Thursday 21 August 2014

FLAVIANA MATATA:NA UTATA WA KUCHUMBIWA......soma pole pole...

Posted by GLOBAL on August 21, 2014
Stori:  ERICK EVARIST

MISS Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata amezua utata wa aina yake baada ya picha zinazomuonesha katika tukio la kuchumbiwa kunaswa na mwenyewe kudai si yeye aliyechumbiwa.
Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo limedaiwa kufanyika kwa siri hivi karibuni nyumbani kwa miss huyo, Shinyanga na kuhudhuriwa na baadhi ya ndugu wa karibu.
“Inaonesha hawakutaka watu wajue maana hata hakukuwa na watu…
Stori:  ERICK EVARIST
MISS Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata amezua utata wa aina yake baada ya picha zinazomuonesha katika tukio la kuchumbiwa kunaswa na mwenyewe kudai si yeye aliyechumbiwa.
Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo limedaiwa kufanyika kwa siri hivi karibuni nyumbani kwa miss huyo, Shinyanga na kuhudhuriwa na baadhi ya ndugu wa karibu.
“Inaonesha hawakutaka watu wajue maana hata hakukuwa na watu wengi siku hiyo, hata hao ndugu wenyewe hawakuwa wengi kiivyo lakini picha zinaonesha Flaviana akichumbiwa,” kilisema chanzo hicho.
Kikizidi kumwaga data chanzo hicho kilidai kwamba, mwanaume anayetaka kumuoa mrembo huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja ni Mchaga mwenye fedha zake aishiye Marekani.
“Nasikia huyo bwana wake ni Mchaga lakini anaishi Marekani, atakuwa ana fedha zake si mtu wa hivihivi,” kilisema chanzo.
Flaviana Matata akiwasalimia wazee kwa kupiga magoti.
Amani lilifanikiwa kuzinasa picha hizo ambazo zinamuonesha mrembo huyo akiwa amepiga magoti huku amemshika mkono mmoja wa wazazi wake aliyeshiriki katika hafla hiyo ya kupokea mahari.
Baada ya kupata madai hayo, paparazi wetu alimtafuta Flaviana kwa njia ya simu ya mkononi ndipo alipokataa katakata kuwa si yeye aliyekuwa akichumbiwa bali ni dada yake.
“Hamna kitu kama hicho,  unayesema alikuwa anachumbiwa si mimi ni dada yangu, mila za kwetu Shinyanga nalazimika mimi kumsindikiza hivyo kama umeona picha hizo uelewe hivyo,” alisema Flaviana.
Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa ni la Flaviana na si dada yake hivyo kuzidi kuzua utata juu ya ukweli halisi, Amani linaendelea kufatilia kwa karibu.

No comments:

Post a Comment