Saturday, 23 August 2014

TCRA:YATOA ONYO REDIO YA WATU...

Clouds FM Yapewa Onyo na Kupigwa Fine Kwa Kukiuka Kanuni za Utangazaji

Udaku Specially on Saturday, August 23, 2014
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imetoa onyo pamoja na kutoza faini ya takribani Sh milioni 5 kwa kituo cha redio na televisheni cha Clouds, kwa kukiuka kanuni za utangazaji za mwaka 2005. 

Wakielezea uamuzi huo jana jijini Dar es Salaam, Kamati ya Maudhui ya mamlaka hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Margaret Munyagi ilisema kuwa ukiukwaji wa kanuni hizo ulifanywa kwa nyakati tofauti na vituo hivyo.

Alisema kwa upande wa kituo cha redio cha Clouds, kupitia kipindi chake cha ‘Njia Panda’ kilichorushwa hewani Juni 15 mwaka huu kati ya saa 8.00 mchana na saa 10.00 jioni kilikuwa na mada iliyohusu safari ya kuzimu ambapo maudhui yake yalijaa simulizi za kufikirika, za kishirikina na kichawi.

Aidha alisema kosa lingine kituo hicho hakikufuata kanuni za Utangazaji(maudhui) za mwaka 2005 zinazowataka kuwasilisha ratiba ya vipindi vyao kwa TCRA ili viidhinishwe na vilevile kuvichapisha katika gazeti kabla ya kurushwa hewani ambapo kipindi cha Njia Panda hakikuwasilishwa kwa ajili ya kuidhinishwa.

Wakati huo huo, kituo cha televisheni cha Clouds kilirusha kipindi cha ‘Bibi Bomba’ Mei 16 na Juni 6 mwaka huu kati ya saa 3.00 na saa 4.00 usiku ambacho kilikiuka kanuni za Utangazaji (maudhui) za mwaka 2005.

Alisema kipindi hicho kilidhalilisha mabibi hao walioshiriki pamoja na wanawake kwa ujumla kutokana na maswali ya aibu waliyokuwa wakiulizwa na waamuzi wa shindano hilo ambayo ni kinyume na kanuni hizo.

Aidha alisema kituo hicho kinatozwa faini ya Sh milioni moja na kutakiwa kuwasilisha TCRA mwongozo wa kuchuja na kusimamia maudhui yasiyofaa kabla ya kutangazwa.

TCRA imesema kama Kanuni za Utangazaji zitaendelea kukiukwa hatua kali zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

habari na picha:OMMY D NA KIDOTI,VIPI WAMEPENDEZA?

USHAURI WA BUREEE

Mimi Binti wa Kitanga Niliyefundwa Mme Wangu Kwa Style Hizi Huwa Achepuki

Saturday, August 23, 2014
Admin Udaku Specially Kila siku nasikia vilio vya wanawake wakilia Waume zao wanachepuka kwa hilo naweza sema wanayataka wenyewe, natamani niwafunde siku moja kidogo mjue kuwa akili ya Mwanaume ni kama mtoto mdogo yaaani ni vitu vidogo sana unaweza ukawa unamfanyia mumeo na hata siku moja asifikirie kuchepuka , Mimi mme wangu akitoka kazini gia ya kwanza ni home na simlazimisha bali vijimambo vyangu vya uchokozi wa hapa na pale ndo vinamuwaisha, yaani namfanya mme wangu kama mtoto mdogo, kwa kupitia mavazi yangu na chakula nachompikia ni silaa moja wapo nayotumia ...Jamani Wanawake Wenzangu Amkeni ...Wacha Kulalamika
Consolata

Jux Afunguka:Kweli Jack Patrick Alikuwa ni Mpenzi Wangu

Jux Afunguka:Kweli Jack Patrick Alikuwa ni Mpenzi Wangu

Saturday, August 23, 2014
Na Musa Mateja
MALOVEE! Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu, staa wa Bongo Fleva anayetamba na wimbo wake wa Nitasubiri, Juma Khalid ‘Jux’, kwa mara ya kwanza amevunja ukimya na kufungukia penzi lake na modo anayedaiwa kufungwa nchini China kwa msala wa madawa ya kulevya ‘unga’, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’.

Jux ambaye anasoma nchini China huku akifanya muziki wa Bongo Fleva, alifunguka hayo juzikati katika ‘exclusive interview’ aliyoifanya na mwanahabari wetu alipokuwa mjini Kahama alipokwenda kwenye Serengeti Fiesta 2014.

Akijibu swali la mwandishi wetu lililomtaka afungukie penzi lake na Jack ambalo alikuwa akichengachenga kila alipotakiwa kutoa ufafanuzi na vyombo vya habari, Jux alianza kwa kukiri kwamba mrembo huyo alikuwa mpenzi wake na walidumu kwa takriban miezi saba kabla hajakutwa na msala wa madawa ya kulevya.

Alisema tangu aanze kuyajua mapenzi, Jack alikuwa ni mwanamke wa pekee kwake ingawa wakati anapatwa matatizo walikuwa wametibuana kwa kipindi cha wiki mbili.

“Nilisikitika sana niliposikia amekamatwa kwa madawa ya kulevya, nilikuwa sijui kama anafanya hiyo biashara na kinachoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa najua yupo Bongo na nikajua tutaonana maana mimi nilikuwa Bongo wakati huo,” alisema Jux.

Alipoulizwa kama ana taarifa za Jack kufungwa miaka sita jela kama ilivyoripotiwa wiki iliyopita, Jux alisema hana taarifa hizo.“Kiukweli sijazipata habari hizo labda nitakapoenda tena China ndiyo nitajua kupitia kwa mwanasheria wake maana kwa sasa hajanipa taarifa na hana namba yangu ya simu ya hapa,” alisema Jux.

Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka jana akiwa amebeba madawa ya kulevya aina ya Heroin yenye uzito wa kilo 1.1 katika Uwanja wa Ndege wa Macau akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China.

USOME WARAKA WA MBUNGE GODBLESS LEMA..endeleaaaaa

Godbless Lema Amshushia Waraka Mzito Jakaya 'Heri Kuitwa Mpumbavu Kwa Ajili ya Haki Na Kweli'

Saturday, August 23, 2014

Mh Rais , bila shaka utakuwa unaifahamu vizuri historia ya Farao

Mh Rais nakusalimu .


Ni usiku wa manane wakati naanza kuandika waraka huu , nimetoka kuangalia historia ya maisha ya Dr Martin Luther Jr na nilipotaka kulala nilishindwa na nilipotafakari jambo jema la kufanya wakati huu nilipokosa usingizi ndipo wajibu huu muhimu wa kuandika waraka huu kwako ulipoanza .


Mh Rais , bila shaka utakuwa unaifahamu historia ya Farao na Wana wa Israel wakati Mungu alipotaka kuwatoa wana wa Israel utumwani Misri , kwa wale Wakristo wanaosoma Biblia wanajua kuwa , maandiko yanasema “ Na Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ili apate kujitukuza mbele ya wana wa Israel . Mh Rais siwezi kuandika sana juu ya nini kilitokea kwa Farao na Watu wake ila nikuombe sana umuombe Mch G. Rwakatare hakueleze kwa ufasaha ili upate kujifunza jambo muhimu hapa .


Mh Rais , ukiona unafanya au unatenda hila au dhambi bila kipingamizi wala taabu , maana yake ni kuwa mauti kwako yamekaribia kwani mwizi aliyeambiwa kuwa siku zake ni arobaini kama angeacha uovu katika siku ya thelasini na nane pengine angeponywa na wito wa mauti…. Nchi hii haiko salama hata kidogo , hali ni tete sana na kwa bahati mbaya Watawala hamuoni kwani macho yenu yamepigwa upofu na shetani na ndipo andiko laGodbless Lema litatimia “ Na Mungu akaufanya Moyo wa Kikwete na ccm kuwa mgumu ili apate kuikomboa Tanzania “


Mh Rais sina mashaka na Uhuru wa kweli na wa pili wa Taifa ili katika siku chache zinazokuja ,, , hamtaweza kuzuia mabadiliko hata kama wanayoyataka sasa watakufa wote leo , ila kukosa hekima katika uongozi kunaweza kusabisha mabadiliko haya yakaja na hasara kubwa katika Jamii . Hata hivyo kiburi mlichonacho kinasababishwa na wajibu na mipango ya Mungu katika Nchi yetu .


Mh Rais , Watu wameendelea kuteseka kila kona , maisha ni magumu , mfumuko wa bei umepoteza thamani ya fedha , Wagonjwa mahosiptalini wanakufa kwani panadol imekuwa dawa ya kutibu maradhi yote, jela kumejaa masikini na wanyonge na Watu wanaokwepa kodi na kulibia Taifa wamekuwa marafiki wa watawala , ajira hakuna na vijana wamekata tamaa , dada zetu wamekuwa malaya wa kutafuta chakula cha siku na ada ya kuendelea na masomo .


Mh Rais , pamoja na rasilimali tele tulizonazo kama vile dhahabu , Tanzanite , Gesi , Almasi , Mbuga za Wanyama , Madini ya Urani , Mlima Kilimanjaro , Kahawa , Pamba , Korosho , Bandari , Mito na maziwa na vitu vingine vingi , bado vimeshindwa kutoa mwanga wa maendeleo katika Taifa hili .


Mh Rais , Tuko katika kipindi ambacho tunaandika Katiba ambayo wakati Wananchi wanatoa maoni walikuwa na matumaini makubwa . Mtafaruku uliopo sasa ni kati ya UKAWA na ccm , sio vita rahisi hata kidogo lakini Watu wajinga wanaweza kukushauri vibaya na ukafikiri unyenyekevu kwenye jambo hili ni kujidhalilisha , Wewe ni Rais , ukishindwa kutambua Mamlaka yako na nguvu zako katika kusimamia ukweli na haki basi Nchi itakuwa imepoteza dira . Mh Rais unapaswa kushuka na kuwa mnyenyekevu kwani dhamira njema yenye malengo mazuri haiwezi kumdhalilisha binadamu . Wasira . Lukuvi na Werema na wengine watakushauri nakukuambia ukilihairisha Bunge utawapa Kichwa UKAWA na Nchi itaenda Upinzani .


Mh Rais ukiitwa mpumbavu kwa ajili ya haki na kweli , upumbavu huo una maana kubwa kuliko kusifiwa na watu wanaopenda dhuluma na hila hata kama ni wengi , ninahisi changamoto unazopitia kama Rais na Mwenyekiti wa Chama , lakini Mtu Hodari na shujaa ni yule anayeshinda majaribu na taabu wakati usio muaafaka .Nakuomba ufanye maamuzi kwa ajili ya Watoto wa watoto wa Rizwan na Watanzania na sio Chama chako . Chama chako kitakuwepo leo na siku moja hakitakuwepo lakini Watoto na Wajukuu zako watakuwepo . Hivyo basi isaidie Tanzania kupata Katiba ambayo itampa binadamu yeyote haki , usawa na fursa katika Taifa lake.


Mh Rais , karibu kila mtu mwenye akili timamu amesema juu ya jambo hili hakuna atakaye kulazimisha lakini wakati ukifika wakati utakulazimisha , Polisi wetu na Jeshi halitaweza kushindana na kulishinda Jeshi linaloitwa WAKATI , hali itakuwa ni mbaya , Watoto wataitafuta Tanzania na kuikosa , ndipo watu wazima watasema tulikuwa wapi wakati misingi ikiharibika ? zitakuwa ni siku za taabu na uchungu na UKAWA hawatakuwepo tena ila WAKATI watakuwepo na hawatamsilikiza mtu yeyote , nyumba za kifahari na magari yanayokusanywa sasa kwa hila na wizi hayatakuwa makazi ya Watu isipokuwa popo na mende , Marekani , Uchina na Ulaya watawageuka watawaita wahalifu wa demokrasia na wauaji , watawatafuta ,watawakamata na Maisha yenu yatakuwa ya Uchungu mkubwa wakati Nchi haitakuwepo , mimi sio mtabiri kama marehemu Sheikh Yahaya , lakini najua kwamba ukiwa na mwanamke mjamzito ndani ya nyumba ni bora na ni muhimu ukaanza kuandaa vifaa muhimu vya mtoto kama nguo nk .


Mh Rais , sikutishi , ila Mungu hadhiakiwi apandacho mtu ndicho avunacho , najua watakuja wapambe hapa watakuambia umeona ujinga wa yule Mbunge wa Arusha ? watasema ameandika ujinga , watakebehi na kudharau kama kawaida yao . Hata mimi siandiki kutafuta sifa kwani mke wangu na watoto wangu wanatosha kunisifu na kila siku wanafanya hivyo asubuhi na jioni hasa pale ninapowaletea Ice Cream .


Mh Rais , nisikuchoshe sana , ila tafakari tena , natambua mara kwa mara huwa unakuja Arusha lakini sijawahi kuambiwa wala kutaarifiwa pengine ningekuambia haya mambo kwa mdomo na mara nyingi huwa nakutana na msafara wako barabarani na ndipo natambua kuwa huko Jimboni kwangu . Hata hivyo tunaendelea kupambana vizuri kujenga demokrasia ya kweli na Chama chako kinaendelea kudhoofika vizuri sana hapa Arusha na tunatarajia kumaliza uchaguzi Mkuu wa 2015 wa Jimbo letu hili mwaka huu mwezi wa kumi na mbili .



Mh Rais , naomba nitoke nje ya mada yangu muhimu kidogo , matukio ya Ugaidi na mauaji bado yanaendelea hapa Arusha , lakini sina taarifa za ndani sana kwani na siku nyingi kidogo sijatembelea matajiri wa Arusha ambao Rpc anawapa taarifa zaidi za matukio yanayotishia usalama wa Jimbo langu kuliko mimi Mbunge hata kama nikizihitaji kwa barua , ni jambo la kusikitisha lakini ni jaribu ambalo tumeweza kulisitahimili , nitajaribu kwenda kuwaona matajiri hawa siku chache zinazokuja ili nipate taarifa za hali ya usalama ya Jimbo langu na nitakuandikia waraka mwingine kukueleza ukweli , hata hivyo kuna watu waliokamatwa hivi sasa ila kwa vile sina taarifa za kutosha nina shindwa kujua vizuri kama watu ha ni wahalifu au la , isipokuwa ni na imani Mungu , Shetani na Polisi wa Arusha wanajua vizuri .

Mh Rais , nakushukuru na ninakuombea kwa Mwenyezi Mungu wakati unatafakari tena kuhusu mchakato wa Katiba , hata hivyo Watanzania wasiogope kwani “ Na Mungu akaufanya Moyo wa Kikwete na ccm kuwa mgumu ili apate kuikomboa Tanzania “


Godbless J Lema (MB)

KISIASA ZAIDI:HUU NDO MGOGORO WA UVCCM ARUSHA.

August 22, 2014

sakata la bifu ndani ya Uvccm Mkoa wa Arusha lachukua sura mpya

six1
 
Katibu mkuu wa umoja wa vijana,Sixtus Mapunda akiongea katika moja ya ziara yake Mkoani Arusha hivi karibuni  ikiwa ni ziara yake ya kwanza ya kikazi kufanya Mkoani hapa
 
SAKATA la Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Arusha sasa kupatiwa muarubaini wake ambapo imedaiwa kuundwa timu maalumu itakayochunguza mgogoro huo  
 
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu mkuu wa umoja wa vijana,Sixtus Mapunda ameeleza mtandao wa jamiiblog kuwa kutokana na kinachoendelea hivi sasa katika umoja wa vijana Mkoa wa Arusha kuwa tayari Makao makuu wameshatuma timu ya kuchunguza mgogoro huo
 
Alisema kuwa tayari timu hiyo imeshawasili jijini Arusha hivyo kuanza kazi rasmi kesho (leo)itakayopelekea kubaini ni nini hasa chanzo cha mgogoro huo ambao unaendelea katika umoja huo wa vijana
 
“Taarifa za kinachoendelea Arusha katika umoja wa vijana tayari ila tumeshatuma timu maalumu ya kuchunguza ni nini hasa kinasababisha vurugu hizo”Alisema Mapunda 
 
Aidha Mwenyekiti wa umoja huo Mkoa wa Arusha Robson Meitinyiku ameshangazwa na utaratibu uliotumika kuwaita katika kikao cha Sekretarieti unaotarajiwa kufanyika kesho ambapo alidai wajumbe walitumiwa mualiko kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno(sms)
 
Kuhusu kikao cha kesho (leo) kilichoitwisha na Sekretarieti ya mkoa chini ya Katibu wake Mary Chatanda, mwenyekiti Meitinyiku alisema utaratibu uliofanyika kuwajulisha wajumbe kuhusu kikao hicho ni wa ‘kihuni’ kwa kuwa walitumiwa taarifa kwa ujumbe wa simu badala ya kujulishwa kwa barua kama inavyotakiwa.
 
 “Nashangaa kwa kweli nimetumiwa ujumbe mfupi wa maneno na Gerald Mwadalu tuliyemsimamisha kuwa kesho kutakuwepo na mkutano wa sekretarieti ya Mkoa sijajua kikao hicho kitahusu nini hasa ila pamoja na hayo haizuii mimi kutohudhuria”alisema Meitinyiku
.
Aidha alisisitiza kikao walichokifanyacha baraza la vijana mkoa na  kuwatimua Katibu wa UVCCM Mkoa Gerald Mwadalu kilikuwa sahihi licha ya kudaiwa kuwa kilikuwa kikao feki kwa kuwa idadi ya wajumbe walikuwa wametimia
 
Mwadalu akizungumza jana alisema kuwa kila kitu kitajulikana kwenye kikao cha (leo) cha Sekretarieti ya Mkoa kwamba hawa wanapata wapi nguvu za kufanya maamuzi ambayo ni kinyume na taratibu za umoja wa vijana.
 
Kwa sasa aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo ni Katibu wa UVCCM Mkoa wa muda Daniel Kayongo kutoka Longido(Habari na Pamela Mollel wa jamiiblog)

 
Katibu mkuu wa umoja wa vijana,Sixtus Mapunda akiongea katika moja ya ziara yake Mkoani Arusha hivi karibuni  ikiwa ni ziara yake ya kwanza ya kikazi kufanya Mkoani hapa
 
SAKATA la Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Arusha sasa kupatiwa muarubaini wake ambapo imedaiwa kuundwa timu maalumu itakayochunguza mgogoro huo  
 
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu mkuu wa umoja wa vijana,Sixtus Mapunda ameeleza mtandao wa jamiiblog kuwa kutokana na kinachoendelea hivi sasa katika umoja wa vijana Mkoa wa Arusha kuwa tayari Makao makuu wameshatuma timu ya kuchunguza mgogoro huo
 
Alisema kuwa tayari timu hiyo imeshawasili jijini Arusha hivyo kuanza kazi rasmi kesho (leo)itakayopelekea kubaini ni nini hasa chanzo cha mgogoro huo ambao unaendelea katika umoja huo wa vijana
 
“Taarifa za kinachoendelea Arusha katika umoja wa vijana tayari ila tumeshatuma timu maalumu ya kuchunguza ni nini hasa kinasababisha vurugu hizo”Alisema Mapunda 
 
Aidha Mwenyekiti wa umoja huo Mkoa wa Arusha Robson Meitinyiku ameshangazwa na utaratibu uliotumika kuwaita katika kikao cha Sekretarieti unaotarajiwa kufanyika kesho ambapo alidai wajumbe walitumiwa mualiko kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno(sms)
 
Kuhusu kikao cha kesho (leo) kilichoitwisha na Sekretarieti ya mkoa chini ya Katibu wake Mary Chatanda, mwenyekiti Meitinyiku alisema utaratibu uliofanyika kuwajulisha wajumbe kuhusu kikao hicho ni wa ‘kihuni’ kwa kuwa walitumiwa taarifa kwa ujumbe wa simu badala ya kujulishwa kwa barua kama inavyotakiwa.
 
 “Nashangaa kwa kweli nimetumiwa ujumbe mfupi wa maneno na Gerald Mwadalu tuliyemsimamisha kuwa kesho kutakuwepo na mkutano wa sekretarieti ya Mkoa sijajua kikao hicho kitahusu nini hasa ila pamoja na hayo haizuii mimi kutohudhuria”alisema Meitinyiku
.
Aidha alisisitiza kikao walichokifanyacha baraza la vijana mkoa na  kuwatimua Katibu wa UVCCM Mkoa Gerald Mwadalu kilikuwa sahihi licha ya kudaiwa kuwa kilikuwa kikao feki kwa kuwa idadi ya wajumbe walikuwa wametimia
 
Mwadalu akizungumza jana alisema kuwa kila kitu kitajulikana kwenye kikao cha (leo) cha Sekretarieti ya Mkoa kwamba hawa wanapata wapi nguvu za kufanya maamuzi ambayo ni kinyume na taratibu za umoja wa vijana.
 
Kwa sasa aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo ni Katibu wa UVCCM Mkoa wa muda Daniel Kayongo kutoka Longido(Habari na Pamela Mollel wa jamiiblog)

Diamond:Sasa Naoa Rasmi,HARUSI UWANJA WA TAIFA

Diamond:Sasa Naoa Rasmi, Harusi Naweza Ifanyia Uwanja wa Taifa Kila Shabiki Ashuhudie

Udaku Specially on Saturday, August 23, 2014
Msanii huyo ghali zaidi nchini kwa sasa, ametamka hayo alipozungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam juzi Jumatano. Alisema kuna mambo mengi yaliyomchelewesha kufikia hatua hiyo, ikiwamo maandalizi kwani amepanga mashabiki wake wahudhurie harusi hiyo.

“Ndoa ni kitu cha heri na baraka, lakini kitu kinachofanya kidogo mambo yachelewe ni kwamba sisi au mimi ni mtu ninayefahamika, kwa hiyo hata ndoa yangu watu wengi wanatamani waihudhurie,” alisema Diamond.

Pia amesisitiza kwamba ndoa si jambo la masihara kwani ni tendo la kiimani na ndio maana amekuwa makini katika mipango yake.

“Nataka kila kitu kishuhudiwe na mashabiki, ninaweza hata kuifanyia Uwanja wa Taifa,” aliongeza.

“Unajua nilishindwa kufanya mambo haya haraka kwa sababu wengi nadhani wangeamini kwamba ninafanya hivyo ili kutafuta umaarufu zaidi, tunataka tufanye kiusahihi yasije tokea mambo kama ya Instagram tunataka tuje kuwa mfano wa kuigwa.”

Alipoulizwa tarehe ya ndoa hiyo Diamond alisema: “Nilishasema ni hivi karibuni, unajua siku zote vitu vya kheri waswahili wanasema lazima uvifiche, hata Mwenyezi Mungu naye anasema anampenda mtu aliye na siri, lazima vitu vingine uvifiche ili vipate kufanikiwa. Wakati mwingine kunakuwa na husda, hasidi kwa hiyo ukiviweka wazi sana vinaweza kutofanikiwa.”

Taarifa kwamba Diamond hataoa zilisambaa na kudaiwa kumchefua mchumba wake Wema Sepetu ambapo katika mahojiano mkali huyo wa wimbo ‘Mdogo Mdogo’ alisema: “Kwanza sikuwahi kusema siwezi kuoa, nilishtushwa na gazeti hilo, nilisikitika kwa kweli na iliniuma sana, lakini nikaona nikijibu nitaonekana kwamba sina adabu, kwa sababu siku zote anayeanza huwa haonekani lakini anayemaliza. Pia siwezi kubishana na vyombo vya habari, mwisho wa siku ni watu haohao nitawategemea wanifanyie kazi zangu,” alisema.

Hata hivyo Diamond alisema mchumba wake anaumizwa na vichwa vya habari ambavyo vimekuwa mwiba kwake.

“Hata hivyo magazeti yetu tumeshayazoea jinsi yanavyoandika, wakati mwingine inakuwa kama chachandu au kufurahisha baraza,” aliongeza.

Kuhusu taarifa kwamba ameachana na mchumba wake huyo, alisema: “Hatuna tatizo watu wengi wanasema tumeachana, lakini hatujaachana na hatuwezi kujibishana.

“Sijui nikujibu nini kwa sababu kila nitakachokujibu utaona namsifia kwa sababu yule ni mchumba wangu.
“Lakini ninachoweza kukwambia ni kuwa sisi ndio tunaoujua ukweli wa uhusiano wetu.

“Sidhani kama ni sahihi mapenzi yetu yakawa na wasemaji wengine zaidi yetu wenyewe. Sasa ni ajabu watu wanaposema yao.”

Friday, 22 August 2014

UCHAMBUZI WA LEO:IJUE CHUNYA NA UTAJIRI WAKE

SAUTI KUTOKA NYIKANI.... MULUGO, MWANASIASA MREFU KAMA UTAJIRI WA CHUNYA MBEYA

 
MBUNGE WA JIMBO LA SONGWE PHILLIPO MULUGO.


NA GORDON KALULUNGA
MWAKA 2011, Mwandishi Mubelwa Bandio, aliwahi kuandika kuwa, anatamani angekuwepo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ili ayaone yanayotendeka hivi sasa.
Alisema tamaa yake ni kuhusu uchumi wa dunia unakoelekea na namna mataifa yanavyochukua umiliki wa uendeshaji wa shughuli muhimu za kiuchumi kisha anaishia kujiuliza kama hii si sehemu ama aina mpya ya ujamaa?
“Kama Baba wa Taifa Mwl Nyerere angekuwepo, basi angeweza kurejea kusema mawili matatu ambayo alishawahi kusema miaka kadhaa iliyopita na ambayo yamekuwa katika hotuba zake na nukuhu zilizopo sehemu mbalimbali” anasema Mubelwa.
Anaendelea kwa kusema kuwa, anatamani angekuwepo akaona viongozi wetu wa sasa ambao hawawezi kusimamisha mapigano mpaka watishiwe na mataifa fulani, ama wawekewe vikwazo na fulani.
Katika andiko la makala yangu wiki iliyopita ukurasa huu, kuhusu baadhi ya wajumbe wa Bunge la katiba kutoka Chadema na kurejea Bungeni, lilileta maoni mengi na ninawashukuru wasomaji wote waliopiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi.
Kabla ya Bunge hilo kuisha, nitaleta takwimu ambazo wengi hawataki kuzisikia ili mradi wahalalishe walichokisikia/wanachokitaka kuhusu serikali tatu, na hapo nitakumbusha neno “ukweli mchungu” la Mhariri wa Mtanzania Jumapili, Ratifa Baranyikwa.
Kwa leo sauti hii inatokea katika nyika ya wilaya ya Chunya mkoani Mbya.
Aliyekuwa Naibu waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi, Philipo Mullugo, kabla hajaangukiwa na jumba bovu la uteuzi mpya, alikuwa akionekana mchapa kazi na jambo hilo halina ubishi, labda ubishi uwe kwenye siasa chafu zinazoendelea kuishi hapa nchini.
Mulugo ni Mbunge wa Jimbo la Songwe, wilayani Chunya mkoani Mbeya. Mwonekano wake ni kiongozi kijana, umbile lake ni mwembamba na mrefu wa kutosha.
Katika wilaya hiyo ya Chunya kuna majimbo mawili ambayo ni Jimbo la Lupa linaloongozwa na Mbunge, Victor Mwambalaswa na linaloongozwa na Mulugo, liitwalo Jimbo la Songwe.
Historia inaonesha kuwa wilaya hiyo ndiyo wilaya kubwa kuliko zote nchini Tanzania.
Wilaya hiyo ina kilomita za mraba zipatazo 29,219 tarafa 4, kata 30 vijiji 73 na idadi ndogo ya watu wapatao 290,478.
Chunya ilianzishwa kwenye miaka ya 1948 na wakati huo ikiwa kama makao makuu ya wilaya ya Mbeya.
Wilaya hiyo ni moja kati ya wilaya za zamani au za mwanzo na zenye historia kubwa na ya pekee nchini.
Upekee wake unaazia kuwa ni wilaya ambayo imesahaulika kimaendeleo licha ya kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo misitu ya mbao na dhahabu.
Enzi za ukoloni wakati nchi ikijulikana kwa jina la Tanganyika, waingereza walichagua wilaya ya Chunya kuwa makao makuu ya jeshi la polisi katika eneo la mgodi wa Saza(mine).
Sababu kubwa ya kuchagua eneo la mgodi wa Saza au Saza Mine kuwa makao makuu ya polisi katika koloni la Tanganyika ilikuwa ni kulinda maslahi ya dhahabu.
Sehemu nyingine za machimbo ya dhahabu katika wilaya hiyo zilikuwa zinasimamiwa na wakoloni, na maeneo hayo ni Chunya mjini, matundasi na Makongorosi.
Wilaya ya chunya imepata umaarufu wa kuwa eneo la kwanza hapa nchini kuleta wachimbaji madini katika maeneo ya Saza na Matundasi kutoka nchi za Northern Rhodesi kwa sasa Zambia na South Africa yaani Afrika kusini.
Enzi za ukoloni kabila wa wawemba kutoka Zambia na makaburu(Boers) kutoka Afrika kusini, ndiyo watu waliokuwa wakifanya kazi za migodini kwasababu walikuwa ndiyo wataalamu.
Utaalamu wao unaelezwa kuwa ulitokana na sababu kwamba nchi zao zilikuwa na migodi mingi ya shaba, dhahabu, Almasi na makaa ya mawe.
Hadi leo hii ukienda Matundasi, Chunya mjini na Saza utawakuta Wawemba wengi ambao zama hizo walitoka Zambia na kwa sasa wamebakia kuwa walowezi.
Marais wa zamani wa Afrika kusini Frederick deKlerk na Pietha Botha wote walizaliwa katika eneo la mgodi wa Saza wilayani Chunya kati ya miaka 1938 na kuendelea.
Viongozi hao mashuhuri baadaye walisoma shule katika sekondari ya Iyunga iliyopo Jijini Mbeya, ambayo zamani ilikuwa ikijulikana kwa jina la Mbeya European School(shule ya wazungu) kati ya miaka ya 50.
Rais wa Zamani wa Namibia Sam Nujoma na akina Thabo Mbeki, wamewahi kuishi Matundasi katika kambi ya wapigania uhuru iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Tumbu.
Wilaya hiyo ya Chunya, ndiyo wilaya ya kwanza kuwa na kiwanja cha ndege na huduma za benki Tanzania, lakini mpaka sasa ni wilaya ya inayoonekana change kati ya wilaya tisa za mkoa wa Mbeya na wananchi kukosa huduma za kijamii.
Hapa hakuna mchawi, bali mchawi wa wilaya hiyo ni serikali yenyewe ambayo inaelezwa kuwa viongozi wengi wa nchi hii ama kwa kuingia ubia na makampuni ya watu wengine, wanaendelea kuila Chunya.
Wananufaika na rasilimali za wilaya hiyo hasa upande wa madini aina ya dhahabu na mbao za asili.
“Kuliwa” kwa Chunya hakujaanza leo, bali ni miaka mingi tangu enzi za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sauti hii ya nyikani, ndiyo maana imeamua kufananisha urefu wa Mbunge Mullugo na utajiri wa mkoa wa Mbeya, ambapo serikali ikiamua, wilaya ya Chunya itakuwa na maendeleo marefu kama alivyo Mullugo.
Mwandishi anapatikana kwa simu 0754 440749

KATUNI YA LEO:CHAMA ukitoa HERUFI YA KWANZA Inabaki nini?

PICHA YA SIKU:WATU WALIVOJAA KUMUONA RAIS WAO KIKWETE

HABARI NA PICHA:KIKWETE NDANI YA JONGOO LA TAZARA MOROGORO

RAIS KIKWETE ASAFIRI KWA TRENI YA TAZARA KATIKA ZIARA YAKE YA MKOA WA MOROGORO‏

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipanda treni ya TAZARA kuelekea Kisaki Mkoani Morogoro akiwa katika ziara yake ya mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Joel Bendera, Mbunge wa Morogoro Kusini  Mhe Innocent Kalogeris na KAtibu wa Rais Bw. Prosper Mbena wakiongea ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki mkoani Morogoro.
Mama Salma Kikwete, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli, Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA Bw. Ronald Phiri (kulia) na viongozi wengine ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa  Morogoro 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa  Morogoro . Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA Bw. Ronald Phiri zawadi ya picha ya jengo la makao makuu ya TAZARA akiwa ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa  Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na viongozi wengine ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa  Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika kituo cha Kisaki baada ya kusafiri kwa treni katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakilakiwa na umati mkubwa wa watu baada ya kuwasili katika kituo cha Kisaki baada ya kusafiri kwa treni katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika mkoa wa Morogoro.
PICHA NA IKULU

JOKATE IS ALREADY TAKEN JAMAN.....HUYU NDO ANAEMMALIZA

Jokate Apost Instagram Ujumbe Wenye Utata Kuhusu Huyu Mwanaume.

Friday, August 22, 2014
Katika Kupita Pita kutafuta Umbea wa Leo Udaku Special Nimekutana na Picha alizopost Jokate Akiwa na Mwanaume Mmoja Kutoka Kenya Anayejulikana Kwa Jina Nick Mutuma , Jokate Mwogelo Ameandika Katika Hiyo Picha Kuwa "Huyu Ananimaliza nampeleka kwa Babu wangu wa Kingoni" . 

Jokate is Taken Jamani 





NAYE YUPO KUMBE:Q-CHILLAH ALAMBA MKATABA MNONO

Q-CHILLAH ALAMBA MKATABA MNONO


Mbongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ akipokea mkataba kutoka 'QS Mhonda J Company'.
 
'Legend' kwenye gemu la Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ akipozi.

LEGEND kwenye gemu la Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’ amelamba mkataba wa nguvu kutoka QS Mhonda J Company ambao ndiyo watakaokuwa wakimsimamia kazi zake zote za muziki kwa sasa.
Mmiliki wa kampuni hiyo, Joseph Mhonda amesema atahakikishia anamsaidia kwa gharama yoyote nguli huyo ili arudi pale alipokuwa na kwenda mbele zaidi ikiwa pamoja na kuzindua bendi itakayokuwa ikifanya kazi zake na wasanii wenzake watakaosimamiwa na kampuni hiyo.
Akizungumzia hatua hiyo kubwa katika maisha yake ya muziki, Chillah alisema:
“Kwa miaka mitano nimekuwa kimya  kwenye radio na anga ya muziki kwa jumla ikiwa ni sehemu ya kuyapitia maisha mengine nje ya muziki but  thanks to God sikutegemea kupata mkataba mkubwa wa kunirudisha tena kwa nguvu zote kwa Watanzania waliomisi muziki mzuri kutoka kwangu, soon ngoma zitaanza kudondoka,” alisema Chillah.

DJ FETTY.....AWA KINUNDA KWA KUDUNDA WATU.

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
 
 Stori: Musa Mateja

MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga.
 
Mtangazaji wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa…
 
Stori: Musa Mateja
MTANGAZAJI wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa starehe pande za Kahama, Shinyanga.
 
Mtangazaji wa Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa kumuona akizichapa na mrembo huyo ikidaiwa walizinguana, hata hivyo waliamuliwa kabla mambo hayajawa mabayaw.
Ziara ya Tamasha la Fiesta kesho itahamia Tanga ambapo wasanii kibao wataangusha burudani ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.

BONGO MUVI...MUVI BADO INAENDELEA

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
Na: Gladness Mallya na Imelda Mtema

JAMBO limezua jambo! Baada ya hivi karibuni wasanii wa Bongo Muvi (Movie) kufanya dua kwa ajili ya wenzao waliofariki dunia, baadhi ya ndugu wa marehemu wamecharuka na kudai kuwa waandaaji wa kisomo hicho walifanya kwa manufaa yao binafsi.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya ndugu wa marehemu wanalalamika kuwa dua hiyo iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity,…
Na: Gladness Mallya na Imelda Mtema
JAMBO limezua jambo! Baada ya hivi karibuni wasanii wa Bongo Muvi (Movie) kufanya dua kwa ajili ya wenzao waliofariki dunia, baadhi ya ndugu wa marehemu wamecharuka na kudai kuwa waandaaji wa kisomo hicho walifanya kwa manufaa yao binafsi.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baadhi ya ndugu wa marehemu wanalalamika kuwa dua hiyo iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na kufanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar, ilikuwa ni kwa ajili ya kujipatia fedha yeye ndiyo maana hakuona haja ya kuwashirikisha.
“Dua ilifanyika lakini baadhi ya ndugu wa marehemu hawakuambiwa na wanalalamikia sana kitendo hicho kwani si cha kiungwana, kimsingi mamilioni waliyopewa na mdhamini wa shughuli yametumika vibaya,” kilidai chanzo hicho bila kueleza fedha hizo zimepatikana wapi.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba akizungumza jambo.
Baada ya malalamiko hayo kutua mezani, mapaparazi wetu waliwatafuta ndugu wa marehemu ambao hawakuonekana kwenye dua hiyo ambapo walifunguka kwa nyakati tofauti:
MKE WA MZEE SMALL
Bi. Fatuma Said ambaye ni mke wa aliyekuwa mkongwe wa maigizo nchini, marehemu Said Ngamba ‘Mzee Small’ alisema kwamba hawakupewa taarifa wao kama familia jambo ambalo limemsikitisha sana.
Aliyekuwa mke wa muongozaji wa filamu Bongo(George Otieno Tyson) Beatrice Shayo.
“Imeniuma kwa kweli kwani sisi wajane tunatengwa sana, yaani wasanii wakishazika hakuna anayerudi nyuma tena, kitendo cha kutokututaarifu kuhusu dua kimeniumiza sana jamani tungepewa tu taarifa,” alisema Fatuma.
BEATRICE SHAYO ‘MKE WA TYSON’
Huyu ni mwanadada aliyekuwa mke wa marehemu, George Otieno ‘Tyson’ ambaye naye alikiri kwamba hakuwepo kwenye dua kwa sababu hakuwa na taarifa.
Aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, marehemu Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ enzi za uhai wake.
“Sikujisikia vizuri na imeniuma sana kwani sikujua inafanyika wapi na imeandaliwa na nani, ukweli walioandaa hawakufanya vizuri kwani walipaswa kutushirikisha sisi wahusika ili tuwe kitu kimoja, sasa nashangaa walifanyaje dua wakati ndugu na jamaa wa marehemu hawana taarifa?” alisema Beatrice.
MAMA SHARO
Mama wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ ambaye alisema kwamba hakuwa na taarifa yoyote kuhusu dua na ndiyo alisikia kutoka kwa mwandishi.
“Ndiyo nasikia kwako, ukweli nimeumia kutokupewa taarifa kwani ningejumuika na mimi kwa ajili ya kumuombea mwanangu, naona wamenitupa na kunisahau kabisa, wasanii msiwe mnanitenga hivyo jamani!” alisema Mama Sharo.
Aliyekuwa mkongwe wa maigizo nchini, marehemu Said Ngamba ‘Mzee Small’ enzi za uhai wake.
SETH BOSCO
Ni mdogo wa marehemu Steven Kanumba ambaye alitafutwa baada ya simu ya mama Kanumba kuita bila kupokelewa ambapo alisema wao kama familia hawakupewa taarifa ndiyo maana hawakuonekana kwenye dua hiyo jambo ambalo limewahuzunisha.
“Aliyeandaa dua hiyo hakufanya jambo la kiungwana, tumejisikia vibaya sana kwani suala kama hilo walitakiwa kuwafuata wahusika na kuwaalika tena ikiwezekana washirikiane kwa pamoja lakini walifanya kwa ajili ya kujipatia fedha tu hakuna chochote,” alisema Seth.
Marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake.
MSIKILIZE RAIS
Naye Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba alilaani vikali kitendo hicho na kusema waandaaji hawakufuata utaratibu.
“Walitakiwa kuwashirikisha wahusika na mazingira haya tata ndiyo maana maswali yanakuwa mengi vinywani mwa watu kwamba hakikuwa kitu chema na cha uungwana,” alisema.
NYERERE SASA!
Akizungumza muandaaji mkuu wa shughuli hiyo, Steve Nyerere alisema wahusika wote walipewa taarifa japokuwa aligawana majukumu na watu wengine kwani asingeweza kuwafikia wote.
“Sisi tuligawana majukumu na nilituma watu kwa wahusika sasa kama hawakuwa na taarifa siyo kosa langu ni la kwao hao niliowapa hilo jukumu, hatukufanya shughuli ile kwa masilahi binafsi zaidi ya kuwakumbuka ndugu zetu,” alisema Steve pasipo kufafanua zaidi.

OLD BUT GOLD:REAL MADRID YA ZAMAN VS MBWA MKALI KWAO KESHO HIYO

Posted by GLOBAL on August 22, 2014
Mratibu wa Ziara ya Wachezaji wa Zamani wa Timu ya Real Madrid,Ssebo (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mechi ya kirafiki kati ya Tanzania Eleven na Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kesho.Mpaka sasa ni wachezaji watatu tu ndio waliowasili nchini huku wengine kadhaa wakitegemewa kuwasili mchana wa leo.Wachezahi hao ambao wapo nchini hivi sasa ni Luis Figo (wa tatu kulia),Christian Karembeu (kulia) na Beki Fernando Sanz Duran (wa pili kushoto).wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TSN,Farough Baghoza na Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven, Jamhuri Kihwelo 'Julio'.…
Mratibu wa Ziara ya Wachezaji wa Zamani wa Timu ya Real Madrid,Ssebo (wa tatu kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mechi ya kirafiki kati ya Tanzania Eleven na Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kesho.Mpaka sasa ni wachezaji watatu tu ndio waliowasili nchini huku wengine kadhaa wakitegemewa kuwasili mchana wa leo.Wachezahi hao ambao wapo nchini hivi sasa ni Luis Figo (wa tatu kulia),Christian Karembeu (kulia) na Beki Fernando Sanz Duran (wa pili kushoto).wengine pichani ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya TSN,Farough Baghoza na Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven, Jamhuri Kihwelo 'Julio'.
Kocha wa Timu ya Tanzania Eleven,Jamhuri Kihwelo "Julio" (katikati) akizungumzia namna Timu yake ilivyojiandaa kuwakabili Wakali hao wa soka Duniani wakati wa Mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo kwenye Hoteli ya SouthernSun jijini Dar es Salaam.Kulia ni Luis Figo na kushoto ni Fernando Sanz Duran ambao ni wachezaji wa zamani wa timu ya Real Madrid ya nchini Hispania.
Mchezaji Kiongozi wa Timu ya Wachezaji wa Zamani wa Real Madrid,Luis Figo akizungumza na Waandishi wa habari juu ya ujio wao hapa nchini.Figo amewaahidi wa Tanzania kuwa yeye na Wenzake watatoa burudani kabambe katika Uwanja wa Taifa jijini Dar hapo kesho.
Mchezaji Fernando Sanz Duran (kati) nae akitoa maneno yake kuhusu mchezo huo.
Mwanasoka Christian Karembeu akizungumza.

HIVI NDO VITU WAPENDAVYO WANAWAKE...but mmmhhh?

Wanawake Hufurahishwa na Vitu Vidogo Vidogo Sana Hakuna Haja ya Gharama

Udaku Special Limebaini Kuwa Sasa hivi imekua ni kawaida mtu kutumia pesa nyingi labda kumpeleka mpenzi wake kwenye mahotel makubwa au kumnunulia vitu vya thamani ili kumuonyesha mapenzi, ila ukweli ni kwamba unaweza ukafanya hayo yote ukajiingiza kwenye gharama kubwa na matumizi usiyotarajia  bila mafaniko. Mwanamke haitaji vyote hivyo mwanamke anahitaji muda, tumia muda mwingi kuwa nae, muonyeshe unamjali, tatizo lake chukua liwe lako. Mpe kidogo ulicho nacho na kitoke moyoni, Usilazimishe mambo utamboa, fanya ajiamini ukiwa nae, kuwa na misimamo yako usiyumbe yumbe katika maamuzi, Usiogope kumwambia hisia zako kwake, kwani wanawake wanapenda mtu anayejiamini. Fanya hayo utaona matokeo yake..!! 

POLE KAMA ULIPATA KAZI UHAMIAJI.... ISOME KWA MAKINI

POLE KAMA ULIPATA KAZI UHAMIAJI....
Week Kama tatu zilizopita Udaku Special tuliweka Habari kuhusu Majina ya Waliofauli Usaili wa Nafasi ya Ukonstebo na Koplo Pale Uhamiaji ambayo ilisemekana yalikuwa yamechakachuliwa kwani wengi waliopata kazi hiyo walikuwa na undugu na wafanyakazi wa Idara hiyo, Baada ya Habari hiyo Serekali ilisimamisha mchakato huo kupisha uchunguzi , Leo taarifa zimepatikana kuwa ni ukweli majibu ya usaili huo yalichakachuliwa na kuwaacha waliofaulu na wahusika kuweka ndugu ama jamaa zao hivyo basi matokeo ya usaili huo yamefutwa rasmi Mpaka hapo Utakapofanyika Usaili Mwingine 

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil alisema hatua hiyo imechukuliwa baada ya kamati maalumu ya kuchunguza ajira hizo kubaini wazi kwamba waliopewa nafasi hizo hawakukidhi vigezo.

Abdulwakil alisema wizara imesikitishwa na udhaifu huo baada ya kubainika wazi kwamba malalamiko yaliyotolewa na wananchi na kusababisha wizara kuingilia kati na kufuta usaili wa kuitwa kwenye ajira kwa watu 200 ulikuwa sahihi.


Alisema baada ya kubainika kwamba kweli kulikuwa na upendeleo wa dhahiri kwani watahiniwa wenye sifa na waliopata alama za juu wakati wa usaili hawakuitwa na kukiukwa kwa vigezo vya wazi, ajira hizo zitatangazwa upya na kusimamiwa moja kwa moja na wizara na siyo idara hiyo kama ilivyokuwa awali.

LULU AHONGWA HELA ILI ANUNUE GARI wakati akina nani WANAHONGWA GARI...NANI MJANJA?

Lulu Michael Aonyesha Kadi ya Gari yake Mpya, Aseme yeye si Kama Wakina Nanii Wanaohongwa

Friday, August 22, 2014
Kwa Kuonyesha kuwa yeye ni Tofauti na Mastaa Wengine wa Kike Walioingia katika Mkumbo wa Kuhongwa Magari wakati kadi ya Gari lina jina la muhongaji ambayo upelekea kunyang'anywa Penzi likiisha Mrembo Lulu Michael Ameonyesha Kadi ya Gari Lake Jipya aina ya Rav 4 New Model ,
Lulu Amesema yeye si Mswahili ndo maana ameamua kuonyesha kadi ya gari yenye jina lake ili kutowapa nafasi watu kusema amehongwa , Ameongeza kuwa yeye si kama wakina nanii ambao waliohongwa na kunyang'anywa magari... Hongera sana Lulu Michael Kwa Gari Jipya.