachukuliwa kwamba umemhonga.
Lakini kama unatoa kitu ama pesa kutaka kulazimisha ama kumshawishi awe rafiki yako, mpenzi wako, mke wako ama kwa kutaka kufanya naye mapenzi, hapo itachukuliwa kwamba umehonga.Kikubwa unachotakiwa kujua ni kwamba, hakuna uhusiano wowote baina ya mapenzi na pesa. Ndio maana mapenzi yanaweza kuwepo hata pale pesa inapokosekana.Kwa kudhibitisha hilo wengi wanaopata penzi kwa njia ya kuhonga, mapenzi yao hayadumu kutokana na mmoja kati ya wawili hao kushawishika kutengeneza uhusiano kutokana na pesa ama kitu kingine.
Utafiti unaonesha kwamba, kwa wanaume walio wengi kuhonga ni sehemu ya maisha yao licha ya kwamba ni katika viwango tofauti.
Hakuna mwanaume asiyehonga ukiachilia mbali wale ambao ni waumini kikwelikweli ambao nao sina uhakika kama hawaingia katika kundi la wahongaji kwa maana halisi ya kuhonga.Licha ya kwamba wapo pia baadhi ya wanawake ambao wana tabia ya kuhonga wanaume ili wawapende, kasi imeonekana kuwepo kwa wanaume ambapo hulazimika kutoa mamilioni ya pesa, magari, simu za mikononi, na vitu vingine vya thamani kwa mabinti ili tu waweze kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Kimsingi niseme tu kwamba, katika uhusiano wa kweli baina ya wawili waliotokea kupendana, suala la kuhongana hakuna. Usimpe mpenzi wako pesa ili kumlainisha akufanyie jambo fulani kwani ipo siku utakuwa huna pesa na unataka akufanyie, hapo ndipo mnaweza kuachana.
Msaidie pale atakapohitaji msaada wako, kama nilivyowahi kusema huko nyuma kwamba, hutakiwi kuwa mbahili kwa mwenza wako kwani wewe ni yeye na yeye ni wewe.

IRAQ and the OBAMA PLAN


Obama announced his new strategy in a televised address on Wednesday [Reuters]
In Baghdad this morn‎ing I was up with rooster as dawn broke over this city. US President Obama's speech was broadcast here at 4am local time and in the distance the call to prayer competed with Obama for the attention of those who were awake. I dare say the call to prayer won in first instance.
His words brought with them a strategy that's been largely welcomed in officialdom here. In particular, two key parts.
The first is setting up of what's been dubbed the "National Guard" to protect towns and cities across Baghdad. This isn't new.
In 2006 when the sectarian violence was at its height in Iraq the American occupiers funded and trained Sunni groups to battle against al-Qaeda forces.
They were successful and al-Qaeda in Iraq was defeated. But then the Americans abandoned them.
That's one of the reasons Islamic State have been able to return.
These national guard units are key, if the Sunni groups can trust the Americans to support them fully and not abandon them once the job is done.
Zebari's position
Air strikes and air support has also been welcomed here. By using American air power alongside Iraq army ground troops, Obama may hand the Iraqis the advantage in beating the Islamic State.
Hoshyar Zebari, Iraqi deputy prime minister, says the strategy, in particular US air support, is crucial.
"We welcome the announcement of the new strategy which President Obama announced last night to face up to ISIS and it's threat not only to the security of Iraq of Syria and the region but the entire world," he told Al Jazeera.
"I believe that this a bold strategy, it will work and definitely we will see an engagement without ground troops and I think from what we have seen with the peshmerga forces and some Iraqi forces that the airstrikes are working and the fighting is being done by Iraqi's themselves."
So far so good. But Syria remains an unknown quantity. Obama was clear that Syria was part of the solution but was less than opaque on what that might mean.
He didn't promise to hit targets in the country, instead saying he would go after the group wherever they posed a threat. This has been met with concern by Iraqis who would rather Obama gave a much fuller idea of what action in Syria might mean.
On Wednesday Haider al-Abbadi, the Iraqi prime minister, said that "Iraq couldn't go into Syria but the Americans could‎", which is an indication that the Iraqis consider action in Syria key to defeating the Islamic state.
Question of ideology
Also as part of this strategy the US is putting together a coalition of Arab states and others to help in the fight and this helps them give cover and allows them to talk of the Islamic State as a wider problem that the region must face together. That has another impact though - one of ideology.
John Kerry, US secretary of state, spoke at length in Baghdad on Wednesday and in particular one thing stood out.
He said: "Countries particularly in the Muslim world, can join together in defining the real Islam and making it clear that there is no legitimacy whatsoever within ISIL for any of the claims that they make with respect to a religious foundation for their Caliphate, their state, or for their actions. It is necessary for moderate, reasonable people around the world to repudiate the distortion of Islam that ISIL seeks to spread‎."
With those words this US administration has declared that beating the Islamic State requires not just military but an ideological battle. But can America lead the ideological ‎charge and help reshape what Islam means globally?
Salman Shaikh, director of the Brookings Doha Centre think tank, says: "One can understand western leaders trying to segregate radical ideology from the rest of Islam but this is fraught. Unless you have Arab and Muslim leaders who want to go down such a route it's better to build on the coalition of countries they're putting together to fight IS and what can be achieved there rather than trying to separate 'bad' Islam from 'good' Islam. The strategy should focus on IS crimes and human right violations which is something everyone can get behind."
'Wide open borders'
Not everyone is on board with the new strategy to defeat the Islamic state, however.
Wathak al-Hashimi, a political writer and head of the of the Iraqi Group for Strategic Studies, told me: "The speech wasn't so optimistic for Iraqis and the countries that suffer from terrorism. Obama won his election by promising to pull out of Iraq and so his desire to re-engage is limited.
"The idea of using air strikes and drones won't have an impact on the ground. IS forces will just regroup in other countries that neighbour Iraq because of our wide open borders.
"The Iraqi government has a red line: no boots on the ground. When your enemy hides itself in civilian population, how do you attack them without civilian casualties?
"Iraq needs a more thorough strategy. This isn't enough."
A more thorough strategy, however, may mean putting American boots on Iraqi ground and that would only give the Islamic State a rallying call that would encourage self-proclaimed jihadists from all over the world to come to Iraq and fight Americans, risking further escalation.
Islamic State's perspective
President Obama is well aware of this and this is why he is hoping that a limited engagement and plan is enough to defeat Islamic State.
There's very little appetite among Americans both within government and outside to see US soldiers return here.
For the Islamic State, Washington's plans are irrelevant.
Through social media one alleged member of its group told me: "Remember. We haven't declared war on America, the beheadings were just a message, blood for blood, soul for soul. Obama is a proxy warrior."
The Islamic State insists that God is on its side and that the "caliphate" will survive and expand, despite what the US and the coalition of Arab states has put together, thinks otherwise.
It is a view that is Illustrated by this message an Islamic State supporter sent out via the social media site Twitter: "Oh Allah, when the world turned against us, we turned to you."

WENYEWE HAO::Marekani bingwa duniani kwa vikapu


Marekani na Serbia wakichuana
Marekani imetawazwa Mabingwa wa kombe la Dunia wa mchezo wa mpira wa kikapu kwa kuichapa Serbia vikapu 129 kwa 92. Marekani wameutetea ubingwa wao waliouchukua huko uturuki mwaka 2010.
Angola na Senegal ziliiwakilisha afrika ingawa hazikufika mbali sana.
Kombe la Dunia la Mpira wa Kikapu la Mwaka huu wa 2014 lilikuwa toleo la 17 la FIBA Basketball World Cup kwa kuwa hapo awali michuano hi ilifahamika kama FIBA World Championship. Michuaono hii iliyofanyika Hispania ni ya mwishopkufanyika katika mzunguko wa miaka mnne kwani michuano ijayo itafanyika miaka mitano ijayo yaani mwaka 2019 ili kurekebisha hesabu za miaka kuingilia ratiba ya Kombe la Dunia na Fifa.
Katika ligi kuu ya England, ushindi wa Manchester United wa mabao 4-0 dhidi ya Queens Park Rangers umempa nguvu meneja wa timu hiyo Luis Van Gaal na kusema kuwa matarajio yake ni kurejesha taji la ligi katika uwanja wao.
Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya mchezo kuisha amesema, "Nataka kushinda taji la ligi kuu, kama si mwaka huu basi msimu ujao na kama sio ujao basi utakaofuata, nataka kuwapa ushindi mashabiki". Van Gaal, akipata nguvu za ushindi.
Hii leo, Hull City wanawaalika West Ham United katika KC Stadium ama Kingston Communications.
Kwa bahati mbaya Hull City italazimika kucheza bila mshambuliaji bwana mdogo aliyezaliwa mwaka 1990 Abel Mathías Hernández Platero.
Mshambuliaji huyo kutoka Uruguay ni mmoja wa wale waliosajiliwa katika ile tunayoweza kuiita dakika ya tisini akitokea Palermo lakini mashabiki wa Hull watalazimika kusubiri baada ya meneja Steve Bruce kutangaza kuwa kibali cha kufanya kazi hakijapatikana bado. Pengine atatokea katika mfumo wa kuwashangaza mashabiki. Uzuri ni kuwa Muuruguay mwingine Gastón Ezequiel Ramírez Pereyra atakuwepo katika safu.

Iraq WAR: HISTORY REPEATING


Will the mistakes of the recent past be made again as Iraq and its allies take the fight to the Islamic State group?
World leaders and global organisations have in recent days raced to condemn the Islamic State group for their lack of Islam. First among them was the US President Barack Obama who called the group "neither Islamic nor a state".
British Prime Minister David Cameron weighed in after the brutal execution of British aid worker David Haines, calling the group "the embodiment of evil". A group of British Muslims representing several organisations even went so far as to plead with the prime minister to stop referring to the group as "Islamic State", instead offering "Unislamic State" as an alternative. This statement was issued just hours before Haines's death.
Curiously, all of these groups have been silent about previous brutal deaths at the hands of IS. I heard no such anger from anyone in officialdom when my dear friend and cameraman Yasser Faisal al Jumali was killed in Syria in December 2013. I heard no condemnation for the eight people beheaded in the Kingdom of Saudi Arabia last month alone. It seems the only way to galvanise the world to act is when westerner's die brutal deaths.
There is historical precedent to back that statement up.
It is 2004 and Iraq is aflame with violence. Two men, unknown to each other but who are now forever linked, are in Iraq. Both are helping rebuild after the American occupation. Nick Berg, a freelance American radio tower repairman, and British Civil Engineer Ken Bigley.
Both are beheaded by al-Qaeda, the killing of Berg in response to American atrocities that took place at Abu Ghraib prison.
Thier deaths send shockwaves throughout the world. The then US president, George Bush, tells reporters that there is no justification for Berg's death. House Majority leader Tom Delay goes even further, calling them "terrorists" and "monsters".
None of them mention Abu Ghraib.
Murderer or freedom fighter?
The outrage is similar when Ken Bigley is killed. The Muslim Council of Great Britain makes great steps to intervene and prevent his killing, but to no avail. ‎His is said to be a response to Iraqi women being held without charge by British forces, a charge the British government denies.
The man behind the group responsible for the beheadings is developing a fearsome reputation. Abu Mus'ab al Zarqawi is a Jordanian national who the US accuses of ties with Saddam Hussien before the war, ties that were never proven. After the war his group becomes one of the most feared and quickly picks up support from Iraqi Sunni groups who felt the war in Iraq was turning against them. Between 2004 and his death in 2006 he creats havoc. The US puts a $25m bounty on his head, the same as Osama Bin Laden.
His impact on Iraq cannot be underestimated. A well trained fighter who honed his skills in Afghanistan, he fled to Iraq ‎in 2001. In 2003 he began to build his organisation, then called the party of "Monotheism and Jihad". He directed his anger toward Iraq's Shia community. For hims it would rally Sunnis to his cause. It worked and his campaign sent suicide bombers into markets, schools, and mosques in predominantly Shia areas.
In 2004, he caught the attention of Osama Bin Laden and pledged alliance to al-Qaeda. The merger made al-Qaeda a powerful force. It didn't last long. Zarqawi's tactics of beheadings and targeting civilians angered al-Qaeda's number two Ayman al Zawahiri. He wrote a letter critising Zarqawi's tactics and sent it to the man himself.
Zarqawi ignored the message and by 2006 wanted more power. He styled himself as a spiritual leader, and increasingly relied on a hardline interpretation of sharia for justification.
In Iraq itself, he killed Iraqi sheikhs who stood in his way. Globally he began to lose support of Muslims, who began to see him as a brutal murderer rather than a freedom fighter. Sunnis in Iraq had by this point begun to turn against Zarqawi's organisation and the US capitalised by funding Sunni "Awakening Councils" to fight the group. In June 2006, the Americans finally hit his hideout and he was killed.
Al-Qaeda in Iraq had lost its leader and the foreign fighters Zarqawi relied on had disappeared. Taking the initiative the US put into place the "surge" in 2007 to finally rout the insurgency, and to train Iraqi forces to take over from them so that they could leave. They finally pulled out in December 2011.
'We have been here before'
Fast forward to 2014. IS are now in the same position. They have developed a fearsome reputation. The international community wants to take action against them. The group's leader has declared himself Caliph Ibrahim, a title which gives him religious and political power. But, once again, the brutal tactics and beheadings have been criticised by other jihadi groups and many Muslim groups are distancing themselves from IS.
There are some differences. The Americans do not want boots on the ground, relying instead on air power. Unlike al-Qaeda in Iraq, IS has a safe haven in Syria and a political situation it can exploit. 'Caliph Ibrahim' knows the appetite to go into Syria is low because ultimately it will help President Bashar al-Assad, and that is not something the US is willing to do. This time around it is going to be a much tougher fight to get rid of the group.
However, the issue with both Zarqawi and with 'Caliph Ibrahim's' organisations is the cult of personality that has developed around them. If the US has learnt anything from history then the lesson it must take away is that by killing the leader you can destroy the group.
But no Western Leader has put forward a strategy to deal with what happens after, and that is where history really comes into play. After Zarqawi died, the US abandoned the very men it relied on to fight al-Qaeda in Iraq. Then Iraqi Prime Minister Nouri Al Maliki, a Shia, ignored and marginalised the Sunni. ‎They lost hope and when Syria disintegrated the jihadi's found a cause, and then from the ashes of that fire rose the Islamic State group. Much of al-Qaeda in Iraq rose with it. The tactics, the ideology is familiar. We have been here before.
The only questions are now these: The international community have begun to act, but will they be willing to move beyond just destroying IS? Are they able to find political solutions in Iraq and Syria that will stop the rise of another Zarqawi or another 'Caliph Ibrahim'? Or are the mistakes of the past due to be repeated?

BIASHARA YA LEO::MICROSOFT WAINUNUA MOJANG KWA DOLA ZA KIMAREKANI BILIONI 2.5


KAMPUNI ya Microsoft imeinunua Mojang, kampuni ya Sweden inayomiliki michezo maarufu ya komputa ya Minecraft kwa dola za Kimarekani bilioni 2.5.
Ununuzi huo umetangazwa na Mkurugenzi wa Xbox, Phil Spencer.
Baadhi ya wachambuzi wamesema ununuzi huo umefanyika ili kuvutia watumiaji wengi kutumia simu za mfumo wa Microsoft wa Windows.
Dili hilo limekamilika ikiwa ni mwaka mmoja tangu Microsoft kuinunua kampuni ya simu ya Nokia.

KWANI MBAYA::Queen Darleen Akanusha Kumtafutia Mademu Diamond

Queen Darleen amekanusha tuhuma kuwa ana mtindo wa kumtafutia mademu kaka yake Diamond Platnumz.

Queen amesema kwa heshima aliyonayo kwake, sio rahisi kumpa kazi hiyo.

“Unajua Naseeb miye ananiheshimu sana hata akiwa na wenzake kama alikuwa anaongea ujinga nikiwepo haongei kwakuwa anajua miye ni mkubwa wake,” Queen ameiambia Bongo5. “Na pia naweza kukaa hata miezi mitatu hatujaonana sasa nashangaa naambiwa namtafutia wanawake. Anajua sasa hivi yeye yupo juu na anafanya vizuri kwahiyo watu wanaongea tu vitu ambavyo hawavielewi. Siwezi kufanya hivyo hata siku moja kwani yeye ana maisha yake na uhuru wake na miye pia hivyo hivyo. Basi nisiwe na marafiki wazuri nitaambiwa namuunganishia mdogo wangu! Kwahiyo niwe sasa na marafiki vijuso sasa? Lazima watu wajue kuwa Diamond ni mdogo sana kwangu na tunaheshimiana sana siwezi kumpangia masuala ya mahusiano miye yeyote nitakayeletewa na yeye kwangu sawa ili mradi kampenda mwenyewe mie sina tatizo,” ameongeza.

Kwa upande mwingine muimbaji huyo amesema anatarajia kutoa wimbo aliomshirikisha mdogo wake huyo.

“Nipo busy sana na kazi zingine si unajua tena ila mashabiki wangu wasijali natoa wimbo mpya soon ambao nimemshirikisha mdogo wangu Naseeb aka Diamond Platnumz. Wimbo umefanyika kwa Tudd Thomas. Jina la wimbo bado sijajua. Sitowaangusha mashabiki wangu kama kawaida.”

JICHANGANYE NA WEWE::Ajuza amfundisha adabu jambazi

Mtaa wa Whitstable, Kent
Ajuza mwenye umri wa miaka 80 alimpiga mwizi usoni mwake nchini Uingereza na kumuogopesha kiasi cha kutoroka.
Mwanamke huyo, alikuwa anamtembeza Mbwa wake katika mtaa wa Whitstable, Kent, wakati jambazi huyo alipomvamia. Alikuwa amevalia mavazi meusi yaliyokuwa yamefunuika kichwa chake.
Alipigana na jambazi huyo na kumgonga kinywani. Polisi mjini Kent wanasema kuwa wangali wanamsaka jambazi huyo.
Afisaa mkuu wa polisi katika eneo hilo alinukuliwa akisema: ''Inaonekana mshukiwa huyo alimlenga mtu asiye wa kiwango chake.''
Shambulizi hilo lilifanyika wakati wa usiku Afisa mkuu wa polisi pia amewataka wakazi wa eneo hilo kutoa habari kuhusu tukio hilo.
"je unamfahamu mtu yeyote ambaye alikuwa nje wakati wa usiku wakati ajuza huyo alipovamiwa na kurejea nyumbani akiwa na jereha kinywani? Tafadhali tunawaomba mtusaidie na uchunguzi wa kisa hiki,'' aliongeza kusema afisaa huyo.

CHOVYA CHOVYA::Sikio la Kufa Halisikii Dawa, Aunty Ezekiel Akutwa Tena na Yule Mume wa Mtu




Stori: Imelda Mtema
Mahaba niue! Baada ya penzi la staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel Grayson na dansa wa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Moses Iyobo ‘Moze’ kushamiri kwa kasi ya umeme, wawili hao wamenaswa wakisindikizana kimalovee kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar.

Tukio hilo lililopigwa chabo na mwanahabari wetu mwanzo mwisho, lilijiri Ijumaa iliyopita ambapo wawili hao walionekana wakiingia pamoja kimahaba eneo hilo.

Aunt ambaye ni mke halali wa Sunday Demonte anayedaiwa kufungwa Uarabuni kwa msala wa madawa ya kulevya, alionekana na Iyobo ambaye pia ni mume wa mtu (Mwengy) wakishikana mikono katika sehemu ya kukagulia mizigo kisha wakaagana kwa mabusu motomoto.

Mwanahabari wetu alipomuuliza Aunt kulikoni, alifunguka: “Nakwenda Marekani lakini wengine wote unaowaona wananisindikiza kama desturi ya watu kusindikizana.”Kweli? 
GPL

UBARIKIWE::MISS ILALA NO 2 AWAPATIA ZAWADI WATOTO YATIMA, WAMUOMBEA DUA MAALUM

Mkuu wa wilaya ya Ilala, Raymond Moshi akitoa mkono wa heri kwa Miss Nasreem Abdul.
Miss Nasreem Abdul akiwa pamoja na wasichana waliofanyiwa ukatili na kutelekezwa na sasa wanalelewa na Taasisi ya wanawake katikaa Jitihada Kimaendele 'WAJIKI' Kilichopo Mwananyamala Kinondoni Jijini Dar.
Miss Nasreem Abdul akiwa na watoto yatima wa kituo cha AL- HIDAYA ORPHANS CENTER cha buguruni.
Miss Ilala namba mbili Nasreem Adbul ameonesha mfano wa kuigwa kwa warembo wengine baada ya kuwapatia zawadi watoto yatima wenye uhitaji na wanaoishi mazingira magumu.

Kwa mujibu wa meneja wa mrembo huyo Livingstone Mkoi alisema kuwa" Katika kile kinachoonekana kuguswa na matatizo  ya kijamii na ni siku chache tu tangu achukukue ushindi wa pili katika kinyang'anyilo cha kumtafuta Miss Ilala mrembo wetu ametembelea vituo kadhaa vya watoto yatima pamoja na TAASISI YA WANAWAKE KATIKA JITIHADA KIMAENDELEO "WAJIKI" Iliyopo Mwananyamala Jijini Dar na kutoa kile alichokuwa nacho" Alisema Mkoi
Aidha kituo kingine alichotembelea  mrembo huyo ni cha AL- HIDAYA ORPHANS CENTER Kilichopo Buguruni ambacho kina watoto zaidi ya 70 huku kila siku wanaongezeka.
Hata hivyo kwa upande wa mrembo huyo alisema" Namshukuru Mungu kwa kunisaidia kuwa mshindi wa pili na wiki hii tunaingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya shindano la Taifa la Urembo hivyo nimeguswa na matatizo wanayoyapata watoto yatima na ndiyo maana nimetoa zawadi yako kwako kama msaada na Mungu akinijalia baadae tena nikishinda taji la Taifa nitaendelea mikoani kwani watoto wako wengi wanaoitaji msaada" Alisema Nasreen

WAATHIRIKA WA MABOMU MBAGALA KUU WAIBUKA WAMLILIA RAIS KIKWETE WAPATE MALIPO YA FIDIA STAHIKI

Dotto Mwaibale 

 WAATHIRIKA wa milipuko ya mabomu iliyotokea katika Ghala la Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Mbagala Aprili 29 mwaka 2009 wameibuka upya wakimuomba Rais Jakaya Kikwete kuwasaidia wapate malipo stahiki kutokana na milipuko hiyo iliyosababisha vifo na kuharibu nyumba na mali zao mbalimbali. 

Ombi hilo limetolewa na waathirika hao kupitia Mwenyekiti wao Steven Gimonge katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na waathirika hao zaidi ya 300 uliofanyika leo asubuhi viwanja vya Shule ya Msingi Mbagaala Kuu iliyopo Manispaa ya Temeke. 

Alisema kwa muda mrefu waathirika hao wamekuwa wakiidai serikali iwalipe fidia tangu uharibifu ulipotokea ambapo serikali ilikubali ingawa fidia waliyolipwa awali haikulingana na uharibifu uliowapata. 

 Gimonge alisema pamoja na fidia hiyo ndogo walipewa fursa ya kuandika barua za mapunjo ambapo kwa mara kadhaa walilipwa fidia ndogo ambapo aslitolea mfano mtu kulipwa fidia ya sh.1400, 2700, 1950 na 4900 mpaka Machi 12 mwaka jana kufikia uamuzi wa kupanga maandamano ya kwenda Ikulu kumuona Rais Jakaya Kikwete. 

 Aliongeza kuwa wanapenda kumkumbusha Rais Jakaya Kikwete kuwa alipokwenda kuwafariji baada ya milipuko hiyo alitoa ahadi ya kuwapa kifuta machozi pamoja na kufidiwa na hata kijiko kilicho potea lakini hadi leo hii wamekuwa wakipigwa danadana. 

Katika hatua nyingine wamemlalamikia Mbunge wao Dk.Faustine Ndugulile kwa kuwaacha bila ya kuwasaidia wakati alionesha njia ya kulipekea suala hilo Bungeni lakini tangu afike huko amebadilika na hakuna mawasiliano yoyote jambo ambalo linawashangaza. 

 Waahtirika hao wanamuomba kwa mara nyingine Rais Kikwete awasaidia kupata fidia hiyo kwani ile iliyotolewa awali ilikuwa kidogo ukilinganisha na ukubwa wa kuathirika kwao.
 Mwenyekiti wa waathirika wa mabomu wa Mbagala Kuu, Steven Gimonge akionesha daftari lenye majina ya waathirika hao na jinsi malipo yalivyofanyika wakati akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi katika mkutano wa hadhara uliowahusisha waathirika wa mabomu hayo yaliyolipuka katika ghala la Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Aprili 29,2009.
 Mwenyekiti wa waathirika wa mabomu wa Mbagala Kuu, Steven Gimonge, akisisitiza jambo katika mkutano huo. Kulia ni Katibu wa Waathirika hao, Thomas Mbasha. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Waathirika hao hapa wakionesha mabango yenye ujumbe tofauti tofauti.
 Mmoja wa waathirika wa mabomu hayo akiwa amejiinamia kwa huzuni huku akitafakari kama Rais atawaonea kwa jicho la huruma wapate fedha hizo kulingana na ukubwa wa kuathirika kwao.
 Mabango zaidi yenye ujumbe tofauti yakioneshwa mbele za kamera za wanahabari.

 Waathirika hapo wakiwa kwenye mkutano huo kujadili jinsi serikali itakavyowapatia fedha zao kulingana na ukubwa wa kuathirika kwao baada ya malipo ya awali kudai walipunjwa.
 Waathirika hao wakiwa kwenye mkutano huo uliofanyika Viwanja vya Shule ya Msingi ya Mbagala Kuu Dar es Salaam leo asubuhi.

 Baadhi ya wazee na vijana waathiriwa wa mabomu hayo wakiwa kwenye mkutano huo.
 Waathirika wakisisitiza kulipwa malipo hayo ya ziada baada ya awali kudaiwa kutolewa kidogo.
 Mkazi wa Mbagala Kuu, Johanaina Mkukumbe akielezea jinsi walivyoa athiriwa na mabomu hayo pamoja na fidia kiduchu waliyolipwa.

Bwana harusi aaga akienda harusini

Bwana Harusi azama baada ya mafuriko kusomba boti lao
Takriban watu 17 akiwemo bwana harusi na watoto wawili wamekufa maji baada ya boti ya uokoaji iliyokuwa imewabeba wageni kwenda kwa sherehe ya harusi kuzama katika mafuriko nchini Pakistan.
Maafisa wanasema kuwa takriban watu 22 wameokolewa huku waokoaji wakiwatafuta watu zaidi.
Msemaji wa shirika la kukabiliana na majanga amesema kuwa zaidi ya watu millioni 2 nchini humo waliathiriwa na mafuriko hayo ambayo yalisababishwa na mvua kubwa.
Maafisa wanasema kuwa takriban watu 289 wamefariki katika mafuriko hayo nchini Pakistan kufikia sasa.
Zahid Ali mwenye umri wa miaka 27,mchumba wake Mashal pamoja na wageni walikuwa katika boti hiyo iliyokuwa ikielekea katika sherehe za kundeleza harusi yao.

Watu 18 waliokuwa wanakwenda kushuhudia harusi wameaga dunia
Maafisa wanasema kuwa boti hiyo iliojaa kupitia kiasi ilikuwa ikivuka mto Chenab uliofurika katikati ya mji wa Punjab eneo lililoathirika vibaya na mafuriko nchini Pakistan.
Msemaji wa huduma ya uokozi katika eneo hilo la Punjab amesema kuwa familia hiyo ilionywa kuhusu mafuriko hayo.
Bi harusi amesema kuwa alinusurika baada ya kushika mti wa stima.
Mazishi ya waathiriwa 17 yamefanyika huku waokoaji wakiendelea kuwatufuta wale waliotoweka.

UCHUMI WA MASTAA WA KIKE WA BONGO...NANI KAMZIDI MWENZIE,JIONEE






RAHA YA PESA!!Wema Sepetu Amjibu Kajala , Naye Agawa Pesa Kama Mvua

 



Wema Sepetu amwaga mijihela usiku maalum wa birthday ya Mr. Jack’s a.k.a Jack Daniel’s uliopambwa na Skylight Band
Hapo Kwenye Picha Wema Alikuwa anaimbiwa Wimbo Maalumu kwa Ajili yake na Kuamua Kufungua Pochi na Kugawa Mijihela Kibao Kwa Mwimbaji Sam wa Skylight Band Kitendo Kinachoonekana Kujibu Mapigo kwa Kajali Kwani Siku si Nyingi nae alimwaga Minoti ya kufa mtu kwa Waimbaji wa ya  Moto Band....Mweee Siku hizi tuna Mapedejee wa Kike...Lol