Monday 18 August 2014

KAULI YA UWOYA JUU ya DIAMOND na ndoa YAKE...

Diamond Hajavunja Ndoa Yangu-Irene Uwoya

Monday, August 18, 2014
Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya amefunguka  katika ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live na kusema kuwa yeye hajaachana na mumeo wa ndoa na wala msanii Diamond Platnum hajavunja ndoa yao kama ambavyo baadhi ya watu na vyombo vya habari walivyokuwa wakisema.
Uwoya ameweka wazi suala hilo baada ya mashabiki wengi kutaka kujua kama ameachana na mumeo ndikumana na ndipo hapo amekanusha kuwa hajawahi kuwa na mahusiano na Diamond Platnum wala Msanii Msami Baby kama ambavyo watu wamekuwa wakijua ni wapenzi bali amesema kuwa yeye na msanii Msami ni marafiki wa karibu na sasa wanafanya filamu ya pamoja.