Thursday 21 August 2014

HUYU NDO MREMBO WA BONGO MOVIE ANAYEBADILI SANA NAMBA ZA SIMU

WOLPER NDO BINGWA WA KUBADILI NAMBA ZA SIMU

Posted by GLOBAL on August 21, 2014
Na Mwandishi Wetu

KUNA nini kwani? Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper anatajwa kuongoza wasanii wenzake kwa kubadili namba za simu za mkononi huku baadhi ya mashoga zake wakijiuliza kulikoni?
Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper.
Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu na Wolper (jina lipo), anamshangaa sana shoga yake huyo kwani amekuwa akibadili namba za simu kwa mwaka mmoja hata mara saba.
“Unajua kwa maisha ya sasa, simu ikipotea mtu unairinyuu laini yako ileile, maana ndiyo…
Na Mwandishi Wetu
KUNA nini kwani? Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper anatajwa kuongoza wasanii wenzake kwa kubadili namba za simu za mkononi huku baadhi ya mashoga zake wakijiuliza kulikoni?
Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper.
Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu na Wolper (jina lipo), anamshangaa sana shoga yake huyo kwani amekuwa akibadili namba za simu kwa mwaka mmoja hata mara saba.
“Unajua kwa maisha ya sasa, simu ikipotea mtu unairinyuu laini yako ileile, maana ndiyo inayojulikana na wadau. Lakini yule mwenzetu siyo. Nimeshamsevu kwenye simu yangu kwa majina ya Wolper, Wolper Tena, Wolper Nyingine, Wolper Nyingine Kabisa na Wolper Hakuna Tena, lakini zote kwa sasa hazipo hewani,” alisema shoga yake huyo huku akicheka.
Wolper alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi iliyozoeleka, hakupatikana. Jitihadi zilifanyika akaja kupatikana kwenye namba mpya ambapo alisema:
“Mimi nikishapoteza laini naona uvivu kwenda kuirinyuu, ndiyo maana nanunua nyingine.”

No comments:

Post a Comment