Monday, 10 November 2014

HABARI::WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA

IMG_5158
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri mara baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga Mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu na wa pili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).

* Ataka iundwe timu kufuatilia utekelezaji wa Azimio la Arusha 2014

Na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema inahitajika dhamira ya kweli kutoka kwa wadau wote katika kutekeleza Azimio la Arusha la kukabiliana na ujangili na kuendeleza hifadhi za wanyama katika nchi za Afrika Mashariki na zilizo Kusini mwa Ikweta.


Akizungumza na waandishi wa habari juzi mara baada ya kufunga mkutano wa kikanda wa siku mbili uliojadili mbinu za kupambana na biashara haramu ya wanyamapori ulioandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Arusha, Waziri Mkuu alisema: “Suala hili linataka uwajibikaji wa pamoja. Mashirika na taasisi, wananchi na viongozi sote kama wadau wakuu, kila mmoja anapaswa kushiriki vita hii kama kweli tunataka tuitokomeze.”

“Kwenye hili Azimio la Arusha na nyie waaandishi wa habari pia mna sehemu yenu mmetajwa... wamesema wanatafuta jinsi ya kushirikiana na vyombo vya habari ili visaidie kutoa elimu kwa jamii kama njia ya kuelimisha umma,” alisema.

Waziri Mkuu aliwaeleza waandishi hao kwamba Azimio hilo lina vipengele 20 ambavyo vinataka utekelezaji katika ngazi ya nchi mojamoja, ngazi na kanda na ngazi ya kimataifa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

IMG_5160
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akielekea kwenye chumba cha mapumziko kabla ya kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh. Lazaro Nyalandu, wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

“Nimepata faraja kwamba mkutano huu haukuisha kijumlajumla tu, bali umekuja na maazimio 20 ambayo yametengwa kwa ajili yetu sisi wa ndani, mengine yanahusisha ushirikiano wa kikanda na yako mengine yanawahusisha wadau wa maendeleo,” alifafanua.

Ili kutekeleza azimio hili, nimeshauri iundwe timu itakayoshirikisha vyombo vingi zaidi badala ya kuiachia Wizara ya Maliasili na Utalii peke yake. Timu hii ikutane kila baada ya miezi sita ili kufuatilia utekelezaji wa maazimio haya na ikibidi Waziri atoe taarifa bungeni kuhusu utekelezaji huo,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema, akizungumza na washiriki wa mkutano huo wakati wa kuufunga, Waziri Mkuu alisema kuwepo kwa watu wa ngazi tofauti kwenye mkutano huo ni kielelezo tosha cha umakini wao na nia thabiti ya kutokomeza ujangili katika ukanda huu.

IMG_5167
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli kwenye chumba maalum cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.


“Tumeanzisha vita, tusisahau kwamba bado kuna kazi kubwa mbele yetu na vita haijaisha. Tuzidishe mapambano katika sehemu tatu: kwenye nchi unakofanyika ujangili, nchi ambazo nyara zinapitishwa na nchi zinazopokea ama kununua hizo nyara,” alisema Waziri Mkuu.

“Nakubaliana nanyi kwamba hakuna nchi inayoweza kukabili suala la ujangili ikiwa peke yake. Tunahitaji tuwe na sera mahsusi, sera ya pamoja ya kutuunganisha na kutuongoza wakati tukitekeleza Azimio hili kwa kusaidiana na wadau wa maendeleo,” alisema.

Alisema Azimio hilo litaipa kazi ya ziada ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo kazi kubwa itakuwa ni kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wa wa Azimio hilo unakuwa wa ufanisi.
Jumla ya nchi tisa zimetia saini azimio hilo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5170
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mbunge wa Kahama, James Lembeli, huku Waziri wa Mali asili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akifurahi jambo ndani ya chumba cha mapumziko kabla ya kuelekea kwenye chumba cha mikutano.

IMG_5169
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli (wa pili kulia) kwenye chumba cha mapumziko baada ya kuwasili ukumbi hapo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.

IMG_5182
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, kwenye chumba maalum cha mapumziko.

IMG_5253
Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akimkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kushoto) kufunga rasmi mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014. Kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Magese Mulongo, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu, Mbunge wa Kahama, James Lembeli na Waziri mdogo wa Marekani anayeshughulikia Uchumi, Nishati na Mazingira, Bi. Catherine Novelli wakiwa meza kuu.

IMG_5264
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akizungumza na wadau waliohudhuria mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanayamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014 wakati akifunga rasmi mkutano huo wa siku mbili.

IMG_5198
Mwakilishi wa Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania akichukua taswira za baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea mkutanoni hapo.

IMG_5197
Baadhi ya wadau mbalimbali walioshiriki mkutano huo.

IMG_5236
Baadhi ya wawakilishi kutoka nchi tisa wakitia saini Azimio la Arusha la kukabili ujangili mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Nchi hizo ni Burundi, Kenya, Uganda, Msumbiji, Tanzania, Sudan Kusini, Zambia, Rwanda na Malawi.

IMG_5205
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akizungumza kwa niaba ya Umoja wa Mataifa kwenye ufungaji wa mkutano wa kupiga vita dhidi ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori mjini Arusha Novemba 8, 2014.

IMG_5224
Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke, akizungumza kwa niaba ya serikali ya Ujerumani.

IMG_5212
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Waziri wa Mali asili na utalii, Mh. Lazaro Nyalandu wakati wa ufungaji rasmi wa mkutano huo uliodumu siku mbili jijini Arusha.
IMG_5268
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiondoka ukumbini hapo mara baada ya kuufunga rasmi mkutano huo.

VIPI TENA::KUNA MTU KAIBIWA???

VIPI TENA::KUNA MTU KAIBIWA???

TUNZA MAZINGIRA:::PANDA MITI

WACHA MUVI IENDELEE::MISS TANZANIA EPISODE 2.



Baada ya kuvuliwa taji aliyekuwa miss Tanzania Sitti mtemvu kwa kughushi umri...nafasi ya mimi Tanzania imenyakuliwa na Mshindi wa pili Lilian Kamaziama

Lakini  mshindi huyu wa pili naye inasemekana sio raia wa Tanzania ni mnyarwanda. LILIAN nini mtoto wa generali wa jeshi KAMAZIAMA ambaye inasemekana sio mtanzania ni mnyarwanda na mmoja wa makamanda na jasusi wa jeshi la kinyarwanda aliyepenyezwa na raisi Kagame.

WACHA MUVI IENDELEE::MISS TANZANIA EPISODE 2.



Baada ya kuvuliwa taji aliyekuwa miss Tanzania Sitti mtemvu kwa kughushi umri...nafasi ya mimi Tanzania imenyakuliwa na Mshindi wa pili Lilian Kamaziama

Lakini  mshindi huyu wa pili naye inasemekana sio raia wa Tanzania ni mnyarwanda. LILIAN nini mtoto wa generali wa jeshi KAMAZIAMA ambaye inasemekana sio mtanzania ni mnyarwanda na mmoja wa makamanda na jasusi wa jeshi la kinyarwanda aliyepenyezwa na raisi Kagame.

WACHA MUVI IENDELEE::MISS TANZANIA EPISODE 2.



Baada ya kuvuliwa taji aliyekuwa miss Tanzania Sitti mtemvu kwa kughushi umri...nafasi ya mimi Tanzania imenyakuliwa na Mshindi wa pili Lilian Kamaziama

Lakini  mshindi huyu wa pili naye inasemekana sio raia wa Tanzania ni mnyarwanda. LILIAN nini mtoto wa generali wa jeshi KAMAZIAMA ambaye inasemekana sio mtanzania ni mnyarwanda na mmoja wa makamanda na jasusi wa jeshi la kinyarwanda aliyepenyezwa na raisi Kagame.

MICHEZO::Ushahidi wa Azam FC kukipokea kifaa kipya kutoka Ivory Coast.

k1
Unaambiwa Azam FC wameshamshusha bongo huyu mkali wa soka kama inavyoonekana kwenye picha na wanatarajia kumsajili  beki huyu wa Ivory Coast aitwae Serges Pascal Wawa Sfondo akitokea klabu ya El Mereikh ya nchini Sudan.
Ameingia na ndege ya saa nane usiku wa kuamkia November 10 2014 ambapo millardayo.com na AyoTV ilikua kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam kuhakikisha stori haipiti bilabila.
Imeshindikana kumpata sana Pascal akizungumza kwenye interview kwa sababu hajui kuzungumza lugha nyingine tofauti na za Kiarabu na Kifaransa alizozizoea.
k2
Club alizozichezea ni ASEC Mimomas kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 alipojiunga na Al-Merrikh ya Sudan ambapo kwa mujibu wa mtandao, hajawahi kuzifungia timu hizi goli lolote.
k3
Umri wake ni miaka 28, alizaliwa January 1 1986.
k4
Kwa leo utanisaheme manake picha hazikua kwenye ubora unaotakiwa.
Screen Shot 2014-11-10 at 4.29.23 AM

MICHEZO::Ushahidi wa Azam FC kukipokea kifaa kipya kutoka Ivory Coast.

k1
Unaambiwa Azam FC wameshamshusha bongo huyu mkali wa soka kama inavyoonekana kwenye picha na wanatarajia kumsajili  beki huyu wa Ivory Coast aitwae Serges Pascal Wawa Sfondo akitokea klabu ya El Mereikh ya nchini Sudan.
Ameingia na ndege ya saa nane usiku wa kuamkia November 10 2014 ambapo millardayo.com na AyoTV ilikua kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam kuhakikisha stori haipiti bilabila.
Imeshindikana kumpata sana Pascal akizungumza kwenye interview kwa sababu hajui kuzungumza lugha nyingine tofauti na za Kiarabu na Kifaransa alizozizoea.
k2
Club alizozichezea ni ASEC Mimomas kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 alipojiunga na Al-Merrikh ya Sudan ambapo kwa mujibu wa mtandao, hajawahi kuzifungia timu hizi goli lolote.
k3
Umri wake ni miaka 28, alizaliwa January 1 1986.
k4
Kwa leo utanisaheme manake picha hazikua kwenye ubora unaotakiwa.
Screen Shot 2014-11-10 at 4.29.23 AM

MICHEZO::Ushahidi wa Azam FC kukipokea kifaa kipya kutoka Ivory Coast.

k1
Unaambiwa Azam FC wameshamshusha bongo huyu mkali wa soka kama inavyoonekana kwenye picha na wanatarajia kumsajili  beki huyu wa Ivory Coast aitwae Serges Pascal Wawa Sfondo akitokea klabu ya El Mereikh ya nchini Sudan.
Ameingia na ndege ya saa nane usiku wa kuamkia November 10 2014 ambapo millardayo.com na AyoTV ilikua kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam kuhakikisha stori haipiti bilabila.
Imeshindikana kumpata sana Pascal akizungumza kwenye interview kwa sababu hajui kuzungumza lugha nyingine tofauti na za Kiarabu na Kifaransa alizozizoea.
k2
Club alizozichezea ni ASEC Mimomas kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 alipojiunga na Al-Merrikh ya Sudan ambapo kwa mujibu wa mtandao, hajawahi kuzifungia timu hizi goli lolote.
k3
Umri wake ni miaka 28, alizaliwa January 1 1986.
k4
Kwa leo utanisaheme manake picha hazikua kwenye ubora unaotakiwa.
Screen Shot 2014-11-10 at 4.29.23 AM

MICHEZO::Ushahidi wa Azam FC kukipokea kifaa kipya kutoka Ivory Coast.

k1
Unaambiwa Azam FC wameshamshusha bongo huyu mkali wa soka kama inavyoonekana kwenye picha na wanatarajia kumsajili  beki huyu wa Ivory Coast aitwae Serges Pascal Wawa Sfondo akitokea klabu ya El Mereikh ya nchini Sudan.
Ameingia na ndege ya saa nane usiku wa kuamkia November 10 2014 ambapo millardayo.com na AyoTV ilikua kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam kuhakikisha stori haipiti bilabila.
Imeshindikana kumpata sana Pascal akizungumza kwenye interview kwa sababu hajui kuzungumza lugha nyingine tofauti na za Kiarabu na Kifaransa alizozizoea.
k2
Club alizozichezea ni ASEC Mimomas kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 alipojiunga na Al-Merrikh ya Sudan ambapo kwa mujibu wa mtandao, hajawahi kuzifungia timu hizi goli lolote.
k3
Umri wake ni miaka 28, alizaliwa January 1 1986.
k4
Kwa leo utanisaheme manake picha hazikua kwenye ubora unaotakiwa.
Screen Shot 2014-11-10 at 4.29.23 AM

Saturday, 8 November 2014

MAISHA NI NYUMBA::NSSF YAKABIDHI NYUMBA KWA WASANII WA ORIJINO KOMEDI

Meneja Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abdallah Mselly (kulia) akimkabidhi msanii wa Orijino Komedi, Mjuni Silvery 'Mpoki funguo ya moja ya nyumba za gharama nafuu walizokopeshwa wasanii  wa kikundi hicho na NSSF wakati wa hafla fupi ya kukabidhi wasanii hao zilizopo Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam hivi karibuni, mkopo huo utalipwa kwa kipindi cha miaka 15.
Baadhi ya nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kukopeshwa wasanii wa kikundi cha Orijino Komedi Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizopo katika mradi wa ujenzi wa Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam.

Mac Reagan 'Kipara' na Mjuni Silvery 'Mpoki wakiangalia moja kati ya nyumba walizokabidhiwa na NSSF baada ya kukopeshwa na Shirika hilo na mkopo utalipwa kwa kipindi cha miaka 15.
Kushoto, Mac Reagan, Joti na Mpoki wakiangalia nyumba zao walizokabidhiwa na NSSF.
Meneja Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abdallah Mselly akimkabidhi funguo ya nyumba msanii wa Orijino Komedi.  

Msanii Isaya Mwakilasa 'Wakuvwanga' akipokea funguo ya nyumba yake.

Muandaaji wa vipindi vya Orijino Komedi, Sekioni David 'Seki' akipokea funguo ya nyumba yake kutoka kwa Meneja Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abdallah Mselly (kulia)
Meneja Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abdallah Mselly akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi nyumba kwa wasanii kikundi cha Orijino Komedi.
Msanii Mac Reagan akizungumza baada ya makabidhiano ya nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NSSF Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam.

Muandaaji wa vipindi vya Orijino Komedi, Sekioni David 'Seki' akifafanua jambo wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa nyumba.

Wednesday, 29 October 2014

MAPINDUZI YA UREMBO::UKISTAAJABU YA MISS TZ 2014....!! UTAYAONA YA MISS UGANDA 2014,WAGANDA WADAI NI MBAYA!!!

missuganda
  Miss Uganda 2014 Leah Kalanguka na Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu hawachekani! Wakati Sitti akiwa kwenye kitimoto kwa kudanganya umri wake, waganda wamewakaba koo waandaji wa shindano lao kuwa Leah ni mbaya na hakufaa kuwa Miss Uganda.
“Miss Uganda World is your theme Beauty with a purpose or Ugly with a purpose?” Mganda mmoja aliwauliza waandaji wa Miss Uganda World kwenye Facebook. “Museveni is always embarrassing Besigye, now he declared him Miss Uganda,” alisema mganda mwingine kwenye Twitter.
“And so this Miss Uganda winner, I have been told super heroes are rarely attractive. I hope she can cure cancer.”
“United States is about to Invade Miss Uganda, she looks like Oil.”
Watu mbalimbali wakiwemo mastaa, wamemtetea Leah.
Bebe Cool ameandika: My take on miss Uganda is that I have no problem with her since I did not take part in the process of choosing her at any one time.i don’t understand why Ugandans r complaining yet they did not put in time to attend the events that led to that choice so let’s respect the choice that was made by the few who had time and interest to be there.
Naye Maurice Kirya ameandika:

My Ugandan Girl!

There is something in the way you carry yourself,
your confidence and the way you wear,
there’s something in the way you move,
like a feather gliding through the air
I know you think I got this from a book,
but I believe you were sent from heaven above
My Ugandan Girl.
I realize it’s in your eyes,
that spark that leads to paradise,
I see my future in your eyes,
or am I just so mesmerized?
I know you think I got this from a book,
but I believe you were sent from heaven above,
My Ugandan Girl
Gwe musaayi gwange,
Gwe bulamu bwange,
Gwe Suubi lyange,
Gwe Uganda yange,
My Ugandan Girl.


Congratulations Leah Kalanguka -Miss Uganda 2014-15
Leah aliyekuwa mkulima wa uyoga na mfugaji wa kuku aliteuliwa kuwa Miss Uganda 2014 kufuatia mabadiliko katika shindano hilo ambalo kwa sasa linafanya kampeni kuhusu kilimo. Leah Kalanguka, 23, aliwashinda warembo wengine 19 kwenye fainali hizo ambapo washiriki walitakiwa kukamua ng’ombe na kufanya kazi na kondoo na mbuzi.

Waandaji wa shindano hilo walishirikiana na jeshi la Uganda kulifanikisha na lengo lake ni kupromote ujasiriamali katika ufugaji kwa vijana. Katika shindano hilo, warembo waliulizwa maswali kuhusu kilimo. Kalanguka pia amesoma computer engineering and science katika chuo kikuu cha Makerere.

SIMANZI ZAMBIA::Rais Michael Sata wa Zambia aaga dunia "KING COBRA"

Rais Michael Sata wa Zambia afariki dunia
Familia ya Bwana Sata wameiambia BBC kuwa Rais wa Zambia, Michael Sata, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 77 katika hospitali ya London alikokuwa akitibiwa ugonjwa ambao haujatajwa.
Kifo chake kimetokea siku chache baada ya Zambia kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa nchi hiyo.
Mwanasiasa huyo mkongwe aliingia madarakani mwezi Septemba 2011 baada ya kuongoza chama chake cha Patriotic Front, na kumshinda Rupiah Banda, ambaye alikuwa rais wakati huo na chama chake cha Movement for Multi-Party Democracy, kikiwa madarakani kwa miaka ishirini.
Michael Chilufya Sata alizaliwa mwaka 1937 katika mji wa Mpika, eneo ambalo lilikuwa wakati huo ni Northern Rhodesia. Muumini wa dini ya Kikristo ya madhehebu ya Katoliki, alifanya kazi kama afisa polisi, mfanyakazi wa reli na mwanachama wa chama cha wafanyakazi wakati wa utawala wa kikoloni. Baada ya Zambia kupata uhuru wake, pia aliishi kipindi fulani mjini London, akiwa mfanyakazi wa reli, na kurejea Zambia, akiwa na kampuni ya teksi.
Akiwa mwenye sauti ya mkwaruzo yakiwa ni matokeo ya kuvuta sigara kwa muda mrefu, Bwana Sata aliibuka katika siasa na kupata umaarufu katika miaka ya 1980.
Haraka akapata sifa ya kuwa gavana mwenye kuchapa kazi kwa bidii, wakati akiongoza jimbo la Lusaka na mtu wa utekelezaji kwa vitendo.
Lakini pia alijulikana kama mtu wa kutoa amri, mtu asiyeendekeza urafiki na mkali- na wapinzani wake walisema jina alilopewa la bandia la "King Cobra" alikuwa anastahili kuitwa hivyo.
Kwa mara ya kwanza alionekana kama mtu ambaye angetekeleza ahadi za kupambana na rushwa na kupata ufumbuzi wa tatizo la ajira na kuleta ustawi wa jamii. Lakini kipindi chake madarakani kiligubikwa na kuuzima upinzani wa kisiasa na kudorora kwa uchumi.
Bwana Sata ni rais wa pili wa Zambia kufariki dunia akiwa madarakani.

MAANDAMANO::Vurugu Bukinafaso wakimpinga Rais

 

 
Kumetokea vurugu kubwa baina ya maelfu ya waandamanaji na maafisa wa polisi katika mji mkuu wa Burkina Faso wa Ougadougou, wakati maelfu ya raia wa nchi hiyo walipokuwa wakihudhuria mkutano kupinga marekebisho ya Katiba itakayomruhusu Rais wa nchi hiyo kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Maafisa wa usalama walitumia mabomu ya kutoa machozi dhidi ya wanadamanaji hao ambao walikuwa akiandamana kwenda kwenye majengo ya bunge.
Waandamanaji hao wanapinga kubadilishwa kwa katiba ya nchi hiyo ambayo itaotoa nafasi kwa rais Compaoure kugombea tena nafasi ya urais wa nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Hata hivyo kama ilivyotarajiwa katika maandamano kama haya maafisa wa polisi kama kawaida walikabilana na wanadamanaji hao kwa mabomu ya machozi.
Hadi sasa hakuna taarifa za watu waliojerehiwa au kupoteza maisha katika vurugu hizo.
Tayari vyuo vikuu, shule na maduka yalifungwa kwa wiki moja kabla maandamano hayo yaliyokuwa yamepangwa.
Rais Blaise Compaore alishika madaraka ya nchi hiyo baada ya kuipindua serikali tangu mwaka 1987 ambapo alichaguliwa katika kwa njia ya kidemokrasia kwa kipindi cha miaka miwili mwaka 2005.
Katika mahojiano na BBC hivi karibuni Rais Blaise Compaore aliwahi kusema kuwa atafanya mambo kwa maslai ya nchi hiyo.
Rais Compaire tayari ameshinda uchaguzi wa nchi kwa vipindi vinne. Hata upinzani umekuwa ukihamasisha raia kumpinga na kumlazimisha kuondoka madarakani ifikapo mwaka ujao.

SAMAHANI KWA PICHA HIZI::MBWA WAKUTWA WAKITAFUNA MWILI WA BINADAMU HUKO SONGEA


Fuvu la kichwa likiwa linazolewa 

 Mabaki ya mwili yaliyokutwa katika eneo la kijiji cha Lupapila wilaya ya songea mkoani Ruvuma yakikusanywa na wataalamu kutoka hospital ya mkoa wa Ruvuma.

 MIFUPA ya masalia ya binadamu wa jinsia ya kiume ambaye hakuweza kufahamika jina na kukadiriwa kuwa na miaka (30) yamegundulika na Zaujia Pilly (70) mkazi wa kijiji cha Lupapila wilaya ya songea mkoani Ruvuma

Ruvuma wakati akienda kuchimba dawa za kienyeji baada ya kuwaona mbwa wakishambulia sehemu za mabaki hayo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo limetokea oktoba 26 mwaka huu majira ya saa 9:45 alasiri huko katika kijiji cha Lupapilamtaa wa Mahinya kata ya Subira nje kidogo ya manispaa ya Songea.
 
Alisema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio kwenye msitu wa uwanja wandege ilikutwa mifupa ya binadamu wa jinsia ya kiume ikiwemo fuvu la Kichwa, Mbavu, Mikono na Miguu wakati sehemu ya kiuno na mapaja ikiwa imeharibika vibaya.
 
Alifafanua kuwa mabaki ya mwili huo yaligunduliwa na Zaujia Pilly wakati akienda kuchimba dawa za kienyeji kwenye msitu huo ghafla aliwaona Mbwa wakifukuzana kugombania mabaki ya mwili wa binadamu.
 
Alieleza zaidi kuwa Zaujia baada ya kugundua tukio hilo alitoa taarifa katika uongozi wa serikali ya Mtaa na kisha taarifa zilipelekwa katika kituo kikuu cha polisi cha songea mjini ambako baadaye polisi walifika eneo la tukio wakiwa wameongozana na Daktari kutoka hospitgali ya Mkoa wa Ruvuma ambaye aliyafanyia uchunguzi mabaki ya mwili huo na kubaini kuwa marehemu alikuwa amepigwa na kitu kizito kichwani kwenye eneo la kisogo kilichopelekea kifo chake.

Kamanda Msikhela alisema kuwa kufuatia tukio hilo hakuna mtu yeyote anayehusishwa na jeshi la polisi mkoani Ruvuma linaendelea kufanya chunguzi wa kina juu ya kifo hicho.

 Na Amon Mtega -Songea

Tuesday, 28 October 2014

Unafahamu kilichomfanya Mnigeria kuruka ukuta wa Ikulu ya Marekani? Kisome hapa.

Adesanya 
Moja ya taarifa zilizochukua headline wiki iliyopita ni kuhusiana na tukio la mtu mmoja kuruka ukuta wa ikulu ya Marekani, na baadaye kukamatwa baada ya kushambuliwa na mbwa kabla ya kutiwa nguvuni na walinzi wa ikulu hiyo, Secret Service.
Habari zinasema hii si mara ya kwanza kwa Mnigeria Dominica Adesanya (23) kuruka ukuta wa White House, na safari hii baada ya kumfikisha mahakamani imebainika kuwa ana tatizo la akili hivyo hawezi kushitakiwa akiwa na hali hiyo.
Daily Mail imeripoti kuwa baada ya mahakama kuthibitisha vipimo kutoka hospitali kuwa ana tatizo hilo, mahakama iliamuru awekwe chini ya ulinzi huku akipata matibabu ya ugonjwa huo mpaka Desemba 22 kesi yake itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Adesanya ametolewa mahakamani hapo akipiga kelele za kuomba msaada huku akilaumu kitendo cha kukamatwa kwake.
Hii ni mara ya pili kwa jamaa huyo kuruka ukuta wa White House, ambapo mara ya kwanza Adesanya ambaye ana asili ya Nigeria kufanya hivyo ilikuwa Julai 27 majira ya saa 4 usiku mwaka huu, na kurudia tena Oktoba 23 majira ya saa 1 jioni.
White-House-jumper-jpg

CHINA::China kufuta hukumu ya kifo?

death_penalty
Bunge la China limeazimia kuondoa hukumu ya kifo kwa baadhi ya makosa ambapo rasimu ya mapendekezo ya marekebisho ya katiba tayari imewasilishwa katika bunge la nchi hiyo.
Rasimu ya mabadiliko hayo imewasilishwa kwa ajili ya kusomwa kwa mara ya kwanza katika kikao cha bunge hilo ambacho kinatarajiwa kukaa kwa muda wa miezi 2.
Katika mapendekezo hayo, makosa ambayo yametakiwa kuondolewa adhabu ya hukumu ya kifo ni pamoja na kosa la usafirishaji ama kumiliki silaha na nyuklia kinyume cha sheria, fedha badhia, kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu, kujishughulisha na biashara ya ukahaba, kumzuia askari au mwanajeshi kutimiza wajibu wake, na kuzusha uvumi wa uongo wakati wa kupigana vita.
Iwapo mabadiliko hayo yakifanyika, wale ambao wamekwishahukumiwa adhabu hiyo, watabadilishiwa hukumu na badala yake kukabiliwa na kifungo cha muda mrefu zaidi.
China inatajwa kuwa ni moja ya nchi zinazoongoza kutoa hukumu ya kifo, ambapo taasisi moja ya haki za binadamu ya Dui Hua imesema kwa mwaka jana peke yake China imehukumu kifo kwa takribani watu 2,400 huku kukiwa hakuna takwimu rasmi zilizopatikana mpaka sasa juu ya idadi ya watu wanaonyongwa kila mwaka nchini humo.

HUZUNII::AJALI YA KUTISHA JETI LUMO DAR


Gari aina ya Toyota Hiace inayobeba abiria ikiwa imekandamizwa na container baada ya kuangukiwa

Kumetokea ajali mbaya jioni hii maeneo ya Jeti Lumo mwisho wa lami Wilaya ya Temeke jijini Dar ambapo gari kubwa la mizigo limeangukia Daladala iliyokuwa kituoni. Ajali hiyo imetokea wakati gari hilo semi-trailer ikikata kona pale mwisho wa lami ambapo kontena lilianguka na kutua juu ya bodi ya daladala.
Mtoa taarifa wetu amesema hali ni mbaya na bado haijajulikana idadi ya vifo na majeruhi kwa ujumla. Pia gari imepondeka sana jambo ambalo linaashiria hatari zaidi.
Kuna gari la kunyanyua makontena limeshafika pale lakini limeshindwa kutoa msaada wa uhakika kutokana na kuzidiwa uzito na kontena ambapo likijaribu kunyanyua kontena kushuka chini na kuzidi kuongeza maafa.
PICHA NA MDAU: GLOBALA WhattAp