Friday 15 August 2014

UMEPANIC DIAMOND PLATINUMZZZZ!!!!!!!!!!!

Diamond Amepanic Kuwajibu Mashabiki wa Wema, Majibu Yake Yanaweza Tia Doa Mapenzi Yao

Written By Udaku Specially on Friday, August 15, 2014 
Leo Diamond Aliamua Kuwajibu Mashabiki wa Wema Sepetu walio mshutumu anamtumia Wema Kwa Faida yake
Bahati mbaya, majibu ya Diamond kupitia Instagram yamekuwa makali kiasi cha kuwashtua wengi na kuona kama kamkosea heshima mpenzi wake. Kwakuwa sitaki kuonekana kama namhukumu Diamond kwa kile alichoandika, ningependa kuongea kwa lugha ya busara kadri iwezekanavyo, na isitoshe nimegusia suala la ‘udhaifu’ na ‘ubinadamu’ katika aya zangu za mwanzo.

Diamond ametumia kauli nzito na ya hasira kidogo katika kuwajibu vinara wa kampeni hiyo. Si jambo la busara kumuita mtu umpendaye kwa kuandika ‘msanii wenu’ baada ya jina lake, pale alipoanza kwa kuandika: Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Msanii wenu’. Ingekuwa vyema kama angeandika; Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Wema Sepetu’. Again, hizo ni hasira tu na ndio maana aliamua kuifuta post hiyo.

Kwa maelezo aliyoyatoa staa huyo, imebainika wazi kuwa ni Wema ndiye aliyeamua kuishi hivyo na pengine ameridhika na hatua aliyofikia. Inavyoonekana Diamond hapendwezi na muenendo na maisha ya mpenzi wake hasa kwa kudai anaendekeza urafiki na watu wanaopenda anasa na kula bata.

Mngemshauri apunguze mashoga wapenda anasa na apunguze starehe zisizo na faida, wenda ingemsaidia pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe,” yanaendelea kusomeka majibu ya Diamond. Maelezo hayo yanaeleweka wazi kuwa Wema amekuwa ni mtu wa starehe na kula raha na marafiki zake (Aunty Ezekiel haikwepi hii sentensi, inamhusu). Kwa kauli ya Diamond, Wema anaonekana kuendekeza ulevi kwa kutumia fedha anayopewa na mchumba wake.

Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumwezesha mtaji wa kufanyia kazi.”

Sentesi hiyo inamaanisha kuwa, Diamond anatimiza wajibu wake na tayari amempa mtaji mpenzi wake. Kuna taarifa pia kuwa hata filamu yake ya Family aliyoigiza na Aunty Ezekiel ilidhaminiwa na Diamond.

Waswahili wanasema mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka ng’ombe wake kwenye maji safi, ila yeye ng’ombe mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji,” anaendelea Diamond. “Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ? Nisiende studio nikae dukani nimuuzie mie? Ni juhudi zako kwanza.”

Maneno ya Diamond yanajielezea yenyewe kuwa Wema amejisahau. Maswali ya wengi ni kuwa wao kama wapenzi hawajawahi kuzungumza haya na kushauriana? Diamond hajawahi kumkanya mpenzi wake kuwa mwenendo wake sio? Au ameshamuambia hadi amechoka na ndio maana ameamua kuuambia umma kile kinachoendelea?

Kwa lawama na matusi ambayo Diamond ameyapata kutokana na kampeni hiyo, ilikuwa inahitaji uvumilivu wa hali ya juu kukaa kimya. Nahisi uvumilivu ulimshinda na ndio maana aliamua kuandika alichokiandika ambacho bahati mbaya kinaweza kutia tena doa uhusiano wao. Sijui Wema atasemaje!!