Wednesday, 17 September 2014

Wanaume Wanaowatelekeza Watoto Wao Nchini Kenya Wanakiona Cha Moto Kupitia Facebook

Tahadhari kwa wanaume wanaowatelekeza watoto wao nchini Kenya.Baadhi tayari wameanza kupata tumbo joto.

Kikundi cha wanaume watatu nchini Kenya kimezindua ukurasa wa Facebook ambao lengo lake ni kuwajibisha wanaume wasiotekeleza majukumu yao ya kuwalea watoto wao.Mtandao huo unaitwa Deadbeat Kenya.

Mtandao huo tayari umepata mashabiki wengi sana huku baadhi ya wale walioaibishwa wekiwemo wanasiasa, wanamuziki na watu mashuhuri, Huu Ndio mtandao ulio Weka Wazi Kuwa Prezzo hatoi matunzo kwa Mtoto wake hivi karibuni

Kwa nini mwanamume mwenye uwezo amtyelekeze mtoto wake? Baadhi ya wanaume wanalalamika kuwa wanawake ni wajanja kwani wanashika mimba kwa njia za kijanja.

Na je Jackson Njeru mwanamume aliyeanzisha ukurasa huu wa Facebook hahofii maisha yake? Hilo ni moja ya maswali aliyoulizwa na mwandishi wa BBC Dayo Yusuf

KWELI::Petit Man Adhibitisha Kuwa Mdogo wa Diamond ni Mchumba Wake na Muda si Mrefu Watafunga Ndoa

Meneja wa msanii, Mirror na mfanyakazi wa kampuni ya Wema Sepetu, Endless Fame Films, Petit Man ambaye awali alidaiwa kuwa na uhusiano na Kajala, kisha kuwa na mdogo wake Vanessa Mdee, amethibitisha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na dada yake Diamond Platnumz, Esma na kwamba ana mipango ya kufunga naye ndoa.

“Ni kweli Esma ni mchumba wangu na Mungu akijalia soon tunafunga ndoa,” alisema Petit kwenye kipindi cha My Playlist cha Clouds TV. Alipoulizwa jinsi Diamond anavyouchukulia uhusiano wao, alisema: Unajua siwezi kumsea moyo wake lakini naona kawaida na hamna tatizo lolote.”

MABOMU YA SONGEA::ASKARI WATATU WAJERUHIWA KWA MLIPUKO WA BOMU SONGEA

Askari Polisi wakiwa eneo la tukio ikiwa ni kuimarisha ulinzi
Eneo la tukio  likiwa limezungushiwa alama na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwangu akizungumza jambo na waandishi wa habari katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma baada ya kuwatembelea majeruhi hao.
Kamati ya ulinzi na Usalama wakiwa Hospital ya mkoa wa Ruvuma.
Aliye lala kitandani ni WP ambaye amejeruhiwa akiwa amelazwa katika hospital ya Mkoa wa Ruvuma
Mganga mkuu wa Hospital ya Mkoa wa Ruvuma Dr Daniel Malekela akizungumza na wandishi wa habari hopitalini hapo.
Askari Ramadhani Ally akiwa anaelezea jinsi mkasa huo ulivowakuta wakiwa kazini
ASKARI watatu  wa jeshi la Polisi wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa  wa Ruvuma  (Homso) iliyopo mjini songea Mkoani humo  wakiwa wanapatiwa matibabu ya majeraha ambayo waliyapata baada ya kushambuliwa kwa kitu kinachodhaniwa kuwa ni Bomu la kurushwa kwa mkono.
Tukio hilo limetokea  September 16, 2014 majira ya saa moja na nusu jioni katika kata ya Msufini karibu na daraja laMatarawe, wilayani Songea Mkoani Ruvuma  ambapo watu watatu wasiofahamika walitupa kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu la kutupwa kwa mkono ambalo limetengenezwa kienyeji na kuwajeruhi askari  hao watatu waliokuwa doria.
Askari hao waliojeruhiwa ni  WP. 10399 PC Felista aliyejeruhiwa mguu wa kulia  kwenye unyayo na pajani  ,G. 7351 PC Ramadhani aliye jeruhiwa mguu wa kulia karibu na goti na tumboni upande wa kulia na  G. 5515 pc John aliyepata majeraha katika mguu wa kulia chini ya goti na jeraha dogo tumboni.
Mganga mkuu wa Hospital ya Mkoa wa Ruvuma Dr. Daniel Malekela ameeleza kutoa vipande vya bati na misumari katika majeraha ya askari hao na mpaka sasa wanaendelea na matibabu.
Alisema kufutia hali hiyo Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linaendelea na uchunguzi  wa kina ili kuwakamata wahusika wa tukio hilo kwa hatua zaidi za kisheria. Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe. Saidi Mwambungu kasema  amesikitishwa sana na kitendohicho cha wahalifu kujeruhi askari tena kwa makusudi na amesema serikali kupitiavyombo vyake vya ulinzi na usalama watahakikisha wanawasaka na kuwakamata.

WEMA AZIMA JEURI YA KAJALA


Stori: Erick Evarist
FEDHA haina mwenyewe! Siku chache baada ya kudaiwa kuyumba kiuchumi kiasi cha kuzidiwa jeuri na aliyekuwa shosti wake, Kajala Masanja ‘K’, Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ameibuka na kujibu mapigo kwa kumwaga ‘mafedha’ ukumbini, Risasi Mchanganyiko linashuka na mzigo kamili.
Wema akimwaga manoti kwa mwimbaji wa Skylite Band.
Tukio hilo lililowaacha watu midomo wazi lilichukua nafasi Ijumaa iliyopita katika Ukumbi wa Thai Village, Masaki jijini Dar kulipokuwa na sherehe maalum ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa vinywaji vikali vya Jack Daniel, Mr. Jack’s.
WEMA ALIUMIA MOYONI
Chanzo kilicho karibu na Wema, kilipenyeza habari kuwa, msanii huyo hakufurahishwa na kitendo cha watu kumuona kafulia kiasi cha kuzidiwa na K ambaye aliwahi kumlipia faini ya shilingi mil. 13 kumnusuru na kifungo cha miaka mitano jela.
KIFUNGO KILIKUWAJE?
Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe, Faraji Agustino kukumbwa na tuhuma za kutakatisha fedha haramu.
Wema akizidi kumwaga manoti kwa mwimbaji huyo.
TUJIUNGE NA CHANZO
“Wema hakufurahishwa na kitendo cha watu kumsemasema kila siku kwamba kafulia, hakupenda kuambiwa kazidiwa fedha na K wakati anaamini bado fedha anazo sema aliamua kukaa kimya kwani hakupenda majibizano ya kwenye vyombo vya habari,” kilisema chanzo hicho.
JEURI YAANZIA TEN LOUNGE
Awali, mwanahabari wetu alimshuhudia Wema akiwa na wapambe wake katika Ukumbi wa Ten Lounge (zamani Business Park) uliopo maeneo ya Victoria, Makumbusho jijini Dar ambapo alifika kushuhudia burudani za wasanii mbalimbali.
RAUNDI ZAZUNGUSHWA
Akiwa ukumbini hapo, wapambe wake walionekana kutumia vinywaji mbalimbali (vilivyo na visivyo na kilevi) huku mwenyewe naye akitumia mvinyo wake ambao kwa macho ya kawaida unaonekana si wa pesa za mawazo.
FULL KUREKODIWA
Kuonesha kwamba fedha ipo, kila tukio alilokuwa akilifanya Wema na wapambe wake ukumbini hapo, lilikuwa likirekodiwa na mtu maalum waliyekuja naye na kisha kuondoka pamoja.
Pesa aliyotunzwa mwimbaji huyo na wema.
THAI VILLAGE SASA
Baada ya kutumia vya kutosha Ten Lounge, msururu wa Wema ulihamia katika Ukumbi wa Thai Village ambako ndipo jeuri ya fedha ilipokwenda kukamilika.
Chanzo makini kilichokuwepo ukumbini humo kilimwaga data kwamba, Wema alifika akiwa na kundi la wapambe wake na kwenda kukaa mahali kwa muda huku raundi za vinywaji zikizungushwa kwa staili ya kata mti, panda mti.
AKUNWA NA MUZIKI WA SKYLIGHT
Wakati Miss huyo asiyechuja tangu alipotwaa taji hilo mwaka 2006 akiendelea kupata vinywaji vya hapa na pale, muziki mzuri wa Skylight Band ulimuinua na kujikuta yupo jukwaani chini ya himaya ya mwanamuziki mahiri anayefahamika kwa jina la Sam Mapenzi.
“Sam alimpagawisha kinoma Wema pale alipopiga wimbo wa All of Me ulioimbwa na John Legend, mtoto wa kike akapanda jukwaani na kukaa karibu yake, akawa anasikiliza mashairi hayo huku akimwaga manoti ya hatari katika kumtunza,” kilisema chanzo hicho.
ZAMZIDI KAJALA
Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, kwa hesabu za harakaharaka, Wema alimwagia Sam noti za elfu kumikumi zisizopungua mia moja (jumla milioni moja) hivyo kuzipiku zile za Kajala alizomwaga hivi karibuni wakati akiwatunza Yamoto Band katika Viwanja vya Leaders zilizodaiwa kufikia shilingi laki saba.
Mwigizaji wa filamu za Kibongo, Beautiful Onyinye, Wema Sepetu.
“Chezea Madam (Wema) wewe, kamwaga pesa kama hana akili nzuri, alitoa pochi ndogo iliyokuwa ndani ya pochi kubwa, balaa.“Zile alizotoa Kajala kwa Yamoto Band zilikuwa fedha za mboga, Madam kamwaga fedha ya maana leo,” kilisema chanzo hicho.
MPAMBANO UNAENDELEA?
Baadhi ya wadau wa burudani waliozungumza na mwandishi wetu, walidai Kajala hawezi kukubali kuzidiwa, hivyo lazima naye atasababisha tukio la maana hivi karibuni.
“Unafikiri Kajala atakubali? Subirini mtaona jeuri yake hivi karibuni,” alisema mdau huyo huku akiomba hifadhi ya jina.
TUJIKUMBUSHE
Makabrasha ya Risasi Mchanganyiko yanaonesha kwamba, Wema na Kajala walikuwa marafiki wa kushibana lakini baadaye walipishana kauli na sasa kila mmoja anaishi kimpango wake.

Tuesday, 16 September 2014

TATIZO LA WANAUME KUWAHI KUFIKA KILELENI (PRE MATURE EJACULATION)

WIKI iliyopita nilifungua somo muhimu sana kwa wanaume ambalo ni tatizo la wanaume kuwahi kufika kileleni au kuwahi kumaliza katika tendo la ndoa ikiambatana na uchovu wa ghafla wa kushindwa kurejea katika tendo na mbaya zaidi usingizi pia huwakumba ghafla wakiwaacha wenza wao bado na hisia kali za mapenzi.
Nilisema ninaliita hili kuwa ni janga la kitaifa kwa kuwa kliniki kwangu nimekuwa nikipokea wanaume wengi wenye tatizo hili lakini sababu ya pili ya kuliita janga la kitaifa ni kuwepo wanaume wengi wenye tatizo hili lakini hawajui kama ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine, lina vyanzo vyake na tiba kamili kwa hiyo wengi wao hubaki na tatizo hili likiwatafuna mpaka uzeeni.
Niliishia kwenye vyanzo na nilianza kwa kusema kwamba:
1. Kujichua (masturbation ) ni chanzo kikubwa cha tatizo hili kwa kuwa mara nyingi mtu mvulana anapoanza mchezo huu huwa anafanya kwa siri na huhitaji amalize mapema kabla hajakutwa na watu na tabia hii hujijenga kisaikolojia na kujikuta mvulana/mwanaume huyu huendelea na tatizo hili la kuwahi kumaliza hata katika tendo halisi.
Madhara haya ya kujichua huambatana na uume kusinyaa, kuwa mfupi na mwembamba tofauti na awali. Tafiti za kitabibu zinatabanaisha kwamba kila mwanaume aliyewahi kujichua mfululizo katika maisha yake ni lazima atakumbwa na tatizo hili kipindi fulani cha maisha yake.
2. Msongo wa mawazo. Wanaume wengi hasa wa mijini hujikuta katika msongo wa mawazo usiokwisha na hivyo hurudi nyumbani kutoka katika shughuli zao za kila siku.
3. Kukamia kupita kiasi.
4. Uoga/kutojiamini. Hali hii huwakumba wanaume wasio na taarifa kwamba wao ni wakamilifu, wanaume ambao hujidharau na kujiona hawafai kuwa na mwanamke wa hadhi fulani
5. Dr. Abrahams James wa Saint Magreth Clinic iliyopo Washington Dc katika andiko lake liitwalo `Sex and Fertility` la mwaka 2011,
amesisitiza kwamba wanaume kutofuatilia majarida /elimu au taarifa za mbinu mbalimbali za kumwezesha mwanaume kuchelewa kufika kileleni, huchangia kuendelea kwa tatizo hili kwa kizazi na kizazi na hasa kwa wanaume wa mijini ambao wengi wao miili yao haifanyishwi mazoezi kwa kazi zao au hata kwa kupanga muda.
Anasisitiza kwamba mwanaume anapopata ufahamu huu hupata hali ya kujiamini na hivyo kushiriki kikamilifu katika tendo la ndoa.
6. Ulaji mbovu ukiambatana na uzito kupita kiasi.Ulaji wa siku hizi hasa mijini ni mbovu kwa maana ya kwamba watu hujali rangi na ladha na si viini lishe vilivyomo na pia hawajali matokeo mabovu ya ulaji huo. Inashangaza kuona wasomi wengi na watu wenye uwezo kifedha wakiongoza kwa ulaji mbovu unaosababisha pamoja na mambo mengine, kukumbwa na tatizo la wanaume kuwahi kufikia mshindo na kutoweza kuendelea mpaka masaa mengi au hata siku zaidi ya moja zipite.
7. Kutofanya mazoezi na mwili kuwa legevu bila stamina ya kutosha. Inashangaza kuwaona watu wenye uzito mkubwa kupita kiasi au wazee au wagonjwa ndio wapo mazoezini asubuhi na jioni.
Hiki ni kiashiria kwamba watu hufanya mazoezi pindi wanaposhauriwa na daktari kwamba hiyo ndiyo suluhu ya wao kuendelea kuishi ilhali mazoezi yanapaswa kuwa sehemu ya maisha ili pamoja na faida zingine, yawasaidie wanaume kuchelewa kufika kileleni hasa wale ambao bado hawajakumbwa na tatizo hili.

Mwanamke ajirusha kwenye bwawa la Mamba

Bi Wanpen alijirusha katika bwawa hili la kuwatunza Mamba la Samut Prakarn
Mwanamke mwenye umri wa miaka 65 mjini Bangkok, Thailand, amefariki baada ya kujirusha katika bwawa lenye Mamba katika shamba la kutunza na kuhifadhi wanyama hao karibu na mji huo.
Walioshuhudia kitendo hicho wanasema kuwa walimuona mwanamke huyo, Wanpen Inyai, akijirusha katika bwawa lenye Mamba katika kituo cha kuwatunza wanyama hao cha Samut Prakarn, siku ya Ijumaa.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la The Bangkok Post. Wafanyakazi wa kituo hicho walikosa kumuokoa mama huyo.
Polisi wanasema kuwa walifahamishwa na familia ya mama huyo kwamba alionekana mwenye afya duni na mwenye kusongwa na mawazo kabla ya kifo chake.
 
Kituo hicho kina zaidi ya Mamba 100,000 katika mabwawa yake
Vituo vya watalii nchini humo vinasemekana kukosa mikakati ya usalama.
Polisi walithibitisha kifo cha Bi Wanpen Jumanne mchana.
Kwa mujibu wa ripoti, Bi Wanpen alivua viatu vyake kabla ya kujirusha ndani ya bwawa hilo, ambalo linasemekana kuwa na kina cha mita tatu.
Wafanyakazi walijaribu kutumia vijiti virefu kuwafukuza Mamba hao kwa lengo la kuwazuia wanyama hao kumshambulia mwanamke huyo.
Mapema siku hiyo, familia ya Wanpen, ilijaribu kutoa taarifa ya kupotea kwake la lengo la kumtafuta ingawa walifahamishwa kusubiri kwa saa 24.
Kifo chake kinafanana na kisa kimoja kilichomkumba mwanamke aliyejiua mwaka 2002 kwa njia hiyo hiyo katika kituo cha kuwatunza Mamba.

MICHEZO::''Nawaonea wivu Chelsea na Man U'' STEVEN GERRARD

steven Gerrard
Nahodha wa timu ya soka ya Liverpool ya England Steven Gerrard amesema amekuwa anazionea wivu timu za Chelsea na Manchester United zikishindana katika mashindano ya kombe la klabu bingwa barani ulaya.
Majogoo hao wa Anflid watashuka dimbani siku ya Jumanne kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009,kucheza na timu ya Ludogorets Razgrad ya nchini Bulgaria.
'Tumekuwa tukisia tamaa na kuhisi wivu kwa kiasi kikubwa kwamba hatutashiriki kinyang'anyiro hicho,'' alisema Gerrard ambaye alishinda taji la michuano hiyo mwaka 2005
Nimekuwa nikitamani sana kuwepo. Kila mtu anazubiri kwa hamu kusikia muziki,'' alisema Gerard.
Chelsea wameshinda kombe hilo huku Manchester United wakimaliza katika nafasi ya pili tangu Liverpool kushiriki michuano hiyo miaka tano iliyopita. ''

FAIDA YA KUTAFUTA NA HASARA YA KUPATA


Ni watu wachache ambao wanaweza kujisifu kwa uhodari wa kutafuta. Naamini ni nadra kumkuta mtu akifurahia kubeba mzigo mzito, kulima, kufanya kazi, kujituma katika shughuli hii na ile kwa sababu kutafuta tunakuchukulia kama kero.
Ni rahisi kutamani kufanya kazi kidogo lakini si kupewa fedha au mgawo wa mafanikio kwa kiwango kidogo. Tamaa ya wanadamu wengi ni kupata na si kutafuta.
Kwa msingi huo, sioni haja ya kusubiri jibu la kipi bora kati ya kupata na kutafuta kwa sababu najua; vijana wengi wanatamani sana kupata kazi nzuri, kuwa na fedha nyingi za kufanyia anasa, mavazi ya gharama na  nyumba za kisasa. Hivyo chaguo lao ni kupata.
Kitaalamu, miongoni mwa makosa makubwa yanayofanywa na watu ni kupenda kupata na kuchukia kutafuta. Msomaji wangu, utajiri si wingi wa pesa au mafanikio bali kufanya kazi na shughuli nyingi zaidi ya mafanikio uliyopata.
Siku zote wanaofanikiwa duniani ni wale wanaopenda kutafuta, hawachoki kuwekeza, hawaachi kujitumikisha, hawatafsiri faida kama pato la kutumia kwa anasa bali nyenzo ya kuwawezesha kutafuta zaidi.
Mchanganuo wa mambo haya mawili uko hivi: KUPATA; mfumo wake ni matumizi. Mtu aliyepata mshahara akafurahi, akaridhika, hana njia nyingine zaidi ya kuutumia mshahara huo kununulia nguo, kulipia umeme, pango la chumba na ada za shule.
Ukweli ni kwamba, hata kama fedha na mafanikio aliyopata mtu yatakuwa makubwa kiasi gani kwa mfumo huu wa kutoa, matokeo tarajiwa ya siku za usoni ni kumalizika kwa pato na hivyo kumpeleka mtu kwenye hatua nyingine ya kutafuta.
Lakini KUTAFUTA; ni mrija uvutao mafanikio. Anayetafuta hupata zaidi na zaidi na uzuri wake ni kwamba, mfumo huu umeunganishwa moja kwa moja na KUPATA. Kwa msingi huo anayetafuta anakuwa sawa na mtu anayeishi ndani ya mifumo miwili kwa mpigo na kwake mtu huyo hakuna kufilisika bali apataye hufilisika.
Nashauri, watu wote tufurahi zaidi wakati wa kutafuta, tujivunie uwezo wa kutenda, tupende kazi zinazotuingizia mishahara na kamwe tusipende mishahara inayotupeleka kwenye matumizi yatakayoturudisha kwenye mfumo wa kutafuta tusioupenda.
Muhimu kuunganisha nguvu katika harakati za kutafuta maisha na kuachana na mfumo wa kushirikiana zaidi kwenye matumizi ya vile tunavyopata kwa sababu mwisho wake ni mbaya.
Nimalizie makala haya kwa kuwashukuru wasomaji wangu wote kwa kuniunga mkono katika safu hii, siku zote nafurahi kusikia jinsi ambavyo makala zangu zimekuwa zikibadilisha maisha ya watu.

HABARI NDO HIYO::YANAYOWEZA KUMFANYA MPENZI WAKO AKATEMBEA NA RAFIKI YAKO!

Ni wiki nyingine tulivu kabisa tunakutana tena kupitia safu hii nikiamini umzima bukheri wa afya na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku kama kawaida.
Mimi namshukuru Muumba wa mbingu na ardhi kwa kuniwezesha kutimiza majukumu yangu ya kila siku likiwemo hili la kuelimishana na kukumbushana juu ya mambo yanayogusa maisha yetu ya kimapenzi.
Mpenzi msomaji wangu, wiki iliyopita nilikuwa na kazi kubwa ya kumshauri rafiki yangu ambaye aliniletea mashitaka ya mpenzi wake kutembea na rafiki yake.
Nilipata wakati mgumu sana kwani nilipoongea na msichana akaniambia wazi kwamba, amekuwa hapati penzi alilotarajia kutoka kwa rafiki yangu.
Msichana huyo akaenda mbele zaidi na kusema kwamba, yule shemeji yake alionesha kumjali sana kiasi kwamba siku alipomtamkia kwamba anampenda ilimuwia ngumu kukataa.
Kuna kitu cha kujifunza hapa kwamba endapo utaishi na mpenzi wako bila kumdhihirishia kwamba unampenda kwa dhati, akitokea mtu wa pembeni akaonyesha kuwa kafa kaoza, tarajia kusalitiwa kama siyo kuachwa kwenye mataa.
Unapokuwa umeanzisha uhusiano na mtu, utambue ana watu wengi wanaomtaka lakini huenda anawakatalia kwa kuwa yuko na wewe, sasa ukionesha kutomjali, hawezi kuendelea kuwa muaminifu kwako. Atachepuka na hata kama ataendelea kuwa na wewe ni kwa kuwa labda hana ujasiri wa kukuacha.
Ndiyo maana leo nikaona nikupe sababu ambazo zinaweza kumfanya mpenzi wako akatembea na rafiki yako tena wakati mwingine kwa siri bila wewe kujua.

Wewe mwenyewe
Endapo utakuwa umeanzisha uhusiano na mtu, wewe mwenyewe unaweza kutengeneza mazingira ya kusalitiwa. Usipoonesha kumpenda, kumjali, kuthamini penzi lake kisha rafiki yako akayaonesha hayo kwake, ni rahisi sana kukupiku.
Kwa mfano, endapo umekuwa na mpenzi wako lakini hata siku moja hujawahi kumpa zawadi au kumtoa ‘out’, siku shemeji yake (rafiki yako) akiamua kufanya hivyo, mpenzi wako atahisi yeye ni mtu sahihi kwake.

Kujirahisi kwake
Wapo ambao wanatembea na mashemeji zao kwa sababu tu ya kujirahisi kwao. Kwa mfano unapopendelea kuzungumza mambo ya chumbani na rafiki wa mpenzi wako unatarajia nini? Unapomvalia kihasara rafiki wa mpenzi wako lengo linakuwa ni lipi?
Mbaya zaidi ni pale utakapokuwa na mashemeji ambao hawabipiwi. Hapa namaanisha wale ambao wakiona dalili ya kupendwa tu, wanaomba chansi.
Kumuamini sana
Haishauriwi kumuamini sana rafiki yako kwani wengine wakipewa uhuru wa kuwa karibu na mashemeji zao, huchukulia kama fursa ya pekee.
Kwa mfano, unapomuamini rafiki yako kiasi cha kumruhusu aende na mpenzi wako baa, klabu au ufukweni ni kujitafutia matatizo.
Tunajua kwamba wapo marafiki waaminifu lakini tambua tu kwamba wengi wanapokuwa katika mazingira hayo ndipo huishia kusaliti na wakati mwingine bila kupenda.
 Kwa nini nasema bila kupenda? Chukulia umemruhusu mpenzi wako aende baa na rafiki yako, wamekunywa pombe hadi wamelewa kisha rafiki yako anamchukuwa mpenzi wako kwenye gari kumrudisha nyumbani.
Wengi kwenye mazingira hayo uzalendo unawashinda. Kwa hiyo kama hutaki yakukute ya kusalitiwa, kama una tabia ya kumruhusu mpenzi wako kwenda baa na shemeji yake, acha mara moja.
Rafiki mnafiki
Unaweza kuwa na rafiki lakini kumbe ni mnafiki. Huyu ni yule ambaye mko pamoja lakini anajiapiza kwamba siku moja lazima atakuchukulia mpenzi wako. Huyu ndiye tunamuita rafiki mnafiki.
Kutokana na tabia hizo ndiyo maana matukio ya baadhi ya wanaume kuwatongoza wapenzi wa marafiki zao yamekuwa yakiongezeka. Pia wanawake wengi sasa hivi hawaoni hatari kuwatongoza marafiki wa wapenzi wao au wapenzi wa mashoga zao.
Penzi la kweli
Mfano Juma ana mpenzi wake aitwaye Asha na Juma ana rafiki yake aitwaye Jamali. Juma na Asha ni wapenzi lakini hawapendani kivile ila Jamali anaonekana kuwa na penzi la kweli na Asha na wakati huohuo Asha naye anahisi kuwa na penzi la kweli na Jamali.
Katika mazingira hayo usije ukashangaa siku moja kusikia Asha katembea na Jamali. Siyo kutokana na tamaa au ushawishi bali ni kutokana na uwepo wa penzi la dhati kati yao.
Katika mazingira haya ndipo ambapo tumekuwa tukisikia fulani kamuacha mkewe kisha yule mke kaolewa na mwanaume ambaye alikuwa rafiki wa wanandoa hao.
Tamaa tu
Endapo utagundua mpenzi wako katembea na rafiki yako, kuna uwezekano ameshawishiwa kwa pesa au mali. Hii ni kwa sababu wapo watu ni dhaifu sana, yaani wao kusaliti wapenzi wao kwa sababu ya pesa, mali au tamaa zao za kimwili siyo kitu kigumu.
Ndiyo maana tunashauriwa kuwa na wapenzi ambao hawana tamaa za kijinga. Katika siku za mwanzo za uhusiano wenu ukigundua uliyenaye si mtu wa kuridhika na penzi unalompa, pesa na mali mlizonazo, mapema muonyeshe mlango wa kutokea kwani itakuwa siyo jambo la ajabu kusikia katembea hata na ndugu au rafiki yako.

BUREEE:::Mahari yapigwa marufuku Tororo Uganda


Mahari wilayani Tororo mashariki mwa Uganda yamepigwa marufuku na baraza la wilaya hiyo baada ya kubaini kuwa mahari Inamdhalilisha mwanamke.
Utafiti uliofanywa na asasi isiyokuwa ya kiserikali ya MIFUMI, umeonyesha kuwa mume akilipa mahari anamgeuza mwanamke kuwa mtumwa.
Mwandishi wetu Issaac Mumena alitembelea wilaya ya Tororo na kutuandalia ripoti hi

USHAURI WA NDOA::NDOA YENYE MZOZO KILA SIKU, MKE ANA KASORO!


NAFURAHI sana kukutana nanyi wapenzi wasomaji wangu wa safu hii inayozungumzia maisha ya mapenzi kwa ujumla.Wiki iliyopita tulikuwa na mada iliyokuwa na utambulisho usemao; Ni afadhali ukimfumania mumeo na demu mzuri kuliko anayepaka wanja wa ‘sina bwana?’Leo tuko na mada mpya; NYUMBA YENYE MZOZO KILA SIKU, MKE ANA KASORO.
Sina nia mbaya ya kuwashambulia wanawake, bali najaribu kukumbusha majukumu ya kila mmoja ndani ya uhusiano huku watu wakitakiwa kufahamu nini maana ya ndoa.
Mada hii italenga ukweli, umuhimu na ujuzi anaoweza kuupata mwanamke ili atengeneze ndoa yake na maisha yaendelee mbele.
NDOA  NI MPANGO WA NANI?
Kwanza ieleweke kwamba, Mungu alipotangaza ndoa kwa mwanamke na mwanaume hakuchagua kundi! Alimaanisha mwanamke yeyote na mwanaume yeyote wenye akili timamu. Kwa hiyo ndoa ni mpango wa Mungu na si utaratibu wa mwanadamu.
KUSHINDWANA
Kumekuwa na ndoa nyingi zinazovunjika madai yakiwa ‘kushindwana’. Utasikia mke au mume anasema niliachana na mwenzangu, kisa tulishindwana tu!
Kwa nini wanandoa washindwane? Ukiwauliza wengi kwa nini mlishindwana? Watajibu tulikuwa hatuelewani ndani ya nyumba.
Watu hao ni wale walioapa kuishi katika shida na raha hadi kifo! Wengi wamekuwa wakila hiki kiapo bila kujua maana yake! Wanaongea kwa kukariri.
Kuishi kwa shida (tabu) ni pamoja na kushindwana na kutoelewana, kuishi kwa raha ni wakati wa maelewano. Sasa wanandoa wakishafika nyumbani baada ya kufunga ndoa hupenda kuishi kwa raha tu.
MKE NA ITIFAKI YA UONGOZI
Mimi naamini, mke na mume kila mmoja ndani ya ndoa anajua nafasi yake ilipo. Mume anajua yeye ni kiongozi mkuu (kichwa) na mke anajua yeye ni msaidizi, sasa kushindwana kunatokea wapi hadi ndoa ivunjike?Katika safu ya uongozi wa kiserikali kuna itifaki, rais wa nchi naye ana msaidizi wake, kwa Tanzania tunasema makamu wa rais. Haiwezekani hawa wawili wakagombana kwa sababu kila mmoja ana mipaka yake ya kazi na anaijua.
Haiwezekani rais yuko nje ya nchi, makamu akaamua kuteua mawaziri na kuwabadilisha wakuu wa mikoa kwa kadiri apendavyo yeye, hiyo ni kazi ya rais.
Lakini ndoa nyingi za leo, kati ya 100, 85 zimevunjika kwa sababu ya migogoro ya kutojua itifaki hii. Wanawake wengi wamekuwa wakitaka kuwa na nafasi ya urais ili na wao waweze kuchagua wakuu wa mikoa na kubadili mawaziri kwa vile watakavyoona inafaa.
Mizozo mingi ndani ya ndoa za leo ni mwanamke kulilia usawa wa kufikia levo ya mume kama kichwa! Hivyo kujikuta ndani ya nyumba kunakuwa na marais (viongozi) wawili lakini usukani mmoja! Mh!
USAWA MGUMU
Ziko ndoa, mume anaposema sitaki hiki, mke anasema mimi nataka. Tena wapo wanawake kwa kutojua au kujua na kupuuza wametunga hadi msemo wenye kuwaaibisha wao wenyewe wakisema ‘kama mume ni kichwa cha nyumba, mke ni shingo’
maana yao ni kwamba kichwa hakiwezi kugeuka bila shingo.
Wamesahau kuwa, ili iitwe shingo lazima kuwe na kichwa ndiyo maana kichwa kikitoka, mwili unaitwa kiwiliwili lakini kichwa kikiwa pembeni ya kiwiliwili kinaendelea kuitwa kichwa.
MANENO YENYE HEKIMA KWA MWANAMKE
Yupo dada yangu wa hiyari anaitwa Mary aliwahi kuniambia maneno ambayo sikuamini kama yalitoka kichwani mwake au alimsikia mtu, alisema:
“Mimi mpaka mwanaume wangu anipige nitakuwa nimejibizana naye nini? Kama akinijia juu kwa maneno makali nitatulia, baadaye akiwa amepunguza hasira nitakaa naye kwa upole na kuongea naye vizuri, ataelewa tu. Sasa utakuta mwanamke mwingine, mume anasema yeye anasema, tena yeye kwa sauti ya juu, basi ndani ya nyumba ni kelele tu.
“Ukiona hivyo, mke ni tatizo! Kujibizana na mume ndani ya nyumba ni kukosa heshima kwani mume ni kiongozi, huwezi kujibizana na kiongozi wako ndiyo maana Mungu alisema mke mwema hutoka kwake lakini hajasema popote kuhusu mume mwema anakotokea.”

UTAJIRI NI UJASIRI ILA UMASKINI NI MAJARIBU>>AUMUA MWANAE ATAJIRIKE

Stori: mwandishi wetu, songea
MY God! Hali huenda ikigeuka, wakati jamii inaamini akina baba ndiyo wenye tabia ya kutokuwa na uchungu kwa watoto, imekuwa tofauti kwa mama huyu!Ni mkazi mmoja wa Kijiji cha Mwanamonga, Kata ya Lilambo, Manispaa ya Songea, Kasiana Komba (60) anadaiwa kuuawa na mumewe, Allan Menas Lwambano (76) kisa kikidaiwa mambo ya kumtoa kafara mtoto.
Bwana Allan Menas Lwambano anayedaiwa kumuua mkewe.
Tukio hilo la kuhuzunisha lilijiri usiku wa Agosti 25, mwaka huu ambapo maelezo ya mume huyo yanasema ni baada ya marehemu kumtaka akubali kumuua mtoto wao mmoja (jina tunalo) kati ya saba ili walipe madeni kwa imani ya kishirikina na kufanikiwa katika kipato (utajiri).
RPC wa mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msekela.
ILIVYOKUWA
Ilielezwa kuwa, mwanaume huyo alikataa ombi hilo na mkewe akamwekea mgomo wa kumnyima unyumba hadi pale atakapokubali ombi lake hilo.
MAISHA YA NDOA
Ilidaiwa kuwa, maisha ya wawili hao yakawa ya ‘sitaki nataka’, mume akitaka unyumba mke hataki kwa vile amemkatalia kumtoa mtoto wao kafara wakati yeye mke alishawaambia wenzake (kwenye ushirikina) kuwa, ameamua kumtoa mtoto huyo lakini baba yake hakutaka kufanya hivyo.
SIKU YA TUKIO
“Siku ya tukio usiku, Lwambano alirudi nyumbani na kumkuta mkewe amelala, alianza kumshikashika mwilini kuashiria alimhitaji faragha, ndipo mke huyo alipotoka nje na kuchukuwa mchi wa kutwangia mahindi kwa lengo la kumpiga mumewe.
Kasiana Komba aliyedaiwa kumtoa kafara mtoto wake ili apate utajili.
“Mumewe aliuzuia, akamnyang’anya na kumpiga mkewe kichwani, alianguka palepale na kufariki dunia,” kilisema chanzo.
MUME AHANGAIKA KUUZIKA MWILI
Habari za ndani zinasema kuwa, mume alipobaini ameua aliuchukuwa mwili wa mkewe na kuupeleka nyuma ya nyumba ambako kuna choo na kuuzika huku akipanda migomba juu ili kuzubaisha watu.
WATOTO: “BABA, MAMA YUKO WAPI?”
Agosti 26, mwaka huu, siku moja tu baada ya tukio hilo la kutisha, watoto ambao wanaishi mbali na nyumba hiyo walifika na walipoona hawamuoni mama yao, walimwuliza baba yao: “Baba, mama yuko wapi?”  akawajibu: “Mama yenu ameenda mjini Songea, atarudi.”
WATOTO WAENDA KWA MGANGA
Ikazidi kudaiwa kuwa, Agosti 27, mwaka huu, watoto hao hawakukubaliana na majibu ya baba yao, wakaenda kwa mganga wa kienyeji (jina halikupatikana mara moja) kwa lengo la kupiga ramli ili kujua alipo mama yao.
Waombolezaji wakiwa msibani.
“Mganga baada ya kuangalia ‘king’amuzi’ chake aliwaambia kama wanataka kujua mama yao alipo, warudi wakamchukue baba yao na kumfikisha kwa mganga huyo kwani yeye (baba) ndiye ana siri nzito.
“Watoto hao wakiongozwa na kaka yao mkubwa (Mathias) walimpa baba yao maagizo ya mganga. Ndipo baba huyo naye akawaambia kama wanataka kujua ukweli wa mama yao alipo, waongozane hadi kwa mtendaji wa kijiji akasimulie mbele yake.
MBELE YA MTENDAJI
Septemba 4, mwaka huu, familia hiyo ikiongozwa na baba mtu walifika kwa Mtendaji wa Kijiji cha Mwanamonga, Said Mango na Mwenyekiti wa Kijiji, Maria Kahimba ambapo katika maelezo yake , mzee huyo alikiri kumuua mkewe kwa kumpiga na mchi kichwani.
NUKUU YA MUME
Mzee huyo ananukuliwa hivi: “Nimemuua mke wangu nikamfukia nyuma ya nyumba yangu kwenye choo (watu wakapigwa butwaa).
Polisi wakiwa eneo la tukio.
“Sababu kubwa ya chanzo cha tukio ni mke wangu nilimkatalia ombi lake la kutaka tumuue mtoto wetu mmoja ili alipe madeni ya uchawi na kufanikiwa kimapato.
“Nilimkatalia, akawa ananinyima unyumba. Siku ya tukio nilimlazimisha kunipa unyumba, akakataa akataka kunipiga na mchi, nikamuwahi yeye na kumpiga, akakata roho.”
NANI ANAYEJUA?
Mwanamke mmoja aliyekataa kutaja jina lake, aliliambia Uwazi kwamba, marehemu aliwahi kumlalamikia kuhusu mumewe kugoma kumtoa mtoto wao mmoja kafara ili waweze kupata  mali. Alisema mumewe haoneshi kutaka mabadiliko.
“Alisema namwambia mume wangu tumtoe mtoto mmoja kafara tupate utajiri lakini alisema sitaki kusikia habari hizo, kwani yeye ameridhika na ufukara,” alisema mwanamke huyo akimkariri marehemu.
POLISI WAFUKUA MWILI, WAKUTA UMEHARIBIKA
Baada ya maelezo ya mzee huyo, vilio vilitawala, hakuna aliyeamini kisha familia kwa kushirikiana na wananchi na jeshi la polisi,
walifika nyumbani kwa mzee huyo akaonyesha sehemu aliyomfukia mkewe, polisi wakaamuru mwili huo ufukuliwe ukakutwa umeharibika vibaya, hasa sehemu ambazo mchi ulipiga.
Baada ya polisi na madaktari kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu, waliwaruhusu wanandugu wauzike.
MTUHUMIWA YUKO POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, ACP Mihayo Msikela (pichani), amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya taratibu za kisheria.

UTALII WA LEO::WELCOME IN TANZANIA.

SIJUI::NYWELE ZA WANAUME(za kichwani) HUOTA HARAKA KULIKO ZA WANAWAKE.

Wanawake tunauwezo wa kufuga nywele zetu zikawa ndefu kweli kweli kwa wale waliojaaliwa nywele zinazokuwa upesi.Lakini ukweli ni kwamba nywele za wanaume zinakuwa upesi kuliko za wanawake.Ndio maana kila wiki lazima waudhurie saloon.Nywele ni body tissue inayokuwa upesi kuliko yoyote katika mwili wa binaadamu.

KUTOKA BUNGENI:SERIKALI YASEMA BUNGE MAALUM LA KATIBA LINA UHALALI KISHERIA NA KISIASA KUENDELEA

 Na Magreth Kinabo,Dodoma
 
Serikali imesema kwamba Bunge Maalum la Katiba linaendelea kwa mujibu wa Sheria, mjadala wa hoja ya kusitishwa kwa Bunge hilo, umefungwa rasmi leo.

Aidha Serikali imewaondoa hofu wananchi kwamba hakuna mgogoro wa kisiasa, hivyo waendelee na shughuli zao za kujipatia kipato(riziki) kama kawaida, pia ipo macho kupitia vyombo vyake vya usalama,itasimamia sheria na taratibu zilizowekwa ili kuhakikisha taifa linaendelea kuwa na amani na utulivu.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha  Rose  Migiro kwenye kikao cha Arobaini cha Bunge hilo wakati akitoa tamko la Serikali  kwenye mjadala wa mwisho wa kujadili sura zote 15 zilizobakia za Rasimu ya Katiba Mpya.

“Bunge hili linaweza kuendelea na shughuli zake. Nawaomba Watanzania wafahamu mjadala wa kusitisha Bunge umehitimishwa hii leo kisheria na Mahakama Kuu ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Dk. Migiro.

Dk. Migiro aliongeza kuwa  kwa taarifa walizonazo majadiliano baina na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania(TCD) pamoja na vyama vyote husika yataendelea Septemba 17 na 18, mwaka huu, kwa sababu mchakato huo si wa chama kimoja, wala viwili au vitatu , bali  mchakato wa Watanzania wote kupitia mfumo ambao umewekwa  wa vyama vyote kisheria.

Akizungumzia kuhusu takwimu za wajumbe wa Bunge hilo, Dkt. Migiro alisema  kuwa lina wajumbe 630, kati yao waliotoka nje ya Bunge hilo ni wajumbe 130 ni sawa na asilimia 21 ya wajumbe wote.

“Wajumbe waliobakia ndani ya Bunge hili ni 500, sawa na asilimia 79 ya wajumbe wote, tukitazama mambo ya takwimu kwa  kutambua Kundi la 201. Imejitokeza dhana kwamba wajumbe waliobakia humu ndani ni wa aina moja, hiyo si kweli,”alisema.

Dk. Migiro alisema  kati ya wajumbe 500, waliobaki katika Bunge hilo, 189, wanatoka katika kundi la 201.

Alisema wajumbe  wengine waliobakia, 348 wanatoka upande wa Tanzania Bara, kati ya hao, wajumbe 125 ni wajumbe wanaotoka Kundi la 201.

“ Tukiangalia upande wa Zanzibar wajumbe waliobakia ni 152, kati yao wajumbe 64 wanatoka Kundi la 201.Tungependa kusisitiza Kundi la 201 ndio wajumbe ambao kwa wingi wao kitakwimu na kimakundi wanawakilisha Taifa  letu  kwa sura zote.

“ Ni dhahiri waliobakia humu ndani ni wengi, hii ina maana kwamba kwa kuzingatia matakwa ya masuala ya kisheria kwa maridhiano, kwa majadialiano na kwa kushawishi hoja.

“Wajumbe waliobakia  ni wengi wana uhalali kisheria na kisiasa. Tutaendelea na shughuli zetu kama sheria inavyotutaka, uwakilishi wa Bunge umetimia …  tuna wajibu  wa kisheria wa kufanya  yale tunayoyataka kuyafanya,” alisisitiza  huku akisema waliotoka nje  kwa pande zote mbili hawafikii theluthi moja.

Alifafanua kuwa vyama vilivyotoka nje ya Bunge hilo, ni vitatu,vilivyobakia  ndani ya ni 18 ambavyo vimesimamia na vinaendelea kusimamia umoja wa kitaifa  wa nchi yetu.

Akichangia mara baada ya tamko hilo, mjumbe wa Bunge hilo, John Shibuda alimpongeza mtoa taarifa hiyo ya Serikali na kuipongeza Serikali kwa kushinda kesi.
Aliwataka Watanzania kuchuja kati ya siasa na maslahi binafsi.

HASARA KWA NANI::WAFANYABIASHARA MUSOMA WAGOMA

Hayo ni baadhi ya maduka ya wafanyabiashara wa Musoma yaliyofungwa.
Maduka ya dawa yakiwa yamefungwa pia.
Wafanyabishara Musoma wamegoma kuendelea na biashara wakishinikiza T.R.A kurekebisha mashine  za kodi.

UNAMTAKA YUPI HAPO::MABINTI WA PRESIDENT OBAMA


Malia na Sasha wamekuwa hao wakati baba yao anaingia madarakani walikuwa madogo.Kingine naona ni vile warefu maana baba na mama warefu watoto watazidi Malia naona kashampita mama yake tayari kwa urefu.

TAFAKURI YA KIPANYA


AJABU NA KWELI::KIJANA AJITOKEZA KWENYEZA KWENYE MAZISHI YAKE

Stori: Makongoro Oging’
DA! Duniani kuna mambo jamani! Katika hali isiyo ya kawaida, maeneo ya Tandale Kwatumbo jijini Dar, waombolezaji hawakuamini macho yao wakati walipomuona ‘marehemu’ Mohamed Salum ‘Fido’ (29) (pichani), akirejea nyumbani hapo huku maandalizi ya mazishi yake yakipamba moto na waombolezaji, hasa mkewe, mtoto na ndugu wakilia kwa uchungu kufuatia ‘kifo’ chake.

Kijana Mohamed Salum ‘Fido’ anayesadikiwa kuwa alikufa.
Tukio hilo la aina yake lilitokea Septemba 12, mwaka huu, saa sita mchana wakati shughuli mbalimbali za mazishi yake zikiendelea zikiwa ni pamoja na maandalizi ya chakula cha mchana kwa waombolezaji.
Iko hivi; Fido ni dereva wa bodaboda, kijiwe chake kikiwa Lumumba Mnazi Mmoja, Dar. Inadaiwa kwamba Septemba 10, mwaka huu alikamatwa na polisi wa ‘Tigo’, Lumumba kwa madai ya kutokuwa na kibali cha kuingia mjini, akapelekwa Kituo Kikuu cha Polisi (Central).
Pale kituoni, habari zinadai maafande hawakumruhusu kumpigia simu mkewe ili kumweleza yaliyompata, ndipo ndugu walipoamua kumtafuta kwa siku mbili bila mafanikio.
Waombolezaji wakiwa msibani.
Septemba 11, mwaka huu, mkewe, kaka yake na baba yake mzazi walikwenda Hospitali ya Mwananyamala na kuingizwa chumba cha kuhifadhia maiti (mochwari) ambapo walioneshwa maiti moja! Vilio vikaibuka kwani wote walisema ni Fido. Marehemu huyo aliuawa kwa kugogwa na kitu kizito kichwani na maiti yake ilipelekwa hapo na polisi.
Ndugu hao walitoka na vilio hadi nyumbani na msiba ukawekwa kwa kukusanya mikeka na chakula kuanza kupikwa huku sehemu ya kuzikia makaburini ikitafutwa achilia mbali sanda kupatikana huku ndugu walio mbali wakijulishwa kuhusu msiba huo.
Siku ya tukio, watu wakiwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kuufuata mwili, ndipo Fido alipoibuka na kusababisha tafrani kubwa.Baadhi ya watu waliingia mitini kwa woga huku ndugu wakishangaa iweje maiti itoke mochwari yenyewe? Ndipo Fido alipotangaza kwa sauti kuwa, hakufa, alikuwa polisi.
Ndugu jamaa na marafiki wakiwa msibani.
Akizungumza na Uwazi huku akifakamia msosi kwa madai kuwa hakula tangu alipokamatwa, Fido alisema alikamatwa na polisi lakini akakosa njia ya kuwasiliana na familia yake.
Naye mke wa marehemu alipopewa nafasi ya kusema alikuwa na haya:
“Nimepigwa butwaa, siamini kama ndiye huyu mume wangu, watu wamekusanyika kwa ajili ya maombolezo, nilijua hatukonaye tena. Ama kweli Mungu mkubwa, nimefurahi kufika kwake nyumbani.
“Ilikuwa Jumatano saa 1.45 asubuhi mume wangu aliniaga na kwenda kazini kwake lakini hadi saa mbili usiku alikuwa hajarudi na si kawaida yake, ilikuwa nikipiga simu yake inaita tu.
“Ilibidi niende Tandale wanakohifadhia pikipiki, nilikuta wenzake wamesharudisha pikipiki lakini yeye alikuwa bado.“Tulifuatana na ndugu zangu hadi Lumumba hatukumuona, tulienda Kituo cha Polisi Msimbazi, Central, Oysterbay na Kawe lakini walituambia hakuna mtu mwenye jina hilo aliyekamatwa ama kupatwa na tatizo, ilibidi twende Hospitali ya Mwananyamala mochwari kuulizia kama kuna maiti iliyookotwa.
Chakula kikipikwa msibani.
“Uongozi wa mochwari ulitueleza kuna maiti tatu zilizopelekwa na polisi lakini hazifahamiki, moja ni kwa ajali ya pikipiki, mwizi kuuawa na wananchi na nyingine kuokotwa ufukweni mwa bahari ikiwa imefungwa kamba mikononi na kukatwa panga kisogoni.
“Mimi, baba pamoja na shemeji yangu tuliingia mochwari kuthibitisha. Tulipofika katika maiti iliyofungwa kamba na kukatwa panga kisogoni wote tulijiridhisha kuwa ndiye yeye kutokana na alama alizokuwa nazo, sikujua kilichoendelea, naamini nilipoteza fahamu baada ya kuuona mwili huo.
“Tulirudi nyumbani kuandaa msiba, kuweka maturubai, kununua sanda na kuandaa jeneza, tulipiga simu sehemu mbalimbali hadi mikoani kuwajulisha ndugu.“Tulijiandaa ili ndugu wa Morogoro na mikoa mingine wakija katika mazishi yaliyotarajiwa kufanyika kesho Ijumaa (iliyopita) katika makaburi ya hapa Tandale ambapo tulishapewa eneo la kuchimba kaburi.
Kijana Mohamed Salum ‘Fido’ anayesadikiwa kuwa alikufa akila.
“Kweli sijui nisemeje, tuliwataka radhi waombolezaji kwa usumbufu, baadhi walitawanyika kwa wakati huo wengine waliendelea kuwepo hata ndugu zetu wengine wako njiani wakitokea Mbeya na Mtwara.”