Friday, 22 August 2014

JOKATE IS ALREADY TAKEN JAMAN.....HUYU NDO ANAEMMALIZA

Jokate Apost Instagram Ujumbe Wenye Utata Kuhusu Huyu Mwanaume.

Friday, August 22, 2014
Katika Kupita Pita kutafuta Umbea wa Leo Udaku Special Nimekutana na Picha alizopost Jokate Akiwa na Mwanaume Mmoja Kutoka Kenya Anayejulikana Kwa Jina Nick Mutuma , Jokate Mwogelo Ameandika Katika Hiyo Picha Kuwa "Huyu Ananimaliza nampeleka kwa Babu wangu wa Kingoni" . 

Jokate is Taken Jamani 





NAYE YUPO KUMBE:Q-CHILLAH ALAMBA MKATABA MNONO

Q-CHILLAH ALAMBA MKATABA MNONO


Mbongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ akipokea mkataba kutoka 'QS Mhonda J Company'.
 
'Legend' kwenye gemu la Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ akipozi.

LEGEND kwenye gemu la Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ amelamba mkataba wa nguvu kutoka QS Mhonda J Company ambao ndiyo watakaokuwa wakimsimamia kazi zake zote za muziki kwa sasa.
Mmiliki wa kampuni hiyo, Joseph Mhonda amesema atahakikishia anamsaidia kwa gharama yoyote nguli huyo ili arudi pale alipokuwa na kwenda mbele zaidi ikiwa pamoja na kuzindua bendi itakayokuwa ikifanya kazi zake na wasanii wenzake watakaosimamiwa na kampuni hiyo.
Akizungumzia hatua hiyo kubwa katika maisha yake ya muziki, Chillah alisema:
“Kwa miaka mitano nimekuwa kimya  kwenye radio na anga ya muziki kwa jumla ikiwa ni sehemu ya kuyapitia maisha mengine nje ya muziki but  thanks to God sikutegemea kupata mkataba mkubwa wa kunirudisha tena kwa nguvu zote kwa Watanzania waliomisi muziki mzuri kutoka kwangu, soon ngoma zitaanza kudondoka,” alisema Chillah.

DJ FETTY.....AWA KINUNDA KWA KUDUNDA WATU.

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
 
 Stori: Musa Mateja

MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga.
 
Mtangazaji wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa…
 
Stori: Musa Mateja
MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga.
 
Mtangazaji wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa kumuona akizichapa na mrembo huyo ikidaiwa walizinguana, hata hivyo waliamuliwa kabla mambo hayajawa mabayaw.
Ziara ya Tamasha la Fiesta kesho itahamia Tanga ambapo wasanii kibao wataangusha burudani ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.

BONGO MUVI...MUVI BADO INAENDELEA

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
Na: Gladness Mallya na Imelda Mtema

JAMBO limezua jambo! Baada ya hivi karibuni wasanii wa Bongo Muvi (Movie) kufanya dua kwa ajili ya wenzao waliofariki dunia, baadhi ya ndugu wa marehemu wamecharuka na kudai kuwa waandaaji wa kisomo hicho walifanya kwa manufaa yao binafsi.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya ndugu wa marehemu wanalalamika kuwa dua hiyo iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity,…
Na: Gladness Mallya na Imelda Mtema
JAMBO limezua jambo! Baada ya hivi karibuni wasanii wa Bongo Muvi (Movie) kufanya dua kwa ajili ya wenzao waliofariki dunia, baadhi ya ndugu wa marehemu wamecharuka na kudai kuwa waandaaji wa kisomo hicho walifanya kwa manufaa yao binafsi.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya ndugu wa marehemu wanalalamika kuwa dua hiyo iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na kufanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar, ilikuwa ni kwa ajili ya kujipatia fedha yeye ndiyo maana hakuona haja ya kuwashirikisha.
“Dua ilifanyika lakini baadhi ya ndugu wa marehemu hawakuambiwa na wanalalamikia sana kitendo hicho kwani si cha kiungwana, kimsingi mamilioni waliyopewa na mdhamini wa shughuli yametumika vibaya,” kilidai chanzo hicho bila kueleza fedha hizo zimepatikana wapi.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba akizungumza jambo.
Baada ya malalamiko hayo kutua mezani, mapaparazi wetu waliwatafuta ndugu wa marehemu ambao hawakuonekana kwenye dua hiyo ambapo walifunguka kwa nyakati tofauti:
MKE WA MZEE SMALL
Bi. Fatuma Said ambaye ni mke wa aliyekuwa mkongwe wa maigizo nchini, marehemu Said Ngamba ‘Mzee Small’ alisema kwamba hawakupewa taarifa wao kama familia jambo ambalo limemsikitisha sana.
Aliyekuwa mke wa muongozaji wa filamu Bongo(George Otieno Tyson) Beatrice Shayo.
“Imeniuma kwa kweli kwani sisi wajane tunatengwa sana, yaani wasanii wakishazika hakuna anayerudi nyuma tena, kitendo cha kutokututaarifu kuhusu dua kimeniumiza sana jamani tungepewa tu taarifa,” alisema Fatuma.
BEATRICE SHAYO ‘MKE WA TYSON’
Huyu ni mwanadada aliyekuwa mke wa marehemu, George Otieno ‘Tyson’ ambaye naye alikiri kwamba hakuwepo kwenye dua kwa sababu hakuwa na taarifa.
Aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, marehemu Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ enzi za uhai wake.
“Sikujisikia vizuri na imeniuma sana kwani sikujua inafanyika wapi na imeandaliwa na nani, ukweli walioandaa hawakufanya vizuri kwani walipaswa kutushirikisha sisi wahusika ili tuwe kitu kimoja, sasa nashangaa walifanyaje dua wakati ndugu na jamaa wa marehemu hawana taarifa?” alisema Beatrice.
MAMA SHARO
Mama wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ ambaye alisema kwamba hakuwa na taarifa yoyote kuhusu dua na ndiyo alisikia kutoka kwa mwandishi.
“Ndiyo nasikia kwako, ukweli nimeumia kutokupewa taarifa kwani ningejumuika na mimi kwa ajili ya kumuombea mwanangu, naona wamenitupa na kunisahau kabisa, wasanii msiwe mnanitenga hivyo jamani!” alisema Mama Sharo.
Aliyekuwa mkongwe wa maigizo nchini, marehemu Said Ngamba ‘Mzee Small’ enzi za uhai wake.
SETH BOSCO
Ni mdogo wa marehemu Steven Kanumba ambaye alitafutwa baada ya simu ya mama Kanumba kuita bila kupokelewa ambapo alisema wao kama familia hawakupewa taarifa ndiyo maana hawakuonekana kwenye dua hiyo jambo ambalo limewahuzunisha.
“Aliyeandaa dua hiyo hakufanya jambo la kiungwana, tumejisikia vibaya sana kwani suala kama hilo walitakiwa kuwafuata wahusika na kuwaalika tena ikiwezekana washirikiane kwa pamoja lakini walifanya kwa ajili ya kujipatia fedha tu hakuna chochote,” alisema Seth.
Marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake.
MSIKILIZE RAIS
Naye Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba alilaani vikali kitendo hicho na kusema waandaaji hawakufuata utaratibu.
“Walitakiwa kuwashirikisha wahusika na mazingira haya tata ndiyo maana maswali yanakuwa mengi vinywani mwa watu kwamba hakikuwa kitu chema na cha uungwana,” alisema.
NYERERE SASA!
Akizungumza muandaaji mkuu wa shughuli hiyo, Steve Nyerere alisema wahusika wote walipewa taarifa japokuwa aligawana majukumu na watu wengine kwani asingeweza kuwafikia wote.
“Sisi tuligawana majukumu na nilituma watu kwa wahusika sasa kama hawakuwa na taarifa siyo kosa langu ni la kwao hao niliowapa hilo jukumu, hatukufanya shughuli ile kwa masilahi binafsi zaidi ya kuwakumbuka ndugu zetu,” alisema Steve pasipo kufafanua zaidi.

OLD BUT GOLD:REAL MADRID YA ZAMAN VS MBWA MKALI KWAO KESHO HIYO

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
Mratibu wa Ziara ya Wachezaji wa Zamani wa Timu ya Real Madrid,Ssebo (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mechi ya kirafiki kati ya Tanzania Eleven na Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kesho.Mpaka sasa ni wachezaji watatu tu ndio waliowasili nchini huku wengine kadhaa wakitegemewa kuwasili mchana wa leo.Wachezahi hao ambao wapo nchini hivi sasa ni Luis Figo (wa tatu kulia),Christian Karembeu (kulia) na Beki Fernando Sanz Duran (wa pili kushoto).wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TSN,Farough Baghoza na Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven, Jamhuri Kihwelo 'Julio'.…
Mratibu wa Ziara ya Wachezaji wa Zamani wa Timu ya Real Madrid,Ssebo (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mechi ya kirafiki kati ya Tanzania Eleven na Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kesho.Mpaka sasa ni wachezaji watatu tu ndio waliowasili nchini huku wengine kadhaa wakitegemewa kuwasili mchana wa leo.Wachezahi hao ambao wapo nchini hivi sasa ni Luis Figo (wa tatu kulia),Christian Karembeu (kulia) na Beki Fernando Sanz Duran (wa pili kushoto).wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TSN,Farough Baghoza na Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven, Jamhuri Kihwelo 'Julio'.
Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven,Jamhuri Kihwelo "Julio" (katikati) akizungumzia namna Timu yake ilivyojiandaa kuwakabili Wakali hao wa soka Duniani wakati wa Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo kwenye Hoteli ya SouthernSun jijini Dar es Salaam.Kulia ni Luis Figo na kushoto ni Fernando Sanz Duran ambao ni wachezaji wa zamani wa timu ya Real Madrid ya nchini Hispania.
Mchezaji Kiongozi wa Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid,Luis Figo akizungumza na Waandishi wa habari juu ya ujio wao hapa nchini.Figo amewaahidi wa Tanzania kuwa yeye na Wenzake watatoa burudani kabambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar hapo kesho.
Mchezaji Fernando Sanz Duran (kati) nae akitoa maneno yake kuhusu mchezo huo.
Mwanasoka Christian Karembeu akizungumza.

HIVI NDO VITU WAPENDAVYO WANAWAKE...but mmmhhh?

Wanawake Hufurahishwa na Vitu Vidogo Vidogo Sana Hakuna Haja ya Gharama

Udaku Special Limebaini Kuwa Sasa hivi imekua ni kawaida mtu kutumia pesa nyingi labda kumpeleka mpenzi wake kwenye mahotel makubwa au kumnunulia vitu vya thamani ili kumuonyesha mapenzi, ila ukweli ni kwamba unaweza ukafanya hayo yote ukajiingiza kwenye gharama kubwa na matumizi usiyotarajia  bila mafaniko. Mwanamke haitaji vyote hivyo mwanamke anahitaji muda, tumia muda mwingi kuwa nae, muonyeshe unamjali, tatizo lake chukua liwe lako. Mpe kidogo ulicho nacho na kitoke moyoni, Usilazimishe mambo utamboa, fanya ajiamini ukiwa nae, kuwa na misimamo yako usiyumbe yumbe katika maamuzi, Usiogope kumwambia hisia zako kwake, kwani wanawake wanapenda mtu anayejiamini. Fanya hayo utaona matokeo yake..!! 

POLE KAMA ULIPATA KAZI UHAMIAJI.... ISOME KWA MAKINI

POLE KAMA ULIPATA KAZI UHAMIAJI....
Week Kama tatu zilizopita Udaku Special tuliweka Habari kuhusu Majina ya Waliofauli Usaili wa Nafasi ya Ukonstebo na Koplo Pale Uhamiaji ambayo ilisemekana yalikuwa yamechakachuliwa kwani wengi waliopata kazi hiyo walikuwa na undugu na wafanyakazi wa Idara hiyo, Baada ya Habari hiyo Serekali ilisimamisha mchakato huo kupisha uchunguzi , Leo taarifa zimepatikana kuwa ni ukweli majibu ya usaili huo yalichakachuliwa na kuwaacha waliofaulu na wahusika kuweka ndugu ama jamaa zao hivyo basi matokeo ya usaili huo yamefutwa rasmi Mpaka hapo Utakapofanyika Usaili Mwingine 

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil alisema hatua hiyo imechukuliwa baada ya kamati maalumu ya kuchunguza ajira hizo kubaini wazi kwamba waliopewa nafasi hizo hawakukidhi vigezo.

Abdulwakil alisema wizara imesikitishwa na udhaifu huo baada ya kubainika wazi kwamba malalamiko yaliyotolewa na wananchi na kusababisha wizara kuingilia kati na kufuta usaili wa kuitwa kwenye ajira kwa watu 200 ulikuwa sahihi.


Alisema baada ya kubainika kwamba kweli kulikuwa na upendeleo wa dhahiri kwani watahiniwa wenye sifa na waliopata alama za juu wakati wa usaili hawakuitwa na kukiukwa kwa vigezo vya wazi, ajira hizo zitatangazwa upya na kusimamiwa moja kwa moja na wizara na siyo idara hiyo kama ilivyokuwa awali.

LULU AHONGWA HELA ILI ANUNUE GARI wakati akina nani WANAHONGWA GARI...NANI MJANJA?

Lulu Michael Aonyesha Kadi ya Gari yake Mpya, Aseme yeye si Kama Wakina Nanii Wanaohongwa

Friday, August 22, 2014
Kwa Kuonyesha kuwa yeye ni Tofauti na Mastaa Wengine wa Kike Walioingia katika Mkumbo wa Kuhongwa Magari wakati kadi ya Gari lina jina la muhongaji ambayo upelekea kunyang'anywa Penzi likiisha Mrembo Lulu Michael Ameonyesha Kadi ya Gari Lake Jipya aina ya Rav 4 New Model ,
Lulu Amesema yeye si Mswahili ndo maana ameamua kuonyesha kadi ya gari yenye jina lake ili kutowapa nafasi watu kusema amehongwa , Ameongeza kuwa yeye si kama wakina nanii ambao waliohongwa na kunyang'anywa magari... Hongera sana Lulu Michael Kwa Gari Jipya.

BOKO HARAM:KAMA CHUO CHA POLISI KINATEKWA,VIPI USALAMA WA RAIA NA MALI ZAKE?

Boko Haram Wateka Chuo Cha Polisi

 
Boko Haram wazidi kumlaza macho Raisi Jonathan Moyo
Kundi la wapiganaji la kiislam la Boko Haram,wamevamia shule moja ya mafunzo ya kipolisi.kituo hicho cha mafunzo kilichoko kwenye kitongoji cha Gwoza kiko karibu na mpaka wa nchi ya Cameroon ambacho hufundisha maofisa wa Polisi nchini Nigeria.
Kikundi hicha Boko Haram pia kinasemekana kuudhibiti mji wa jirani na Gwoza uitwao Buni Yadi.
Nalo shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch wametoa takwimu ya vifo vilivyosababishwa na kundi hilo kua watu zaidi ya elfu kumi mpaka sasa tangu walipoanzisha harakati za kutaka upande wa kaskazini mwa Nigeria uwe chini ya utawala wa Kiislam.

Kwanini kila baada ya kombe la dunia tu?Shakira Atuhumiwa Kuiba Wimbo

Shakira Atuhumiwa Kuiba Wimbo

 22 Agosti, 2014

Mwimbaji nguli wa pop Shakira atuhumiwa:
Wimbo uliovuma wa mwimbaji wa Pop Shakira ulinakiliwa kwa njia isiyo ya moja kwa moja kutoka kwa kazi ya mtungaji mwingine wa nyimbo, jaji mmoja mjini New York amegundua.
Jaji Alvin Hellerstein alisema toleo la wimbo “Loca” la lugha ya kihispania 2010 lilikiuka haki za umiliki za wimbo wa mwimbaji Ramon Arias Vazquez.
Toleo la Ramon la “Loca” kwa lugha ya kiingereza- lililotumika katika Dizzee Rascal – “halikutolewa kama ushahidi,” katika kusikizwa kwa kesi hiyo.
Hakuna toleo lolote kati ya matoleo hayo mawili lililotolewa Uingereza.
Hata hivyo, toleo la kihispania – linalomshirikisha Eduard Edwin Bello Pou, anayefahamika kama El Cata – lilitolewa na kuvuma kote ulimwenguni na kuuza zaidi ya kanda milioni tano na kuongoza kwenye chati za kilatino kwenye Billboard Magazine.
Aidha, wimbo huo ulikuwemo kwenye albamu yake ya 2010 ‘Sale el Sol’ iliyouzwa kwa wasikilizaji wa Kiingereza na mada ya “The Sun Comes Out,” na matoleo yote mawili ya wimbo huo yalikuwemo.
Katika uamuzi uliotolewa Jumanne, jaji Hellerstein alisema kuwa, japo wimbo huo ulikuwa umetungwa ukifuata wimbo uliokuwa umerekodiwa hapo awali na Bello [El Cata], pia ulikuwa umenakiliwa kutoka kwa wimbo mwingine wa Arias Vasquez.
"Hakuna shaka kuwa toleo la Shakira la wimbo huo lilitungwa likifuata toleo la hapo awali la Bello,” jaji huyo aliandika kwenye uamuzi wake.
"Kwa hiyo, nimepata kuwa, kwa kuwa Bello alinakili Arias, yeyote aliyeandika toleo la Shakira pia alinaliki kwa njia isiyo ya moja kwa moja Arias,” alikata kauli.
Ramon Arias Vazquez alitunga wimbo Loca con su Tiguere miaka ya 1990, lakini Bello amekana kuunakili wimbo huo.
Uamuzi unatarajiwa kuelekeza fidia atakayolipwa mlalamikaji Mayimba Music, mmiliki wa haki miliki za hati ya Aria.
Sony ilisambaza matoleo yote mawili ya wimbo wa Shakira, toleo la Kiingereza, na la Kihispania, lakini tuhuma zilizotolewa ziliangazia toleo la kihispania.
Tarehe 13 Julai, Shakira, mwimbaji wa Colombia, alitumbuiza umati na wimbo huo katika sherehe ya kuhitimisha kombe la Dunia huko Rio de Janeiro.

DIVA KWA KING CRAZY GK AMEOZA MPAKA BASI!!!!

Diva:Sijampenda Gk Sababu ya Pesa Au Umaarufu Nampenda Yeye Kama Yeye

Udaku Specially on Friday, August 22, 2014
Ile hatua ya U boifriend na U girlfriend ikiwa imepita na kuingia katika hatua ya uchumba wa mahaba kedekede, dada yetu Diva alijikuta anamwaga chozi baada ya watu mbalimbali kumtupia maneno kwamba amempendea King Crazy Gk umaarufu wake ili abaki kupata KIKI Mjini.
Diva alijikuta anatoa maneno makali ya hasira na kuangua kilio na kudai kuwa hajampendea Gk umaarufu wake sababu yeye ni Diva ni maarufu pia hapa Tanzania, hakuishia hapo alizidi kudai ya kuwa amechoshwa na watu wengi kusema ana mahusiano na Gk ambae hana Pesa na ameachana na mwanaume ambae anapesa na cheo kikubwa Tanzania.
Diva:Nimechoshwa kuulizwa maswali ya Prezzo au mwanasiasa sababu huko siko tena na sina mahusiano nao zaidi ya urafiki wa kawaida wa kuongea nao kama watanzania wenzangu na pili amedai kuwa hana hisia zozote za kimapenzi na watu hao sababu yeye yuko na Mpenzi wake na anafurahia mapenzi hayo na mume wake ambae ni Mungu wa Muziki Tanzania.
Diva Binti mwenye mvuto na umbo la kuvutia na mvuto wa sura ya babyface na macho ya duara alidai kuwa King Crazy Gk ni Mtu mwenye kipato kizuri tu ila sio mtu wa kujionyesha au kuishi maisha ya kujionyesha na ni mtu mtaratibu anaeishi maisha yake alioridhika nayo na anatumia pesa zake kulipia elimu na kufanya mambo yake na biashara zake binafsi tofauti na watu wanavyomfikiria. Diva la Diva alisema kuwa Hakumpendea Gk Pesa au Umaarufu wake amempenda yeye kama yeye na anachukia baadhi ya watu kumuingilia kimawazo maisha yake ya mapenzi ambayo mashabiki wengi wameonekana kuvutiwa nayo kupitia mtandao wa instagram.

PESA ZA DIAMOND ZAITISHA SERIKALI....MPAKA WAKAHISI NI PUSHA KUMBE ZA SHOW TU..

Fahamu Kiwango Kipya Anacholipwa Diamond Kwa Show Moja ya Mziki Hapa Tanzania

Udaku Specially on Friday, August 22, 2014
Tangu mwaka juzi tulifahamu kuwa Diamond Platinumz ndiye msanii wa Tanzania anaelipwa kiasi kikubwa cha pesa, na mwaka jana ikaelezwa kuwa bila milioni 10 au 8 za Kitanzania humpati kwenye show yako.

Lakini kiwango kipya kilichotajwa jana kitawapa kizunguzungu zaidi hasa mapromota wenye mitaji midogo wenye ndoto za kufanya kazi na mwimbaji huyo.

Kwa mujibu wa, Babu Tale ambaye ni meneja wake, hivi sasa kiwango cha chini anachochaji kwa show moja hapa nchini ni $15,000 (sawa na shilingi Milioni 25 za Tanzania).

“Tuna show Marekani show kumi na tano (15), show kumi na tano dola elfu ngapi? Na kwa hapa Tanzania hatufanyi show chini ya dola e15,000.”  Babu Tale aliiambia Bongo5.

Kwa mujibu wa Babu Tale, wanachaji kiasi cha hadi dola 25,000 kwa show moja za nje ya nchi (ikiwemo Marekani).

“Tunalipwa milioni 20 show moja, tunalipwa dola elfu 25,000 show moja, hii ni zaidi ya madawa ya kulevya.” Alisema wakati akikanusha tuhuma kuwa Diamond anauza dawa za kulevya.

Kwa mahesabu ya haraka haraka, shows 15 mara dola 25,000 ni sawa na  $375,000 (Sawa na shilingi za Tanzania 625,687,500).

Yesss! Ni zaidi ya Milioni mia sita ishirini na tano za kitanzania.

Kama ni kweli, basi Diamond anastahili kweli kuitwa Dangote wa Bongo Flava.

Bado michongo inaendelea kumiminika ambapo hivi karibuni meneja wa Trey Songz alimtumia ujumbe kuwa atakapokuwa na nafasi amshitue waongee.


Thursday, 21 August 2014

KATUNI:MECHI ZA UGENINI HIZO(MICHEPUKO)

HUU NDO USHAURI ALIOPEWA CHID BENZZZZ......

Chid Benz Zingatia Haya ili Usirudi Ulipotoka La Sivyo Tutakupoteza Kama Wengine

Udaku Specially on Thursday, August 21, 2014
Kati ya watu ambao hawakufiri kama msaanii Chid benz angeweza kurudi vyema kwenye ulingo wa muziki Mimi ni mmoja wapo maana nilihisi kama huyu mtu amesha changanyikiwa na amepoteza uwezo wa kufikiri au kukaa chini akatunga wimbo mzuri tena.

Pengine mwenendo wake na tabia zake zilimponza na sasa amejua pakurekebisha. Chid Benz ni kati ya wasanii waliopendwa na wengi na alipata mafanikio makubwa kupitia mziki wake na akabweteka na kujisahau!

Ujio wake mpya umenifurahisha sana na hakika tunaanza kumuona Chid Benz yule wa wimbo kama" Dares-salaam stand up" na nimefarijika sana kumsikia karudi rasmi na huyu ndio Chid benz ambaye tumekuwa tukimfahamu.

Wanajamvi hasa wale wapenzi wa burudani kama mmepata nafasi ya kuusikiliza wimbo wake unaoitwa "Mpaka kuchee" ambao amewashirikisha Diamond na Ay mtakubaliana nami kuwa huyu ndio Chid Benz mwenyewe maana mule ka rapu vyema naona sasa yuko serious!

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni ...Diamond anajua kutumia nafasi anazopewa hasa kwenye kuimba, kwakweli kwenye wimbo huu kaimba vizuri sana na kautendea haki wimbo huu!Hata Ay mzee wa biashara ametenda haki nusu afunike.... kwakweli walijipanga big up sana kwa zawadi hii.

USHAURI KWA CHID BENZ

Kuna mambo ambayo amekuwa akifanya Chid benz na huwa kera wengi hasa sisi mashabiki wake mfano ...Kupigana hovyo,Kupiga hovyo,Matumizi ya madawa na bangi
hayo inabidi aachane nayo maana yanamchango mkubwa kuharibu muziki na kipaji chake.

Hawa alio imba nao ndio wanaweza kuwa muongozo wake hasa Ay anaweza akamsaidia sana kama akiamua kuwa sambamba nae.
Nivyema akaangalia aina ya marafiki ambao amekuwa nao siku zote ambao wamempelekea kuzama kwenye madawa inabidi awapunguze na afanye muziki sasa.

Namtakia kila la kheri kwenye safari alio ianza upya.

TAFAKAFARI YA KATUNI:WAKUSOMA JIBEBE

DIAMOND KUFANYA KOLABO NA ALIKIBA ANYTIME....Wanafiki wamefyata mikia

HII NDO KOLABO YA DIAMOND NA ALIKIBA FOR REAL>>>Coming soon.

Ulichokuwa ukisubiri kwa muda mrefu huenda kikatokea hivi karibuni. Collabo ya Alikiba na Diamond Platnumz mabibi na mabwana inanukia.

Akizungumza na kipindi cha Jahazi cha Clouds FM leo (20/8), Alikiba amesema upo uwezekano wa kufanya kazi ya pamoja kama kukitokea mabadiliko.

“Mawazo ya kolabo yapo, mawazo unapata mengi tu, hiyo nimeshaisikia vilevile, na wewe sio mtu wa kwanza kuniuliza hicho kitu kipo.

 "Lakini muziki vile vile kama unavyoona kuna mavazi na style, vazi hili linatakiwa liende disko hili ni vazi la beach, vazi hili la ofisini, vazi hili la mpirani, hili la mchangani, hili la kwenye ukumbi unajua vitu kama hivyo! 

"Kwahiyo Diamond akipata vazi lake ambalo linahusiana na vazi ambalo natakiwa nivae, hakuna tatizo tunafanya kazi kama kawaida, kwa sababu yeye anafanya kazi vizuri,” alisema AliKiba.

Alipoulizwa kama kuna uwezekano wa kufanya show kubwa na Diamond alijibu kwa kicheko: “Wewe hujui kama watu wanasubiria (show) au unajisahaulisha.”
Udaku Specially

HABARI NA PICHA:NANI MZURI HAPO.......mie mgeni tu ndo nafika



PICHA YA LEO:UMEGUNDUA NINI HAPO KINAENDELEA.....

FLAVIANA MATATA:NA UTATA WA KUCHUMBIWA......soma pole pole...

Posted by GLOBAL on August 21, 2014
Stori:  ERICK EVARIST

MISS Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata amezua utata wa aina yake baada ya picha zinazomuonesha katika tukio la kuchumbiwa kunaswa na mwenyewe kudai si yeye aliyechumbiwa.
Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo limedaiwa kufanyika kwa siri hivi karibuni nyumbani kwa miss huyo, Shinyanga na kuhudhuriwa na baadhi ya ndugu wa karibu.
“Inaonesha hawakutaka watu wajue maana hata hakukuwa na watu…
Stori:  ERICK EVARIST
MISS Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata amezua utata wa aina yake baada ya picha zinazomuonesha katika tukio la kuchumbiwa kunaswa na mwenyewe kudai si yeye aliyechumbiwa.
Miss Universe Tanzania 2007, Flaviana Matata.
Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilo limedaiwa kufanyika kwa siri hivi karibuni nyumbani kwa miss huyo, Shinyanga na kuhudhuriwa na baadhi ya ndugu wa karibu.
“Inaonesha hawakutaka watu wajue maana hata hakukuwa na watu wengi siku hiyo, hata hao ndugu wenyewe hawakuwa wengi kiivyo lakini picha zinaonesha Flaviana akichumbiwa,” kilisema chanzo hicho.
Kikizidi kumwaga data chanzo hicho kilidai kwamba, mwanaume anayetaka kumuoa mrembo huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja ni Mchaga mwenye fedha zake aishiye Marekani.
“Nasikia huyo bwana wake ni Mchaga lakini anaishi Marekani, atakuwa ana fedha zake si mtu wa hivihivi,” kilisema chanzo.
Flaviana Matata akiwasalimia wazee kwa kupiga magoti.
Amani lilifanikiwa kuzinasa picha hizo ambazo zinamuonesha mrembo huyo akiwa amepiga magoti huku amemshika mkono mmoja wa wazazi wake aliyeshiriki katika hafla hiyo ya kupokea mahari.
Baada ya kupata madai hayo, paparazi wetu alimtafuta Flaviana kwa njia ya simu ya mkononi ndipo alipokataa katakata kuwa si yeye aliyekuwa akichumbiwa bali ni dada yake.
“Hamna kitu kama hicho,  unayesema alikuwa anachumbiwa si mimi ni dada yangu, mila za kwetu Shinyanga nalazimika mimi kumsindikiza hivyo kama umeona picha hizo uelewe hivyo,” alisema Flaviana.
Hata hivyo, baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa ni la Flaviana na si dada yake hivyo kuzidi kuzua utata juu ya ukweli halisi, Amani linaendelea kufatilia kwa karibu.

HUYU NDO MREMBO WA BONGO MOVIE ANAYEBADILI SANA NAMBA ZA SIMU

WOLPER NDO BINGWA WA KUBADILI NAMBA ZA SIMU

Posted by GLOBAL on August 21, 2014
Na Mwandishi Wetu

KUNA nini kwani? Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper anatajwa kuongoza wasanii wenzake kwa kubadili namba za simu za mkononi huku baadhi ya mashoga zake wakijiuliza kulikoni?
Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper.
Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu na Wolper (jina lipo), anamshangaa sana shoga yake huyo kwani amekuwa akibadili namba za simu kwa mwaka mmoja hata mara saba.
“Unajua kwa maisha ya sasa, simu ikipotea mtu unairinyuu laini yako ileile, maana ndiyo…
Na Mwandishi Wetu
KUNA nini kwani? Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper anatajwa kuongoza wasanii wenzake kwa kubadili namba za simu za mkononi huku baadhi ya mashoga zake wakijiuliza kulikoni?
Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper.
Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu na Wolper (jina lipo), anamshangaa sana shoga yake huyo kwani amekuwa akibadili namba za simu kwa mwaka mmoja hata mara saba.
“Unajua kwa maisha ya sasa, simu ikipotea mtu unairinyuu laini yako ileile, maana ndiyo inayojulikana na wadau. Lakini yule mwenzetu siyo. Nimeshamsevu kwenye simu yangu kwa majina ya Wolper, Wolper Tena, Wolper Nyingine, Wolper Nyingine Kabisa na Wolper Hakuna Tena, lakini zote kwa sasa hazipo hewani,” alisema shoga yake huyo huku akicheka.
Wolper alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi iliyozoeleka, hakupatikana. Jitihadi zilifanyika akaja kupatikana kwenye namba mpya ambapo alisema:
“Mimi nikishapoteza laini naona uvivu kwenda kuirinyuu, ndiyo maana nanunua nyingine.”